Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts

Monday, April 22, 2013

RAIS TENGA ATOA MIPIRA YENYE THAMANI YA DOLA 30,000


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametoa mipira zaidi ya 1,200 yenye thamani ya dola 30,000 za Marekani kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na vituo 21 vilivyo hai vya kuendeleza vijana (academies).

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) lilimpa Rais Tenga fedha hizo ikiwa ni shukrani kwake kwa kushughulikia mgogoro wa uongozi wa mpira wa miguu nchini Kenya uliodumu kwa miaka miwili; ambapo nchi hiyo kutokana na mgogoro huo ilikuwa na vyama viwili (KFF na FKL).
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mipira hiyo kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam leo (Aprili 22 mwaka huu), Rais Tenga amesema amefanya hivyo kwa vile anaamini kuwa mipira ndiyo kitu muhimu katika kuinua mchezo huo mahali popote.

“Dhamira yangi si kushukuru kwa hafla hii, bali kutoa sababu kwa nini nimefanya hivi. Ninaamini kwa kuanzia mipira ndiyo muhimu, pili kwa kufanya hivi itaonekana kweli mipira imegawiwa,” amesema Rais Tenga.

Amesema amesema mpira wa miguu kwa Tanzania unahitaji sana watu wa kujitolea, na yeye amefanya hivyo kwa kujitolea kutokana na ukweli shughuli anazotumwa na FIFA ni za kujitolea.
Rais Tenga ambaye pia alitumwa na FIFA kutatua matatizo ya uongozi wa mpira wa miguu katika nchi za Uganda, Zambia na Sudan Kusini amesema anaamini anapata fursa hizo kutokana na kuwa kiongozi wa TFF, na kwa kuwakumbuka waliomchagua ndiyo maana hakusita kupeleka fedha hizo kwenye mipira.

Amesema moja ya ndoto zake wakati anaingia kuongoza TFF mwaka 2004 ameshindwa kutimiza ni kusaidia mipira, kwani uwezo wa kununua mipira kwa wanaocheza katika ngazi ya chini hasa watoto haupo.

“Hizi kelele zote za maendeleo ya mpira wa miguu ni kwa sababu shuleni hakuna vifaa. Nia yangu ilikuwa shule zote zipate mipira, lakini hiyo ni moja ya ndoto nilizoshindwa kutekeleza. Vipaji haziwezi kupatikana kama watoto hawachezi.

“Tunashukuru sana kwa Serikali kurejesha mpira shuleni. Hata nitakapoondoka madarakani nikipata nafasi nitaendelea kuomba mipira kwa ajili ya shule,” amesema Rais Tenga.

Vyama vya mikoa ambavyo jumla ni 32 (Tanzania Bara na Zanzibar) kila kimoja kimekabidhiwa mipira 25 (kumi saizi namba tano, 15 saizi namba nne kwa ajili ya vijana). Kwa academies ambazo ni 21 kila moja imepewa mipira 25 (minane saizi namba tano, na 15 saizi namba nne).

Viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Almasi Kasongo, Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) Nassib Mabrouk na Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Riziki Majala.

Kwa upande wa shule alikuwa Kanali mstaafu Idd Kipingu ambaye ni mmiliki wa shule ya Lord Baden ya Bagamoyo mkoani Pwani. 

CHANZO:TFF

Sunday, April 21, 2013

NJIA YA YANGA KUTWAA UBINGWA WA LIGI KUU YAZIDI KUTAKATA,YAILAZA JKT RUVU 3-0

Fuatana nami ujue nini kilikuwa kinatokea hatu kwa hatua kama ifuatavyo:-
Mpira unamalizika Yanga 3 - 0 JKT

Dk 90+4 Mgosi anachezewa faulo na Yondani nje kidogo ya eneo la hatari la Yanga. Faulo inapigwa na mpira unaokolewa na kuwa kona. Yanga 3-0 JKT

Dk 90+1 Nizar anapiga shuti kali linalopanguliwa na kipa wa JKT, Dihile.

Dk 89 Mwamuzi wa akiba Idd Soud anaonyesha bango kwa mpira umeongezwa dakika 5

Mara yangu ya mwisho kumuona Said Mohamed kwenye uwanja huu ni mwaka jana alipoingia kama sub kuchukua nafasi ya Yaw Berko kwenye mchezo ambao yanga walifungwa mabao 5:0 na Simba

Dk 86 Yanga inafanya mabadiliko ametoka Barthez ameingia Said Mohamed.
Dk 86 Inaonekana Barthez hawezi kuendelea na Said Mohamed anapasha misuli moto kujiandaa kuingia.

Dk 84 Kipa wa Yanga, Barthez anaanguka mwenyewe na mpira unaendelea kusimama ili Barthez atibiwe.

Dk 83 Mpira unasimama kwa muda baada ya Msuva kuchezewa rafu na Zahor Pazi. Yanga 3-0 JKT.

Dk 80 Jerry Tegete anaingia badala ya Hamis Kiiza

Dk 78 JKT wanafanya mabadiliko ametoka Ally Mkanga ameingia Charles Thadei.

Dk 76 JKT wamefanya mabadiliko ametoka Hassan Kikutwa ameingia Sosthenes Manyasi.

Dk 76 JKT wamefanya mabadiliko ametoka Hassan Kikutwa ameingia Sosthenes Manyasi.

Dk 75 Chuji wa Yanga anamchezea faulo Hussein Bunu wa JKT.

Dk 73 Msuva anachezewa faulo na Nashon Naftal nje kidogo ya eneo la hatari la JKT. Faulo inapigwa JKT wanaokoa. Yanga 3-0 JKT

Leo Yanga wametoa burudani kwa mashabiki walioingia uwanjani kwa soka safi

Shuti kali la Chuji linadakwa na kipa wa JKT

Goaaaaaaaaaaaal Nizar Khalfan anaipatia Yanga goli la 3

Dk 62 Mgosi anachezewa faulo na Kelvin Yondani.

JKT wanafanya mabadiliko anatoka Amos Mgisa anaingia Abdallah Bunu

Gooooooooal Free kick iliyopigwa na luhende imeunganishwa na Hamis Kiiza kwa kichwa

Dk 57 yanga wanapata faulo baaada ya Msuva kufanyiwa madhambi

Dk 55 Ally Nkanga analimwa kadi ya njano baada ya kumfanyia madhambi Nizar

Dk 53 Kiiza wa Yanga anashindwa kuunga vizuri pasi ya Domayo kwa shuti lake kutoka nje ya eneo la hatari la JKT.

Dk 49 JKT wanapiga kona na Yanga wanaokoa.

Dk 49 JKT wanapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari. Faulo inapigwa lakini Cannavaro anautoa nje mpira na kuwa kona.

Dk 48 Mgosi anapiga shuti hafifu na Barthez anaudaka mpira.

Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, JKT Ruvu 0 - 1 Young Africans

Dk 45 HALF TIME! Yanga 1-0 JKT

Simon Msuva anaipatia yanga bao hapa

Dk 41 Stanley Nkomola anapiga kona lakini kipa Barthez anaokoa.

Dk 39 Mgosi anamchezea faulo Cannavaro.

Dk 36 JKT wanapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Yanga. Faulo inapigwa na mabeki wa Yanga wanaokoa.

Dk35 Hamis kiiza anakosa bao la wazi

Dk 31 Yanga inapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari la JKT. David Luhende anamtengea Haruna Niyonzima lakini shuti lake linawababatiza mabeki wa JKT na mpira unaokolewa.

Dk 30 yanga wanapata kona nyingine Dihile anaokoa

Dk 26 Kwa mara ya tatu ndani ya dakika nne zilizopita mabeki wa Yanga wanamwekea Mgosi mtego wa kuotea naye anashindwa kung'amua hali hiyo na mara nyingi anajikuta akiwa ameotea.

Dk 26 Kwa mara ya tatu ndani ya dakika nne zilizopita mabeki wa Yanga wanamwekea Mgosi mtego wa kuotea naye anashindwa kung'amua hali hiyo na mara nyingi anajikuta akiwa ameotea.

Dk 24 Mussa Mgosi wa JKT anaipangua ngome ya Yanga lakini shuti lake linadakwa na kipa Ally Mustapha 'Barthez'.

Almanusura Nadir aipatie yanga bao kutokana na faulo ya Luhende

Dk 22 yanga wanapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari

Dk 19 Athuman Idd Chuji wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa JKT lakini mpira unatoka nje kidogo ya lango.

Dk 18 Zahor Pazi wa JKT anachezewa faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Yanga. Faulo inapigwa lakini mpira unatoka nje.

Dk 16 Yanga wanapata kona baada ya Damas Makwaya kuutoa nje mpira. Kona inapigwa na Dihile anaudaka mpira.

Dk 15 Kipa Dihile wa JKT anaudaka mpira wa krosi uliokuwa ukiwaniwa na Kiiza.

Dk 13 JKT wameanza kumiliki mpira na kuisumbua ngome ya Yanga. Yanga 0-0 JKT

Dk 12 Yanga inapata kona lakini kipa wa JKT, Shaaban Dihile anaudaka mpira.

Dk 10 Hamis Kiiza wa Yanga anamiliki mpira vizuri akipokea pasi ya Frank Domayo lakini mwamuzi Oden Mbaga anasema Kiiza ameoteaM

Yanga wanacheza vizuri sana hasa kwenye eneo la kiungo.

Dk 8 Mbuyu Twite wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa JKT lakini mpira unatoka juu kidogo ya mlingoti.

DIHILE AMENYANYUKA ANAPIGA FAULO

Shambulio hilo limesababisha golikipa wa JKT Dihile kuumia yupo chini anatibiwa

Dk ya tatu kona ya Luhende imesababisha kizaazaa kwenye lango la jkt ruvu

Yanga wanapata kona na inapigwa na David Luhende

Musa mgosi anamlazimisha Cannavari kuutoa nje mnamo dk 2

Mpira umeanza hapa taifa Yanga SC 0-0 JKT

Muda wowote kuanzia sasa soka litaanza na yanga ndo wanaanzisha kipute

Makame Rashid alifariki mwanzoni mwa juma hili,alikuwa mdau mkubwa wa soka

Wachezaji wanasimama kuomboleza kifo Makame rashid

JKT Ruvu line up: Shabani Dihile, Hassan Kikutwa, Stanley Mkomola, Madenge Ramadhan, Damas Makwaya, Nashon Naftar, Amos Mgisa, Ally Mkanga, Mussa Mgosi, Zahor Pazi na Haruna Adolph.


Kikosi cha Yanga

1.Ally Mustafa 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.David Luhende
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6. Athunman Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Hamis Kiiza
10.Nizar Khalfani
11.Haruna Niyonzima


Subs:
1.Said Mohamed
2.Shadrack Nsajigwa
3.Oscar Joshua
4.Salum Telela
5.Nurdin Bakari
6.Said Bahanuzi
7.Jerson Tegete
 
CHANZO,SHAFII DAUDA

Saturday, April 20, 2013

AZAM YABANWA MBAVU NYUMBANI NA RABAT

 AZAM FC imelazimishwa sare ya bila kufungana jioni hii na AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu, Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yanaifanya Azam iwe na mtihani mgumu katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo Morocco, wakitakiwa lazima kushinda au kutoa sare ya mabao ili kufuzu.



Pamoja na sare hiyo, Azam watakumbuka sana mabao matatu ya wazi waliyokosa kupitia kwa washambuliaji wao wa pembeni, Kipre Herman Tchetche mawili na Khamis Mcha ‘Vialli’ moja,
Kipre aligongesha mwamba mashuti mawili katika dakika za 51 pembeni kushoto katikati  na dakika ya 90+1 mwamba wa juu katikati baada ya jitihada za kuwatoka mabeki wa AS FAR Rabat.


Khamis Mcha naye alimtoka vizuri beki wa pembeni wa AS FAR Rabat dakika ya 52 lakini akapiga nje shuti lake.


Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Emile Fred wa Shelisheli, aliyesaidiwa na nduguze Steve Maire na Jean Ernesta pembeni, kipindi cha kwanza Azam walionekana kucheza kwa tahadhari zaidi na kufanya mashambulizi machache.


Lakini kipindi cha pili, walifunguka na kuanza kushambulia moja kwa moja jambo ambalo liliweka kwenye misukosuko lango la AS FAR Rabat kwa muda mrefu hadi wachezaji wa timu hiyo kuanza kufanya hila za kupoteza muda ili kupunguza kasi ya wenyeji.


John Raphael Bocco ‘Adebayor’ naye alilitia misukosuko mara kadhaa lango la wageni kila ilipoingizwa mipira ya juu kutokea pembeni hususan kona japokuwa alikuwa chini ya ulinzi mkali leo.


Kikosi cha Azam FC leo kilikuwa
; Mwadini Ally, Himid Mao, Waziri Salum, David Mwantika, Joackins Atudo/Luckson Kakolaki dk7, Kipre Balou, Kipre Tchetche, Salum Abubakar, John Bocco ‘Adebayor’, Humphrey Mieno na Kahmis Mcha ‘Vialli’/Mwaikimba dk78.


AS FAR Rabat; Ali Grouni, Mustafa Mrani, Younes Hammal, Younes Belakhdar, Yassine El Kordy, Abdelrahim Achchakir/Mostafa El yousfi dk74, Salaheddine Said, Mohamed El Bakkali, Salaheddine Aqqal/Souffiane Alloudi dk80, Mustafa Allaoui na Hicham El Fathi/Youssef Anouar dk69.

Friday, April 19, 2013

LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KUANZA MEI 12,2013

 Ligi ya Mabingwa wa Mikoa kutafuta timu tatu zitakazopanda kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao chini ya usimamizi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itaanza Mei 12 mwaka huu.

Mwisho wa mikoa kuwasilisha majina ya mabingwa wao ni Mei 1 mwaka huu wakati ratiba ya ligi hiyo itapangwa mbele ya waandishi wa habari Mei 3 mwaka huu kwenye ofisi za TFF.

Uwasilishaji wa jina la bingwa wa mkoa unatakiwa kufanyika pamoja na ulipaji ada ya ushiriki ambayo ni sh. 100,000. Mfumo wa ligi hiyo ni bingwa wa mkoa X kucheza na bingwa wa mkoa Y nyumbani na ugenini ambapo mshindi ndiye anayesonga mbele katika hatua inayofuata.

Usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika katika hatua ya mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho. TFF inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi hiyo.

NANI KUWA MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA ENGLAND KATI YA VAN PERSIE, BALE, SUAREZ, CARRICK, HAZARD NA MATA ???

Leo imetangazwa rasmi orodha ya wachezaji ambao wanagombania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa ligi kuu ya Uingereza - Man United imetoa wachezaji wawili, kiungo Micheal Carrick  na Robin Van Persie, Luis Suarez anaiwakilisha Liverpool, Gareth Bale, Juan Mata na Eden Hazard wakiliwakilisha jiji la london. Mabingwa watetezi Manchester City hawajatoa mchezaji hata mmoja katika listi hiyo iliyotangazwa leo.

Orodha yenyewe ni:-
Michael Carrick (Manchester United)
Gareth Bale (Tottenham Hotspur)
Robin van Persie (Manchester United)
Luis Suarez (Liverpool)
Eden Hazard (Chelsea)
Juan Mata (Chelsea)


Washindi wa miaka iliyopita

2011-12: Robin van Persie (Arsenal)
2010-11: Gareth Bale (Tottenham)
2009-10: Wayne Rooney (Man Utd)
2008-09: Ryan Giggs (Man Utd)
2007-08: C Ronaldo (Man Utd)

Thursday, April 18, 2013

REAL MADRID KLABU TAJIRI DUNIANI, YA PILI MAN UNITED

 Manchester United wameondolewa kwenye nafasi ya kwanza ya klabu yenye utajiri na thamani kubwa inayotolewa na jarida la Forbes.

United wamekuwa wakishika nafasi ya kwanza kila mwaka tangu Forbes walipoanza kutoa list ya vilabu vye thamani kubwa zaidi duniani mwaka 2004, lakini mwaka huu wameondolewa kileleni na Real Madrid - klabu ambayo iliitoa kwenye michuano ya champions league hive karibuni.

Barcelona wanashika nafasi ya tatu nyuma ya United, Arsenal wapo nafasi ya nne na mabingwa wa Bundesliga Bayern Munich wakikamilisha nafasi ya tano.

Real Madrid wanatajwa kuwa na thamani ya £2.15billion - na kwa namba hizo klabu hiyo ya Spain inakuwa ndio klabu ya michezo yenye thamani kubwa zaidi duniani - huku Manchester United wakiwa na thamani ya  £2.07billion.

Kwa upande wa wachezaji wa soka, David Beckham bado anaongoza kwa utajiri akiwa ameingiza kiasi cha kati ya £33m - £29m ambazo zimetokana zaidi na mikataba ya kibiashara ya matangazo.

Staa wa Real Madrid Ronaldo ameingiza kiasi cha (£28.8m) akishika nafasi ya pili, wakati mwanasoka bora wa dunia Lionel Mess akishika nafasi ya 3 kwa kuingiza jumla ya £26m mwaka jana kwa kupitia mshahara na mikataba ya kibiashara.

MAKOCHA WA AZAM, FAR RABAT KUNENA KESHO



Makocha wa timu za Azam, Stewart John Hall na AS FAR Rabat ya Morocco, Abderazzak Khairi watakutana na waandishi wa habari kesho (Aprili 19 mwaka huu) kuzungumzia mechi yao itakayofanyika Jumamosi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mkutano huo ambao pia utawahusisha manahodha wa timu hizo mbili utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Barabara ya Uhuru na Shaurimoyo.

Timu hizo zitakutana katika mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho itakayoanza saa 10 kamili jioni. Mechi ya marudiano itachezwa nchini Morocco wiki mbili baadaye.

Tuesday, April 16, 2013

SERIKALI YAMTEUA MOHAMED DEWJI KUIONGOZA KAMATI YA USHINDI YA TAIFA STARS.


Mohamed Dewji.
 Katika kuhakikisha kuwa Taifa stars inafuzu na kushiri fainali za kombe la Dunia huko Brazil, Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo imeteua kamati ya Ushindi kama ifuatavyo:-

"Kama mnavyofahamu, hivi sasa Timu ya Taifa ya mpira wa Miguu kwa Wanaume (Taifa Stars) ipo kwenye michuano ya kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwaka 2014.
Katika Afrika, Tanzania (Taifa Stars) imepangwa kundi C kati ya makundi 10. Kundi C linajumuisha timu za Ivory Coast, Morocco, Gambia na Tanzania.
Kwa sasa katika kundi C, Taifa Stars inashika nafasi ya pili ikiwa na alama sita (6), nyuma ya Ivory Coast yenye alama saba (7), Morocco ina alama mbili (2) na Gambia ina alama moja(1).
Kwa mara nyingine Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inapenda kuwapongeza Taifa Stars, kwa kazi nzuri ambayo wameishaifanya ikiwemo ushindi wa Bao Tatu kwa Moja dhidi yaMorocco. Watanzania wote na Wadau wa Soka nchini wamefurahishwasanana mafanikio yaliyofikiwa na Taifa Stars na yenye kutupa matumaini  katika kuitayarisha Taifa Stars kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia  kwa mwaka 2014 nchiniBrazil.
Kwa hali ilivyo hivi sasa, Taifa Stars ipo katika nafasi nzuri ya kufuzu. Ili Tanzania tuweze kufuzu, Taifa Stars inatakiwa ishinde mechi zote tatu (3) na kuongoza kundi C na baadae iingie katika Timu kumi (10) bora na kisha zipatikane Timu tano (5) kutoka Afrika ambazo zitakuwa zimefuzu kwenda Brazil katika Fainali za Kombe la Dunia kwa mwaka 2014.  Tunaamini hili linawezekana.
Sasa kwa kuzingatia uzito wa jukumu lililo mbele yetu na kwa Taifa Stars kwa ujumla; Serikali imeunda Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars.
Jukumu la msingi la Kamati tunayoiunda ni kuhakikisha Taifa Stars inawezeshwa na kuandaliwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuunda kikundi cha kuishangilia timu ya Taifa ndani na nje ya nchi. Wajumbe wa Kamati ya Taifa Stars Stars itakayoongozwa na Mhe. Mohamed Dewji ni hawa wafuatao:-
 1. Mhe Mohamed Dewji           -       Mbunge
2. Bi. Teddy Mapunda             -       Montage
3. Dkt. Ramadhani Dau           -       Mkurugenzi Mtendaji NSSF
4. Bw. Dioniz Malinzi               -       Mwenyekiti BMT
5. Bw. Abji Shabir                  -       New Africa Hotel
6. Bw. George Kavishe            -       TBL
7. Mhe. Mohamed Raza           -       Zanzibar
8. Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
9. Bw. Joseph Kusaga             -       Clouds
10. Mhe. Kapt. John Komba    -       Mbunge
11. Mhe. Zitto Kabwe             -       Mbunge
Kamati hii iliyoteuliwa leo, naomba ianze kazi mara moja.  Hadidu za rejea zitakazowaongoza kutekeleza majukumu yao chini ya Kamati hii watazipata kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Kamati itashirikisha wadau mbalimbali kadri itakavyoona inafaa.
Serikali inaahidi kutoa ushirikiano utakaohitajika katika kuhakikisha Kamati hii inafanya kazi vizuri ili kuiwezesha Taifa Stars kushinda Mechi zote zilizombele yetu.
Aidha nichukue fursa hii kutoa wito kwa Watanzania wote, kuiunga mkono Taifa Stars na Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars kwa hali namalikatika kuhakikisha timu yetu inafuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia.
Kwa niaba ya Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu naomba niwasilishe salaam zao za kuwapongeza Vijana wetu wa Taifa Stars, pamoja na benchi la ufundi likiongozwa na Kocha Mkuu Kim Poulsen. Kwa pamoja wanaomba Taifa Stars iendelee kujipanga kwa mechi zijazo.  Nawahakikishia kuwa Serikali, Watanzania na wadau wa Soka nchini wapo nyuma yao.

Mungu Ibariki Taifa Stars.
Mungu Ibariki Tanzania.
Dkt. Fenella Mukangara (Mb)
WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
16 Aprili, 2013"

Saturday, April 13, 2013

YANGA YAIVUA RASMI SIMBA UBINGWA WA LIGI KUU YA VODACOM NA KUICHAPA OLJORO 3

 Katika mchezo wa ligi kuu ya vodacom kati ya Yanga na JKT Oljoro uliomalizika muda si mrefu Yanga imeshinda kwa jumla ya magoli 3 na oljoro hawakupata kitu.
Goli la kwanza la lilifungwa dakika ya 5 na nahodha Nurdin Kanavaro,goli la pili limefungwa na Simon Msuva dakika ya 19 na la tatu limefungwa na Hamis Kiiza dakika ya 34.

MATATIZO YA KIUFUNDI YASABABISHA KUTOONESHWA "LIVE" MECHI ZA LIGI KUU TANZANIA BARA LEO

 
Afisa Habari wa TFF Boniface Wambura
Kutokana na habari aliyoitoa Afisa Habari wa TFF, ni kwamba  mechi zilizokuwa zioneshwe hii leo na kesho hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.Taarifa kamili hii hapa:-

"Mechi tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.
Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)"

Friday, April 12, 2013

UKWELI KUHUSU LADY JAYDEE KUANZISHA KITUO CHA REDIO


Kutokana na uvumi na taarifa mbali mbali kuhusu mpango wa Lady Jaydee kuanzisha kituo cha redio kiitwacho KWANZA FM leo mhusika (Jidee) kaweka mambo hazarani na kusema kuwa kwanza taarifa hizo zilikuwa ni uzushi kutokana na tarehe hiyo zilipotoka kuwa ni siku ya wajinga.

Ameweka bayana maneno hayo usiku wa leo wakati akifanya mahojiano (Interview) katika kituo cha televisheni cha Channel ten. Mahojiano hayo yalikuwa ni kati ya Jay dee na Dj Tass. Lakini lady Jaydee amesema kutokana na mwitikio aliouona kwa watu ameamua kuwa na mpango huo wa kuanzisha kituo hicho cha redio.

Kuhusu wimbo wake wa Joto hasira, amesema ameutunga na kuuimba kwa kumlenga mtu ambaye hakuwa tayari kumtaja.

UJUMBE WA FIFA KUSHUGHULIKIA UCHAGUZI WA TFF KUWASILI APRILI 15

 TANGAZO TOKA TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwatangazia wadau wa mpira wa miguu kuwa ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utawasili nchini Jumatatu (Aprili 15 mwaka huu) kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka FIFA, ujumbe huo utaongozwa na Mkuu wa Idara ya Uanachama ya FIFA, Primo Covarro na utafanya kazi kwa siku tatu kuanzia siku ya ujio na kuondoka Aprili 18 mwaka huu.
Ukiwa nchini, ujumbe huo utakutana na wagombea uongozi walioathiriwa na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ambao waliomba mashauri yao yaangaliwe upya, wagombea ambao walikata rufani FIFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya Rufani na Sekretarieti ya TFF.
Wajumbe hao wangependa kukutana na waziri anayehusika na michezo, hivyo TFF imeiandikia Wizara ikipendekeza kuwa ujumbe huo ukutane na Waziri na wakuu wengine wa michezo Aprili 16 mwaka huu 2013 kabla ya kuanza kazi zao.
Wagombea watakaosikilizwa na ujumbe huo wa FIFA ni:
1.   Farid Salim Mbaraka Nahdi: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alienguliwa na Kamati ya Uchaguzi na baadaye rufani yake kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kutupwa na hali kadhalika ombi lake la kutaka shauri lake liangaliwe upya, kukataliwa.
2.   Elliud Peter Mvella: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kukata rufani Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kabla ya maombi yake ya kutaka shauri lake kuangaliwa upya, kukataliwa.
3.   Mbasha Matutu: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi na kukata rufani ambayo pia ilitupwa kabla ya kuomba shauri lake liangaliwe upya, ombi ambalo lilikataliwa.
4.   Hamad Yahya: Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ligi ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na kuondolewa. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ikatupa ombi lake.
5.   Jamal Emily Malinzi: Mgombea wa nafasi ya urais wa TFF ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, hivyo kuondolewa kwenye mchakato. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini likakataliwa. Hata hivyo, alikuwa ameshakata rufani FIFA.
6.   Michael Wambura: Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na rufani yake kukataliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF. Hakuomba shauri lake liangaliwe upya, lakini alikata rufani FIFA.
Shirikisho linawaomba wote waliotajwa hapo juu kujiandaa kwa utetezi na maelezo ya kutosha na kwamba barua za kuwaita zinafuata.

BARCELONA vs BAYERN MUNCHEN, REAL MADRID vs BORRUSIA DOTTIMOND


"The best of Spain face the best of Germany in the semi-finals after today's draw paired FC Bayern München with FC Barcelona and pitted Borussia Dortmund against Real Madrid CF."

Haya ni maneno yaliyokutwa kwenye Website ya UEFA baada ya kupanga ratiba ya nusu finali ya Kombe la UEFA.

Thursday, April 11, 2013

TAIFA STARS YAPANDA NAFASI 3 VIWANGO VYA SOKA DUNIANI.

Kocha mkuu wa Taifa stars Kim Poulsen
Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa stars imepanda nafasi 3 katika viwango vya soka Duniani.
Katika ukanda wa Afrika,Timu ya kwanza ni Ivery Coast ikishika nafasi ya 12 Duniani na Afrika Mashariki,bado timu ya Uganda inaongoza ikiwa ya 92 duniani.
Duniani timu 10 Bora ni:- 1. Hispania, 2.Ujerumani, 3.Ajentina, 4.Koratia 5.Ureno, 6.Korombia,7.Uingereza, 8.Italia, 9.Uholanzi na 10.Ekwado.


Rnk
Team
Pts
+/- Pos


1
Spain
1538
0
Equal


2
Germany
1428
0
Equal


3
Argentina
1292
0
Equal


4
Croatia
1191
5
Up


5
Portugal
1163
2
Up


6
Colombia
1154
0
Equal


7
England
1135
-3
Down


8
Italy
1117
-3
Down


9
Netherlands
1093
-1
Down


10
Ecuador
1056
1
Up


11
Russia
1052
-1
Down


12
Côte d'Ivoire
1008
1
Up


13
Greece
986
-1
Down



92
Uganda
413
-7
Down


93
Estonia
411
-4
Down


94
Angola
401
1
Up


94
Guatemala
401
-3
Down


96
Dominican Republic
396
0
Equal


96
Iraq
396
-2
Down


98
China PR
388
11
Up


99
Benin
381
-13
Down


100
Niger
362
-7
Down


101
Zimbabwe
349
-1
Down


102
Qatar
346
-4
Down


103
Oman
344
2
Up


104
Liberia
334
14
Up


105
New Caledonia
333
-2
Down


106
Mozambique
330
1
Up


107
Ethiopia
328
5
Up


108
Saudi Arabia
324
-2
Down


109
Malawi
323
2
Up


110
Latvia
322
-2
Down


111
Lithuania
316
4
Up


112
Tajikistan
312
40
Up


113
Kuwait
311
0
Equal


113
Suriname
311
-3
Down


115
Korea DPR
310
-13
Down


116
Tanzania
305
3
Up


117
Bahrain
291
0
Equal
 

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...