Friday, February 1, 2013

BREAKING NEWS: MVUA ZALETA MAAFA MJINI MOROGORO

Barabara Morogoro ikiwa imejaa maji

Mvua zinazoendelea kunyesha mjini Morogoro zinazidi kuleta maafa baada mvua zilizonyesh usiku wa leo zimewaathiri wakazi wa hapa baada ya nyumba kujaa maji na baadhi ya barabara kufungwa kutokana na kujaa maji.
Maji yakiwa yamejaa barabarani eneo la Mtawala karibu na uwanja wa Shujaa


Magari yakiwa yanajiuliza namna ya kupita katika barabara Uwanja wa Shujaa.

Tatizo hili limeweza kuzikumba na baadhi ya Ofisi za Serikali ambapo katika ofisi za MORUWASA na Ofisi za Bonde la Wami/Ruvu maji yalijaa getini kiasi cha wafanyakazi wenye magari kushindwa kupita na kusubiri maji yapungue.

Geti la ofisi za MORUWASA na Bonde la Wami/Ruvu likiwa limejaa maji.


No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...