Monday, February 11, 2013

BREAKING NEWS: MAPIGANO YA KIDINI YAPOTEZA MAISHA YA RAIA BUSELESELE GEITA

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa kumezuka mapigano kati ya Waislam na Wakristu huko Geita .Inadaiwa katika machafuko hayo,mtu mmoja amepoteza maisha kufuatia sakata la uchinjaji nyama ambapo inasemekana wachungaji wa kanisa la AIC wamewatangazia waumini wake kutokula nyama inayochinjwa na Waislam na kwamba leo wakristo wa eneo la Buselesele wamefungua Mabucha yao na kuanza kuuza nyama. Tutaendelea kuwapasha habari zaidi kadri tutakavyokuwa tunazipata habari.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...