Thursday, May 30, 2013

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE. EZEKIAH DIBOGO WENJE (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014

1.0 UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika bajeti ya wizara hii mwaka 2012/13, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA ilibaini mapungufu mengi ya kiutendaji na kiuwajibikaji katika wizara hii, na hivyo kuitaka Serikali  kufanya mambo yafuatayo ili kuboresha utendaji na ufanisi:
1.      Kuziwezesha balozi zetu nje kwa kuzitengea fedha za kutosha  ili ziweze kufanya kazi kwa ufanisi
2.      Kutoa idadi ya majengo ya balozi zetu nje (nyumba za mabalozi, nyumba za maafisa wa balozi na ofisi za balozi) kwa mchanganuo wa idadi ya nyumba katika nchi na kama nyumba hizo zina hati miliki au la.
3.      Kutoa taarifa ya namna kila ubalozi ulivyotekeleza sera ya Diplomasia ya uchumi kwa kuzingatia kwamba balozi nyingi ziko hoi kifedha kiasi cha kwamba waambata wa kiuchumi wanakosa fedha za kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa ajili ya upelelezi wa masuala ya kiuchumi.
4.      Kulikarabati jengo la ubalozi wa Tanzania huko Msumbiji lililokuwa limechakaa kwa kutofanyiwa ukarabati tangu 1975 ingawa jengo hilo tulipewa bure na Serikali ya Msumbiji chini ya FRELIMO.
5.      Kujenga kitega uchumi katika kiwanja  cha Tanzania kilichopo Dubai na kukiendeleza kiwanja namba 19  tulichopewa bure na Serikali ya Uingereza kilichopo Uingereza (Central London) ambavyo vimekuwa maficho ya wezi kwa kutoendelezwa kwa muda mrefu na kusababisha Serikali za nchi hizo kutaka kutaifisha viwanja hivyo.
6.      Kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma za balozi zetu nchini China, na Uingereza kutoa hati za kusafiria kwa mataifa mengine hasa ya Afrika Magharibi ili kubaini ukweli na kuliondolea taifa aibu kutokana na tuhuma hizi.
7.      Kukarabati jengo la ubalozi wetu nchini China ambalo lilikuwa na nyufa na kuvuja nyakati za mvua, na kununua samani  na vifaa vya ofisi kama mashine za nukushi na za kurudufu ambazo zilikuwa hazipo,
8.      Kununua magari mapya ya ofisi ya ubalozi wetu nchini China kwa kuwa  magari matatu yaliyokuwepoyalikuwa yameshapitiliza muda wa miaka 10 ambao kwa mujibu wa sheria za China hayapaswi kutumika tena,
9.      Kupeleka mwambata wa kiuchumi (economic attaché)  nchini China ili kufuatilia fursa mbalimbali za kiuchumi katika kutekeleza diplomasia ya uchumi kutokana na mahusiano makubwa ya kibiashara  kati ya nchi yetu  na China
10.  Kuwawekea zuio wahusika wa kashfa ya rada kuwa viongozi wa shughuli za kiserekali ili walau kuonesha uwajibikaji wa kimaadili (moral accountability) baada ya kushindwa kuwawajibisha kisheria, ili kuondoa dhana iliyojengeka miongoni mwa jamii kwamba dola imetekwa na mafisadi.
11.  Kuchunguza na kuwachukulia hatua watanzania (wafanyabiashara na wanasiasa) waliotorosha kiasi kikubwa cha fedha za nchi yetu (zaidi ya shilingi bilioni 315) na kuzificha katika mabenki ya uswisi
12.  Kutoa mchanganuo wa jinsi fedha za rushwa ya rada (chenji ya rada) zilivyotumika
13.  Kueleza bayana faida za kiuchumi tunazopata kama taifa kwa kushirikiana na jumuiya mbalimbali za kimataifa ili kuthibitisha kwamba mashirikiano hayo hayatumiki kupora rasilimali za nchi yetu kwa hila ya “uwekezaji”
Mheshimiwa Spika, kabla sijajielekeza kwenye mambo mahsusi kwa kipindi hiki cha bajeti ya 2013/2014, napenda kuchukua nafasi hii kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA, kuitaka Serikali kutoa majibu mbele ya Bunge hili tukufu, kwamba imetekeleza kwa kiwango gani masuala yaliyoorodheshwa hapo juu, tuliyoitaka iyatekeleze (moja baada ya jingine) kwa mwaka wa fedha unaomalizika wa 2012/2013?


BALOZI BISWARO AWAPA CHANGAMOTO STARS.


Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Joram Biswaro amewataka wachezaji wa Taifa Stars kuhakikisha wanaipeleka timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.

Ametoa changamoto hiyo wakati alipotembelea mazoezi ya timu hiyo jana (Mei 29 mwaka huu). Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imepiga kambi nchini Ethiopia na inafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Addis Ababa.

“Watanzania tunafurahi kutokana na uwezo mnaouonyesha, hasa baada ya kuifunga Morocco mabao 3-1. Kama mliwafunga nyumbani hata kwao mnaweza kuwafunga. Tunataka kuwaona Maracana (Brazil) mwakani, mimi tayari ninayo tiketi mtanikuta kule,” amesema Balozi Biswaro ambaye enzi zake aliwahi kuichezea timu ya Yanga.

Taifa Stars ambayo iko Addis Ababa tangu Jumatatu (Mei 27 mwaka huu) imeweka kambi katika hoteli ya Hilton ambapo Jumapili (Juni 2 mwaka huu) itacheza mechi ya kirafiki na Sudan (Nile Crocodile) kwenye Uwanja wa Addis Ababa.

Balozi Biswaro ameikaribisha Taifa Stars ubalozini Addis Ababa mara baada ya mechi dhidi ya Sudan ambapo itakutana na baadhi ya Watanzania wanaoishi Ethiopia kabla ya kuondoka alfajiri kwenda Marrakech, Morocco kwa kupitia Cairo, Misri.

Kocha Kim Poulsen amesema kikosi chake kinaendelea na mazoezi vizuri na kitaimarika zaidi baada ya wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kujiunga nacho Juni 3 mwaka huu jijini Marrakech kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu.

Wachezaji walioko katika kikosi cha Stars jijini Addis Ababa ni Juma Kaseja, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Addis Ababa
+251 919910240

URUSI YAIKABIDHI SYRIA 'ZANA ZA KIVITA'

Syria imepokea ngao za kwanza kutoka kwa Urusi, za kuikinga nchi hiyo dhidi ya mashambulizi ya makombora ya angani. Hii ni kwa mujibu wa rais wa nchi hiyo, Bashar al-Assad.
Urusi imeahidi kuendelea na mpango wake wa kuhami Syria, mara tu baada ya uamuzi wa muungano wa Ulaya wa kuondolea nchi hiyo vikwazo vya silaha.
Bwana Assad pia anaripotiwa kuambia televisheini yenye uhusiano na kundi la Hezbollah, kuwa sasa kumekucha kwani vita ndio vinaanza kushika kasi.
Awali, kiongozi mmoja wa waasi aliambia BBC kuwa Hezbollah imekuwa ikishambalia Syria.
Generali Selim Idriss, kwenye mahojiano na BBC alisema kuwa zaidi ya wapiganaji 7,000 wa kishia kutoka Lebanon, wanashiriki vita dhidi ya utawala wa Syria mjini Qusair, mji ambao unadhibitiwa na waasi.
Mfumo wa S-300 ni wa hali ya juu ambao unaweza kukinga makombora ya angani na ya sakafuni.
Hatua ya Urusi kuikaibidhi Syria zana kama hizo, inazua wasiwasi zaidi hasa baada ya Syria kusema kuwa itajibu mashambulizi yoyote kutoka kwa Israel, msimamo ambao pia umechukuliwa na Urusi.
Wadadisi wanasema kuwa huenda pande zinaojihusisha na mzozo wa Syria zikaanza kutumia makombora kwenye vita hivi.
Pia inahofiwa kuwa mashambulizi ya makombora yanaweza kutishia juhudi za kuandaa mkutano wa amani kuhusu Syria mjini Geneva mwezi Juni.
Waziri wa mambo ya nje wa Syria amesema kuwa majeshi ya nchi hiyo sasa yamerejea katika hali nzuri ya kupambana na waasi.

TAARIFA KWA UMMA: TAHADHARI YA UGONJWA WA NIMONIA.

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
TAARIFA KWA UMMA.
TAHADHARI YA UGONJWA WA NIMONIA INAYOTOKANA NA CORONA VIRUS


Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imepokea taarifa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) mnamo tarehe 22 Mei 2013, kuhusu kuwepo kwa ugonjwa wa Nimonia unaosababishwa na kirusi cha “Novel Coronavirus”.Taarifa hiyo inaeleza kuwa,tangu ugonjwa huo utokee mwishoni wa mwaka 2012 hadi tarehe 23 Mei 2013 idadi ya wagonjwa wapatao 44 na vifo 22 viliripotiwa
Shirika la Afya Duniani limethibitisha ugonjwa huu kuwepo katika nchi za Mashariki ya Kati yaani Jordan, Qatar, Saudi Arabi na Falme za Kiarabu (UAE). Katika bara la Ulaya, ugonjwa huu umethibitishwa kutokea nchi za Ujerumani, Ufaransa, na Uingereza. Katika bara la Afrika, ugonjwa huu umetokea Tunisia.
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa tahadhari ya Ugonjwa huu kwa wananchi wote, katika mikoa yote ya Tanzania na hasa wale wanaosafiri kuelekea maeneo tajwa yenye uthibitisho wa ugonjwa huu.
Ugonjwa huu unaenezwa na kirusi kiitwacho “novel coronavirus (nCoV).”. Dalili kuu za ugonjwa huu ni kushindwa kupumua kwa ghafla, homa kali, kukohoa, na kubanwa na mbavu na hatimaye kupata Nimonia. Dalili nyingine ambazo zinaweza kutokea ni pamoja na kupata maumivu makali ya tumbo pamoja na kuharisha.Vile vile ugonjwa huu unaweza kupelekea figo kushindwa kufanya kazi na hata kusababisha kifo. Kipindi cha kuonekana kwa dalili za ugonjwa huu
ni kati ya siku 2 hadi 10 baada ya kupata maambukizi. Ugonjwa huu hauna tiba wala chanjo.
Ugonjwa huu unaweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Njia za maambukizo bado hazijajulikana ingawa uwezekano mkubwa wa maambukizo ni kwa kwa njia ya hewa (kukohoa/kupiga chafya) au kwa kugusa majimaji/makamasi kutoka kwa mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa huo.
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imechukua hatua zifuatazo katika kukabiliana na tishio la ugonjwa huu:
Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa huu kupitia kwa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya kwa Tanzania bara. Aidha, taarifa hii pia imejumuisha namna mgonjwa anavyoweza kutambuliwa (Ainisho la Ugonjwa), “Fact sheet” ya ugonjwa, Mwongozo kwa watumishi wa afya wa namna ya kuchukua sampuli ikiwa ni pamoja na vipeperushi vinavyoelezea jinsi ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu.
Kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huu kupitia kwa Wataalamu wa Afya katika Mikoa, Wilaya na maeneo ya mipakani. Aidha watalaamu hawa pia wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu dalili za ugonjwa huu na jinsi ya kujikinga na maambukizi ili endapo ugonjwa huo utatokea uweze kutolewa taarifa mapema.
Wizara inasisitiza kuwa hakuna vikwazo vyovyote vilivyowekwa kwa ajili kwa wasafiri watakaokwenda au kurudi katika maeneo tajwa yaliyothibitishwa kuwa na ugonjwa huu. Vipeperushi vya ugonjwa huu vimetumwa katika maeneo ya mipakani ili iwapo msafiri anayeondoka au kurudi nchini akiwa na dalili tajwa atoe taarifa kwa watumishi wa afya wa mpakani ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa.
Kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya na mipakani wa namna ya kutambua na kujikinga dhidi ya maambukizo ya ugonjwa huu pamoja na uchukuaji wa sampuli iwapo mgonjwa atapatikana
Kupeleka vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa afya
Wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu kwani mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyeripotiwa nchini. Wizara inapenda kutoa tahadhari kwa wananchi juu ya umuhimu wa KUNAWA MIKONO VIZURI KWA SABUNI NA MAJI MARA KWA MARA na pia KUZUIA MDOMO NA PUA KWA KITAMBAA AU KARATASI LAINI WAKATI WA KUKOHOA AU KUPIGA CHAFYA.
Pia wananchi wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kilicho karibu mara watakapoona mgonjwa yeyote atakayehisiwa kuwa na dalili za ugonjwa huu.
Imetolewa na;
Nsachris Mwamwaja
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
30/05/2013

TAARIFA KWA UMMA: TAHADHARI YA TISHIO LA MLIPUKO WA UGONJWA WA KUPOOZA (POLIO)

TAARIFA KWA UMMA

TAHADHARI LA TISHIO LA MLIPUKO WA UGONJWA WA KUPOOZA (POLIO)
 
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imepokea taarifa mnamo tarehe 22 Mei 2013 kutoka Shirika la Afya Ulimwenguni, (WHO) ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa wa kupooza (Polio) katika Wilaya ya Fafi nchini Kenya. Mpaka sasa kuna mgonjwa mmoja bila kifo.
 
Ugonjwa wa Polio ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vijulikanavyo kama “Polio Virus”. Ugonjwa huu unaathiri misuli na mfumo wa fahamu hivyo kusabisha kupooza kwa viungo hasa miguu na hata kifo. Ulemavu huu ukishajitokeza huwa ni wa kudumu. Waathirika wakuu wa ugonjwa huu ni watoto hasa walio na umri chini ya miaka mitano. Hata hivyo ugonjwa huu unazuilika kwa chanjo ya Polio ambayo ni salama na inatolewa bure na Serikali katika vituo vyote vya huduma ya afya. Mtoto aliyepata chanjo ya Polio anakuwa amekingwa na ugonjwa wa Polio kwa maisha yake yote.
 
Kutokana na taarifa hiyo ya kutoka nchini jirani ya Kenya, baadhi ya mikoa ina uwezekano mkubwa wa kupata maambukizo ya ugonjwa huo kufuatia ushauri wa kitaalam. Aidha, mikoa hii mingine inapakana na nchi jirani ya Kenya na mingine ina mapungufu yaliyopo katika hali ya chanjo ya Polio. Mikoa hii ni pamoja na Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Mara na Mwanza.
 
 
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imechukua hatua zifuatazo katika kukabiliana na tishio la ugonjwa huu:
 
·        Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa huu kupitia kwa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya.
    
·        Kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huu kupitia kwa Wataalamu wa Afya katika Mikoa, Wilaya na maeneo ya mipaka
 
·        Kufuatilia kwa karibu hali ya chanjo mikoani na wilayani hususan ya Polio hususani iliyo katika hatari ya maambukizi
 
·        Kuhamasisha watoto ambao hawajakamlisha ratiba yao ya chanjo hususani ya Polio au ambao hawajapata ya chanjo hii waweze kwenda vituo vya karibu vya afya vya kutolea chanjo
 
Wizara inapenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa Viongozi na Watendaji wa ngazi zote kutoa ushirikiano ili kuhakikisha kila mtoto mlengwa anapata chanjo ya Polio. Aidha Wizara inatoa rai kwa wadau wetu, taasisi za dini, taasisi zinazofanya kazi katika jamii na vyombo mbalimbali  kuhamasisha watu wapeleke watoto wao kwenye vituo vya huduma wakapewe chanjo hii muhimu. Chanjo hii ni salama na inatolewa bila malipo.
 
 
Wananchi wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu mara wanapoona au kupata taarifa ya mtoto yoyote anayepata ulemavu wa ghafla pasipo sababu yoyote. Mtoto huyo apelekwe katika kituo cha huduma za afya kwa uchunguzi na hatua za haraka.
 
 
 
 
Imetolewa na;
Nsachris Mwamwaaja
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
30/05/2013

Scholarships for High Achieving International Students at RMIT University in Australia, 2013

RMIT university, Australia offers Seventy four international scholarships. These scholarships are awarded to pursue various program at undergraduate and postgraduate level at university in Semester 2 2013 (July intake). Each scholarship worth of  A$3000 will be awarded towards tuition fees. Before applying these scholarships, applicants must apply for admission into one of RMIT program. Applications should be submitted till June 7, 2013.


KINANA NA NAPE WAENDA "BEACH" ZIWA NYASA.

Katibu mkuu wa CCM Kinana na Nape Nnauye wakiwa ziarani mkoani njombe wamekagua ufukwe wa ziwa Nyasa katika mwambao wa ziwa hilo kwenye kijiji cha Lupingu, Wilayani Ludewa, na kuwambia wananchi wasihofu na maneno Malawi kuhusu ziwa hilo, Serikali ipo imara kuwalinda usiku na mchana.





HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MH. JOSEPH O. MBILINYI (MB)

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHESHIMIWA JOSEPH O. MBILINYI (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA KAZI NA AJIRA KWA MWAKA 2013/2014 (Inatolewa chini ya Kanuni ya 99(9) ya kanuni za Bunge toleo la mwaka 2013)

1.0 UTANGULIZI
Mheshimiwa spika, mwaka jana nilianza hotuba yangu kwa kutoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki  wa wale wote waliofariki dunia kwa ajali ya mv skagit, mwaka huu naomba nianze hotuba yangu kwa kutoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki wa wale waliofariki kwa ajali nyingine ya kizembe ya kuanguka kwa ghorofa la Dar Es Salaam. Aidha, mwaka jana nilianza kwa kutoa pole kwa Mh. Joseph selasini kwa kufiwa na baba yake na mwaka huu nianze pia kwa kutoa pole kwa Mh. mchungaji Israel Natse kwa kufiwa na baba yake mzee Yohana Natse. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake , mahali pema peponi.
Mheshimiwa Spika, hakuna ubishi wala ushindani kuwa Serikali yoyote makini duniani huweka sera na mifumo thabiti ya kuhakikisha kuwa ajira za kutosha zinatengenezwa, mazingira ya kazi yanaboreshwa na wafanyakazi wanalipwa ujira na mishahara yenye staha, si tu kwaajili ya kuwawezesha kumudu gharama za maisha, bali pia kuwapa morali wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi kwa maendeleo ya taifa.
Mheshimiwa Spika, napenda kusisitiza kuwa  Taifa lolote duniani ambalo haliwezi kutengeneza ajira na hivyo kuwafanya vijana wake wengi wenye uwezo wa kuajiriwa kuzurura mitaani, na wale walio vyuoni wanashindwa kusoma kwa sababu ya Serikali kushindwa au kupuuza kugharamia masomo yao; sote tunatambua kuwa Taifa hili  limejaliwa rasilimali nyingi za utalii na madini ya thamani, lenye vyanzo vingi vya kodi na mapato, lakini limegubikwa na migogoro mingi, ya mara kwa mara na isiyokwisha, ya wafanyakazi wanaodai haki na mafao yao halali, huku wakiishia kunyamazishwa kwa kauli laini zenye matumaini hewa; Kwa namna yoyote ile taifa hilo, ni kielelezo cha nchi inayoongozwa na Serikali isiyo na vipaumbele, yenye viongozi wasiojali na wanaotekeleza sera wasizozijua au zilizoshindwa.
2.0 MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII
Mheshimiwa Spika, katika Maoni yetu ya mwaka jana, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ilituhumu kwamba Serikali hii ya CCM haiijatekeleza ahadi zake kwa Watanzania kuhusu mifuko ya hifadhi ya jamii kama zilivyotajwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2010 – 2015. Katika Maoni hayo tulidai kwamba ahadi ya “… kurekebisha viwango vya mafao ili visipishane mno haijatekelezwa hadi sasa kwani viwango vya mafao vinavyotolewa na Mifuko mbali mbali ya Hifadhi ya Jamii ni vile vile vya kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010.” Aidha, tulifafanua jinsi ambavyo ahadi ya “… ya kupanua wigo wa kinga ya hifadhi ya jamii ili Watanzania wengi zaidi wafaidike na huduma hiyo nayo haijatekelezwa.” Vile vile, tulionyesha jinsi ambavyo ahadi ya “kuelimisha jamii … juu ya umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa maendeleo ya wafanyakazi na ya nchi kwa ujumla”, nayo haikutekelezwa kwa sababu Serikali yenyewe imekiri kwamba ‘“… bado kuna uelewa mdogo wa masuala ya hifadhi ya jamii kwa watunga sera, waajiri, waajiriwa, wanachama na wananchi kwa ujumla.”’
Mheshimiwa Spika, katika Maoni yetu hayo tulionyesha kwamba ahadi pekee ambayo Serikali hii ya CCM imeitekeleza ni “… kuendelea kutumia fedha za wafanyakazi zilizomo katika Mifuko mbali mbali ya Hifadhi ya Jamii kuwekeza katika miradi ambayo haina manufaa yoyote kwa wafanyakazi wenyewe.” Tulifanya rejea pana ya Taarifa Kuu ya Mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kuhusu Hesabu za Mashirika ya Umma na Taasisi Zingine kwa Mwaka 2010/2011, iliyoonyesha kwamba “… kuna udhaifu mkubwa katika vitega uchumi vinavyosimamiwa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.”
Hivyo, kwa mfano, ukaguzi wa vitega uchumi vya NSSF ulionyesha kwamba licha ya Mfuko huo kuwekeza zaidi shilingi bilioni 269.272 za wafanyakazi katika ujenzi wa Awamu ya Kwanza na ya Pili ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), sio tu Mfuko huo ‘“… ulikuwa haujasaini mkataba na Serikali juu ya fedha za mradi huo”’, bali pia ulikuwa ‘“… haujapokea fedha ya pango, au malipo ya mkopo kutoka Serikalini ambao tayari umelimbikiza riba ya shilingi bilioni 14.157.”’

Wednesday, May 29, 2013

VACANCIES ANNOUNCEMENT - MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL


MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL
VACANCIES ANNOUNCEMENT

1.0 MEDICAL SPECIALIST I (5 POSITIONS)
1.1 Reports to: Head of Firm
1.2 Duties and Responsibilities
 To participate in the planning and implementation of quality improvement strategies.
 To coordinate preparation of department budget input.
 To review inputs for, and coordinate preparation of periodical reports.
 To carry out operational and investigative research and issue reports accordingly.
 To review conditions of hospitalized staff and advise on appropriate medication.
 To supervise patients’ case presentation and participate in training other staff.
 To plan and carry out research.
 To attend to IPPM Clinics.
 To set performance targets for all staff in the unit and ensure that all staff have elaborate job plans.
 To supervise, appraise staff and identify development and training needs.
 To perform any other duty assigned from time to time by the supervisor.
1.3 Required Qualifications
 Holder of three or more years Postgraduate Degree (M.Med/M.Dent.) in one of the medical fields.
 Must be registered with the Medical Council of Tanganyika
 Mmust have worked as a specialist Medical Doctor for not less than three years
 Must have published not less than two research papers in their areas of specialization in the last six years, one of which he must be the principal author.
 Must be computer literate

2.0. MEDICAL SPECIALIST II (57 POSITIONS)
 Cardiac Anesthesiologists – 6 positions
 Surgeons - Training - 4 positions
 Cardiothoracic Surgery Trainees - 6 positions
 Cardiac Surgeons(Adults /Paediatric - 8 positions
 Vascular Surgeons - 2 positions
 Paeditricians –Training - 2 positions
 Physicians –Training - 2 positions
 Paediatric Cardiologist (Trainees ) - 10 positions
 Adult Cardiologists - 6 positions
 Anesthesiologists-Training - 2 positions
 Other specialties - 9 Positions
2.1 Reports to: Head of Firm
2.2 Duties and Responsibilities
 To provide routine specialized medical services for in-patients and out patients in their areas of specialization.
 To participate in the training of student doctors in their areas of specialization.
 To plan, supervise and evaluate medical services offered in their respective fields.
 To prepare periodic reports regarding medical services
 To carry out research in the medical field and publish results for use by other experts.
 To supervise junior medical doctors and give them needed technical advice in their respective areas of specialization.
 To plan and supervise outreach programmes in their areas of specialization.
 To carry out any other duties as assigned from time to time by their supervisors.
2.3 Required Qualifications
Holder of Doctor of Medicine degree with three or more years Masters Degree in one of the medical fields.
Must be registered with the Medical Council of Tanganyika.

MDIS MERIT SCHOLARSHIP FOR INTERNATIONAL STUDENTS, 2013/14


Management Development Institute of Singapore (MDIS), Singapore offers merit scholarship for international students. These scholarships are open to new students for pursuing a pre degree, degree or master’s degree programme at five renowned university partners from the United Kingdom, Australia and France.  Each scholarship is tenable only for the academic years for which it is awarded and will cover the subsidised portion of the tuition fee. Applicants can apply till 31st August 2013 for Phase 1 and 31st March 2014 for Phase 2.


LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...