Friday, June 7, 2013

RAIS KIKWETE AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI SINGAPORE KWA KUTEMBELEA MAENEO MBALIMBALI.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembelea Taasisi ya Elimu ya ufundi (Institute of Technical education) iliyo sawa na VETA kwa Tanzania jana Juni 6, 2013.ambapo pamoja na mambo mengine walijionea jinsi wanafunzi wake wanavyofundishwa kuunda vipuli vya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na vya ndege.
Baadhi ya wafanyabiashara walioongozana na Rais Jakaya Kikwete katika ziara ya kikazi nchini Singapore wakiwa katika picha ya kumbukumbu na mawaziri walio katika msafara huo jana Juni 6, 2013. . Wa pili kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda na Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe (wa tatu) kulia.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Upya ya Miji ya Singapore jana Juni 6, 2013.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi ya Elimu ya Ufundi ya Singapore baada ya kutembelea kampasi yao jijini Singapore jana Juni 6, 2013.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji mijini ya Singapore jana Juni 6, 2013.ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji Upya wa Miji  ya Singapore jana Juni 6, 2013 ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu.PICHA NA IKULU.

Thursday, June 6, 2013

JIJI LA MWANZA LAENDELEA KUSHIKILIA TAJI LA USAFI TAIFA.

Kwa mara ya nane mfululizo jiji la Mwanza limeendelea kushika nafasi ya kwanza kwa kuwa jiji linaloongoza kwa Usafi Tanzania.Ushindi huo umetangazwa jana katika kilele cha siku ya mazingira kitaifa sherehe zilizofanyika Wilayani Nkasi Mkoa wa Rukwa.Akiongea na blogu hii Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Stanslaus Mabula  amesema kuwa Jiji lake liko kwenye mpango wa kushindana kimataifa kwa usafi.
Hongera sana Mwanza na majiji mengine yanatakiwa kuiga mfano huo ili nayo yaweze kutwaa taji hilo.
Miongoni mwa mitaa ya Jiji la Mwanza.




TANGAZO LA AJIRA 2013/2014 - JESHI LA POLISI



                                                     TANGAZO LA AJIRA
Jeshi la Polisi Tanzania katika mwaka wa fedha 2013/2014 litaajiri vijana kutoka katika makundi yafuatayo: waliomaliza kidato cha nne mwaka 2012, kidato cha sita mwaka 2013, JKT/JKU mwaka 2013 na vyuo vya elimu ya juu mwaka 2013.Taratibu zinakamilishwa ili waliomaliza kidato cha nne na sita na waliojaza fomu za maombi kabla ya kumaliza mitihani yao ya mwisho waitwe kwenye usaili. Usaili wa vijana wa JKT umekamilika mapema mwezi Aprili, 2013.Tangazo hili linawaalika vijana walioko kwenye vyuo vya elimu ya juu nchini watakaohitimu masomo hivi karibuni na wanaopenda kujiunga na Jeshi la Polisi kujaza fomu za maombi zinazopatikana kwenye tovuti ya Polisi kwa anuani www.policeforce.go.tz Fomu za waombaji baada ya kujazwa kikamilifu ziletwe na mkuu wa chuo kabla ya tarehe 30/6/2013 kwa:
Inspekta Jenerali wa Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
S.L.P. 9141,
DAR ES SALAAM.
Fani zinazotakiwa ni; Shahada za Menejimenti ya Rasilimali watu, Utawala, Uchumi, Usimamizi wa Sheria na Utekelezaji(BaLE), Ualimu, Sosholojia, Saikolojia na Ushauri Nasihi(Educational Psychology and Councelling),Takwimu, Lugha(Kiswahili/Kiingereza/Kifaransa/Kireno/Kiarabu), Usimamizi wa Programu za Maendeleo ya Jamii, Uhusiano wa Kimataifa, Uhandisi Mitambo(Mechanical Engineering), Uhandisi Kompyuta(Net Work, System Analyst, Data Base, Electronic & Telecommunications), Uandishi wa Habari, Mawasiliano ya Umma, Upangaji na Uendeshaji miradi, Jinsia na Watoto. Pia stashahada katika Usimamizi wa programu za maendeleo ya Jamii, Utunzaji kumbukumbu na Ukutubi.
Sifa za Muombaji:
  • Awe raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Awe na umri usiozidi miaka 28.
  • Awe na tabia njema.
  • Awe hajawahi kushtakiwa kwa kosa la jinai.
  • Awe na afya njema.
  • Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto.
  • Awe tayari kufanya kazi popote ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  • Asiwe na alama za kuchora mwilini(Tatuu).
  • Awe hajawahi kutumia madawa ya kulevya na
  • Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya Polisi.
Imetolewa na:
Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
S.L.P. 9141,
DAR ES SALAAM.

BREAKING NEWS: KHADIJA KOPA AFIWA NA MUMEWE.

Kwa taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mwimbaji wa Taarab wa kundi la TOT Khadija Kopa amefiwa na mumewe.Kwa taarifa zaidi endelea kutembelea blogu hii.

Wednesday, June 5, 2013

KENYA YAFUNGWA 1-0 NA NIGERIA,KATIKA HARAKATI ZA KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2014

Mchuano wa kufa na kupona umeshuhudiwa kati ya bingwa wa Afrika Super Eagles wa Nigeria na Harambee Stars wa Kenya katika uwanja wa kimataifa wa Moi Kasarani mjini Nairobi-Kenya ambapo Nigeria wameshinda 1-0 dhiki ya Harambee Stars ya Kenya.
Goli la Nigeria limefungwa na Musa Ahmed kunako dakika ya 81 ya mchezo huo. Mashabiki wa .

Kikosi cha Harambe Stars: Mlinda mlango Duncan Ocheng, Safu ya ulinzi David Owino, Brian Mandela, David Ochieng . Wachezaji wa kiungo cha kati Mulinge Ndeto, Victor Wanyama, Jamal Mohammed, Johana Omolo na Peter Opiyo. Washambulizi ni Kefa Aswani na Fracis Kahata
 .Kikosi cha Eagles:Golikipa ni Enyeama, Efe, Oboabona, Omeroo Elderson, Onazi, Mikel, Mba,Oduamadi,Musa, Ideye

MAMA MANGWEA HALI TETE WAKATI MWILI WA MAREHEMU UKISUBIRIWA.

Mama mzazi wa marehemu Albet Mangwea Bi.Denisia Mangwea akiwa kitandani nyumbani kwake kihonda mazimbu road muda mfupi baada ya kutoka hospital ya mkoa wa Morogoro alikokuwa amelazwa baada ya kuanguka ghafla baada ya kuelezwa kwamba mwili wa mwanae ulishindwa kuwasili nchini juzi kama ilivyolipotiwa awali.

Leo blog hii ilifika tena nyumbani kwa mfiwa huyo kwa lengo la kumjulia hali na kujua hali ya maandalizi ambapo alipohojiwa alidai kwamba bado afya yake haijatengemaa.

Hata hivyo alisema vyovyote itajkavyo kuwa ni razima ashiriki kikamilifu ibada na mazishi ya mwane kitinda mimba.

 Albaet aliyekufa ghafla nchini Afrika kusini jumanne ya wiki iliyopita.Mwili wa msanii huyo unatarajiwa kuzikwa jirani na kaburi la marehemu baba yake Mzee Keneth Mangwea kwenye makaburi ya Kihonda yaliyopo nje ya kanisa la Mtakatifu Monica kesho Alhamisi.

MASTERS SCHOLARSHIPS AT CARDIFF UNIVERSITY IN UK, 2013/14 .

The School of History, Archaeology and Religion, Cardiff  University offers masters studentships in the field of archaeology, ancient history, conservation, history, religious studies and theology. Minimum of 2:1 or equivalent for overseas applicants) in a BA Degree in a relevant subject. The masters studentships are awarded on the basis of academic merit. Awards are open to students of any nationality. International students will be offered an award equivalent to the value of the UK/EU course fees and will be required to cover the remaining international fees themselves. The application deadline is 1st July 2013.

Study Subject(s): Studentships are provided in the field of archaeology, ancient history, conservation, history, religious studies and theology.
 

TASWIRA YA ZOEZI ZIMA LA KUUAGA MWILI WA MANGWEA DAR LEO.




TAARIFA KWA UMMA JUU YA MAOMBI YA MIKOPO 2013/2014 KWA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU.

  1.0            UTANGULIZI
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inawafahamisha waombaji wa mikopo kwa mara ya kwanza, Wanafunzi wanaondelea na masomo na Umma kwa ujumla kwamba mchakato wa maombi mikopo kwa mwaka wa masomo 2013/2014 ulizinduliwa rasmi tarehe 1 Mei, 2013.  Mchakato huo unaendelea vizuri na kwamba wanafunzi wengi wameweza kujaza fomu za maombi ya mikopo kwa njia ya mtandao (OLAS).

2.0   WAOMBAJI WA MIKOPO WA MARA YA KWANZA

Utaratibu wa kujaza fomu za maombi kwa waombaji wa mara ya kwanza, unawaelekeza waombaji hao kutoa taarifa zao za kihistoria kama vile shule za sekondari walizosoma (Kidato cha IV na Kidato cha VI), hali ya mwombaji au wazazi wake kiafya na pia taarifa za mdhamini wa mwombaji mkopo. Taarifa hizo zinaiwezesha Bodi kuchambua na kujua iwapo mwombaji husika ana sifa ya kukopesheka au la. Ikumbukwe kwamba lengo la utoaji wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ni kuwawezesha wanafunzi wasio na uwezo wa kulipia gharama za elimu ya juu kusaidiwa kufikia malengo yao. Kwa njia ya uchambuzi huo Bodi inaweza kubaini kiasi cha mkopo unaohitajika au kiasi ambacho mwanafunzi anapaswa kuchangia katika gharama zake za elimu ya juu.
Kwa vile taarifa za ufaulu katika mitihani ya kidato cha sita hazihitajiki katika hatua hii ya Mwanzo, mwombaji wa mkopo haulizwi mahali popote katika fomu yake ya maombi kuhusu kiwango cha ufaulu. Hapo baadaye Bodi itakapohitaji kuthibitisha kiwango cha ufaulu wa mwombaji itapata taarifa hizo za ufaulu moja kwa moja kutoka Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).  Kutokana na utaratibu huu, mwanafunzi aliyehitimu kidato cha sita mwaka 2013 anaweza kuomba mkopo hata kabla ya matokeo ya Kidato cha Sita kitaifa kutolewa.  Hii ni muhimu ili kuipa Bodi muda wa kutosha kupokea maombi ya mikopo, kuchambua na kisha kupanga mikopo kwa wanafunzi stahiki watakaokuwa wamedahiliwa kwa mwaka mpya wa masomo 2013/2014.

3.0       IDADI YA WANAFUNZI WALIOKWISHAOMBA MIKOPO KUFIKIA MEI 30, 2013

Hadi kufikia tarehe 30 Mei, 2013, waombaji mikopo wa mara ya kwanza waliokwishakamilisha maombi yao ni   424, Waombaji wa mara ya kwanza ambao wako kwenye hatua mbalimbali za ukamilishaji ni 5,320 na wanafunzi wanaoedelea na masomo waliokwishathibitisha kuendelea kupatiwa mikopo kwa mwaka ujao wa masomo ni 60,367, kama inavyoonekana kwenye jedwali hapa chini.
Na.
Waombaji wa mara ya kwanza waliokamilisha kujaza fomu
Waombaji wa mara ya kwanza ambao wako kwenye hatua mbalimbali za ukamilishaji
Wanafunzi wanaoendelea na masomo waliojaza fomu na kukamilisha

424
5320
60367

4.0            HITIMISHO

Bodi inatoa msisitizo kwa waombaji wa mikopo kama ifuatavyo:
(i)                Kuzingatia taratibu zote muhimu zilizowekwa kwa ajili ya maombi ya mikopo.
(ii)              Kutumia huduma ya msaada kwa wateja (Help Desk) kikamilifu kila wanapopata tatizo lolote katika mchakato wa ujazaji wa fomu za maombi.  Huduma hiyo inapatika kwa kupiga namba 022 550 7910; kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 2 usiku siku za jumatatu hadi ijumaa na kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 10 alasiri siku ya jumamosi.
(iii)            Kuzingatia muda uliopangwa wa maombi ya mikopo ambapo siku ya mwisho ni tarehe 30 Juni, 2013.

IMETOLEWA NA:
BODI YA WAKURUGENZI
BODI YA MIKOPO YA ANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

RAIS KIKWETE ATUA SINGAPORE KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU 3

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Bw. Laurence Bay, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Singapore. Kushoto ni Balozi wa Tanzania India na Singapre Injinia John  Kijazi na mbele yao ni Naibu Mkurugenzi wa Itifaki wa Singapore Bi. Christine Tay.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Kasulu mjini Mhe Moses Machali pamoja na wadau wengine wakati akiwasili Singapore.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea jijini Singapore jana wakati alipokutana na wafanyabaishara za ujenzi wa nchi hiyo mara tu baada ya kutua kutoka Japan alikokuweko kwa ziara nyingine ya kikazi. Katika mkutano huu  Rais Kikwete aliwakaribisha wafanyabishara hao wa Singapore  Tanzania kuwekeza katika sekta ya nyumba wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...