Friday, December 19, 2014

TUME YA MIPANGO WATEMBELEA BANDARI YA BUKOBA.


Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwasili kwenye Bandari ya Bukoba, walipofika kujionea bandari hiyo kongwe iliyopo kwenye fukwe za Ziwa Victoria, mkoani Kagera. Waliotangulia mbele ni Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Wapili kulia). Wengine ni baadhi ya wajumbe wa msafara huo kutoka kushoto ni Bw. Omary Abdallah, Bibi Zena Hussein (Wapili kushoto) na Bw. Julius Edward (Kulia).

Mandhari ya gati la Bandari ya Bukoba

Wajumbe wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa kwenye ngazi za kupandia kwenye meli zinazotia nanga kwenye Bandari ya Bukoba.

Wajumbe wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa kwenye Ofisi za Bandari ya Bukoba. Jengo la Ofisi hiyo limejengwa takriban miaka 70 iliyopita. 

Sehemu ya kupumzikia abiria wa Bandari ya Bukoba.

Wajumbe wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwa kwenye moja ya maghala ya kuhifadhia mizigo kwenye Bandari ya Bukoba.  
PICHA NA SAIDI MKABAKULI

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...