Friday, December 19, 2014

JOB VACANCIES - TANZANIA POSTAL BANK.


JOB OPPORTUNITIES - SUA (RE-ADVERTISEMENT).

TUME YA MIPANGO WATEMBELEA BANDARI YA BUKOBA.


Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwasili kwenye Bandari ya Bukoba, walipofika kujionea bandari hiyo kongwe iliyopo kwenye fukwe za Ziwa Victoria, mkoani Kagera. Waliotangulia mbele ni Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Wapili kulia). Wengine ni baadhi ya wajumbe wa msafara huo kutoka kushoto ni Bw. Omary Abdallah, Bibi Zena Hussein (Wapili kushoto) na Bw. Julius Edward (Kulia).

Thursday, December 18, 2014

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO IRDP & GST-DODOMA 17-12-2014

Wasailiwa waliochaguliwa kuendelea na usaili wa mahojiano wanatakiwa kufika muda, eneo na wakati kama ilivyo onesha kwenye ratiba.

Wasailiwa wanatakiwa kufika na vyeti vyao halisi (Original Certificates)

ACCOUNTANT II - IRDP          

S/N   NUMBER                   SCORE    REMARKS
1    PSRS IRDP ACC II 0072    72    SELECTED
2    PSRS IRDP ACC II 0029    57    SELECTED
3    PSRS IRDP ACC II 0154    57    SELECTED
4    PSRS IRDP ACC II 0208    56    SELECTED
5    PSRS IRDP ACC II 0239    56    SELECTED
6    PSRS IRDP ACC II 0037    54    SELECTED
7    PSRS IRDP ACC II 0111    50    SELECTED
8    PSRS IRDP ACC II 0001    50    SELECTED
9    PSRS IRDP ACC II 0194    50    SELECTED

JOB VACANCIES - EWURA.

Wednesday, December 17, 2014

WAKURUGENZI 6 WAFUKUZWA KAZI KWA KUBORONGA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, AISHA MADINDA AFARIKI.

WaziriI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI), Hawa Ghasia 
WaziriI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI), Hawa Ghasia leo amewavua madaraka Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkuranga, Kaliua, Kasulu, Serengeti, Sengerema na Bunda kufuatia kasoro za uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba, 14 mwaka huu. Wakurugenzi wengine watano (5) bado wanachunguzwa.
Aidha Waziri Ghasia amesema kuwa hawezi kujiuzulu kama alivyoahidi baada ya watendaji waliozembea kugundulika.

Kifo cha Madinda.
 Msanii mnenguaji wa bendi ya Extra Bongo, Aisha Mbegu "Madinda" amefariki leo mchana katika Hospitali ya Mwananyamala na chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika.

Kwa taarifa zaidi, endelea kutembelea blogu hii.

JOB VACANCIES - TANZANIA POSTAL BANK.


KAGERA KUJIVUNIA UWANJA WA NDEGE WA KISASA

Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kagera kujionea maendeleo ya Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja hicho. Waliotangulia mbele ni Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto), Meneja Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Bukoba, Mhandisi Suleiman Athuman (Katikati) na Meneja wa kiwanja hicho, Bw. Julius Mulungwana (Kulia).
Na Saidi Mkabakuli, Kagera
Mkoa wa Kagera na maeneo ya jirani wataanza kujivunia uwanja wa ndege wa kisasa kufuatia kukamilika kwa Kiwanja cha Ndege cha Bukoba.
Akizungumza na Wakaguzi wa Miradi ya Maendeleo toka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Meneja Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kagera, Mhandisi Suleiman Athuman, amesema kwamba maendeleo ya ujenzi wa jengo la abiria la kiwanja hicho upo kwenye hali nzuri na mkandarasi atabidhi kazi hiyo mapema mwakani.
“Katika mwaka wa fedha wa 2013/14 kazi zilizopangwa ni ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya kiwanja, ikijumuisha barabara ya kuruka na kutua ndege, maegesho ya ndege, barabara ya kiungio, kwa sasa ujenzi unaendelea vizuri na Mkandarasi atatukabidhi kazi mapema mwakani,” alisema Mhandisi Athuman.
Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Kiwanja cha Bukoba, Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa kiwanja hiko, Mhandisi Pius Gobolo amesema kuwa kazi za usimikaji wa mfumo wa taa za kuongozea ndege, ujenzi wa jengo jipya la abiria na uzio wa usalama zimeshakamilika kwa asilimia 80.

Friday, December 12, 2014

SUALA LA ESCROW, TANZANIA YABANWA ZAIDI.

MCC Statement on Board of Directors’ Discussion of Tanzania at the December 2014 Meeting
Washington, D.C.—The U.S. Government’s Millennium Challenge Corporation (MCC) issued the following statement after its Board of Directors (Board) held its annual country selection meeting on December 10, 2014:
“MCC takes seriously all of its country partners’ commitments to combat corruption. At today’s meeting, MCC’s Board expressed continued concern over corruption in Tanzania, including the implications of the recent case involving Independent Power Tanzania Limited (IPTL). The Board noted that Tanzania has experienced a significant decline over the past seven years on the key indicator measuring efforts to control corruption. While the Board voted to allow Tanzania to continue working to develop a compact proposal—given its passage on MCC’s policy scorecards and its strong previous performance as an MCC partner—the Board stated its expectation that the Government of Tanzania must take firm, concrete steps to combat corruption before a compact is approved. Further, the Board voted to continue MCC’s engagement with Tanzania with the understanding that, in accordance with the Tanzanian State House December 9 statement, the Tanzanian government would act promptly and decisively on the late November parliamentary resolutions regarding IPTL. The Board also reaffirmed more broadly that Tanzania must undertake a series of previously agreed upon structural reforms to improve the efficiency, effectiveness and transparency of the energy sector, and more generally to deal with wider corruption.”
Source: http://www.mcc.gov

KATIBU MKUU KIONGOZI AMUAGA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI, BW. LUDOVICK UTOUH, NA KUMKARIBISHA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU MPYA WA HESABU ZA SERIKALI PROFESA MUSSA JUMA ASSAD, ALHAMIS, 11 DESEMBA 2014

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue (kulia), akimkabidhi zawadi, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mstaafu, Bw. Ludovick Utouh (kushoto), katika hafla ya kumpongeza na kumuaga iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, 11 Desemba, 2014.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, leo tarehe 11 Desemba 2014, amemuaga rasmi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mstaafu Bw. Ludovick Utouh, katika hafla maalum iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na baadhi ya Watendaji Wakuu na Waandamizi kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali ilikuwa mahsusi pia kumkaribisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu mpya wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Juma Assad.
Katika hotuba yake ya kumpongeza Bw. Utouh, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue, alielezea historia ya Utumishi uliotukuka ya Bw. Utouh ambayo imeleta sifa kubwa Ofisi hiyo ndani na nje ya nchi na katika medani za kimataifa. Kwa ujumla, hotuba ya Katibu Mkuu Kiongozi ilijikita kuelezea mchango binafsi wa Bwana Utouh kwa taifa ndani ya miaka zaidi ya arobaini (40) ya Utumishi wake Serikalini.
Aidha, Katibu Mkuu Kiongozi alielezea mafanikio ya Serikali kwenye eneo la utawala bora, uwajibikaji na uzingatiaji wa sheria, kanuni na taratibu za fedha za umma ambayo yamechangiwa na Bw. Utouh. Balozi Sefue aliwasihi watumishi wa umma kuiga weledi, uaminifu, msimamo, bidii na maarifa ambayo Bw. Utouh alivionyesha kwa vitendo katika utumishi wake.
Katibu Mkuu Kiongozi alitumia fursa hiyo pia, kumtakia kila la kheri, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali mpya, Profesa Juma Assad, katika kufanikisha majukumu aliyopewa.
Bwana Utouh alistaafu rasmi nafasi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, tarehe 19 Septemba, 2014 baada ya kuitumikia nafasi hiyo kwa miaka saba na miezi kumi tangu alipoteuliwa na Rais, tarehe 19 Agosti, 2006

NB: Hotuba Kamili iko katika Tovuti ya Katibu Mkuu Kiongozi.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mstaafu, Bw. Ludovick Utouh (kulia), na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu mpya wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Juma Assad(kushoto), katika hafla ya kumpongeza na kumuaga Bw. Utouh iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es Salaam,11 Desemba, 2014.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...