Monday, September 30, 2013

NIA YA ZITTO KABWE JUU YA KUFANYA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MAGAZETI.

Nimetoa taarifa rasmi kwa katibu wa Bunge kwa mujibu wa kanuni za Bunge kwamba katika mkutano ujao wa Bunge nitawasilisha muswada binafsi wa sheria kufanya marekebisho ya sheria ya magazeti kwa lengo la kuifuta kabisa sheria hiyo.
Madhumuni ya muswada huo ni;

“kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 kwa sababu inakizana na Katiba ya Nchi kuhusu haki za Raia kupata habari na kwamba iliorodheshwa na tume ya Nyalali ni sheria kandamizi’
...
Muswada wenyewe nitauwalisilisha siku ya ijumaa ili uchapwe kwenye gazeti la Serikali uweze kuingia kwenye shughuli za Bunge zitakazoanza tarehe 15 Oktoba 2013 kwa ngazi ya kamati.

September 30, 2013
Source : Zitto social media.

JOB VACANCIES - NELSON MANDELA AFRICAN INSTITUTE OF SCIENCE & TECHNOLOGY.

YANGA - TAARIFA KUHUSU MRADI WA UWANJA.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Francis Kifukwe (katikati) ambaye pia ni mwenyekiti wa mradi wa ujenzi wa uwanja eneo la jangwani akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu leo, kushoto ni mzee Jabir Katundu (mwenyekiti wa baraza la wazee) na kulia Lawrence Mwalusako katibu mkuu wa Yanga SC
 
LEO tungependa kupitia kwenu kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi wetu wa Uwanja wa kisasa wa mpira katika Jiji la Jangwani kama itakavyojulikana

Mara ya mwisho tuliongea ama kuonana ilikuwa mwezi wa tatu wakati Ndugu zetu wa BCEG walipokabizi Concept design ama Usanifu wa awali na kuanzia sasa tutakuwa tunatoa taarifa za mara kwa mara kuhusu mradi huu. Wahenga walisema UKICHA KUSEMA HUTATENDA JAMBO lakini pia KUKAA KIMYA SANA kunajenga hisia mbaya na kutoa nafasi ya upotoshwaji wa habari. 

Kwa kifupi napenda kuwakumbusha kuwa Makubalino ya Awali (Memorandum of Understanding) yalisainiwa 23 Novemba 2012. Pamoja na mengineyo YANGA inatakiwa:
Kupata na kuwa na eneo la kutoshereza malengo ya mradi
Kupata ushauri mzuri, michoro mizuri na mkandarasi mzuri wa mradi
Kupata na kutenga fedha za kukamilisha usanifu na ujenzi wa mradi

Kwa upande wa BCEG wajibu wao ni kuwa na utaalamu na uzoefu wa kutosha. BCEG wameandaa na kukabidhi michoro ya usanifu wa awali kukidhi matakwa ya YANGA. YANGA tunatakiwa kutoa maoni yetu na na kuingia RASMI mkataba wa ujenzi.

Kutokana na kukua kwa Jiji la Dar es Salaam, na katika hali ya kutaka klabu iwe na vitega uchumi klabu imeonelea ni vyema kama ingekuwa na uwanja wa mpira wa karne ya sasa na baadaye ambao pamoja na mambo mengine utakuwa na mioundombinu ifuatayo:-

Mahojiano na Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Willbrod Slaa _ MAREKANI

EMPLOYMENT VACANCIES - PCCB.

EMPLOYMENT VACANCIES
The PCCB is an Independent Public Institution and law enforcement Agency established by Section 5 of the Prevention and Combating of Corruption Act No. 11 of 2007. The Bureau is mandated to carry out three major functions: Prevention, Community Education and law enforcement in Tanzania mainland.
Suitably qualified Tanzanians are invited to join our family in the following positions:

1.0 INVESTIGATION OFFICERS (214 POSTS)
1.1   DIRECT ENTRANTS (FROM COLLEGES/UNIVERSITIES)
  • Applicants should posses three years Advanced Diploma or Undergraduate degree from recognized higher learning Institutions in any of the following fields: Quantity survey, Accountancy, Human Resources Management, Law, Procurement, Journalism, Information Technology, Highways Engineering, Building Constructions, Electrical Engineering, Land Management and Valuation, and Forensic Knowledge.

JOB OPPORTUNITY IN TANZANIA.

Climate Change

Job Opportunity Energy Efficiency Expert (National)
Posted on 17 Sep, 2013
Application by 8 Oct, 2013
Project Status: Tender
Project Title Sustainable use of Renewable Energy - Component: Promotion of Energy Efficiency
Period of Project: Feb, 2014 - Dec, 2016
Duration of assignment:35 months
Country:Tanzania
Duty Station:to be determined
Job Code AFR-TZA13GIZ0232/2

Project Description: The goal of the program (target module) is: The conditions for the sustainable use of Renewable Energy (RE) are improved in Tanzania. The program supports the expansion of grid-connected renewable energies through advisory on the general framework and capacity building. The procedures for approval of small RE systems (10 MW), which are supported through the Rural Energy Agency REA, should be organized more efficiently. In addition, strategies and support measures for Energy Efficiency are supported. Political support is the Ministry of Energy and Minerals (MEM).

Job Description:Subject to this tender is the "promotion of energy efficiency (EE)".

Key tasks include:

  • Promotion of energy efficiency
  • Technical design and economic analysis of pilot projects 
  • Design of measures for the promotion of EE
  • Technical audits/energy audits
  • Organization of workshops and awareness raising campaigns


Qualifications:
  • Master degree or equivalent diploma in engineering, economics or other relevant sector
  • Specific technical and economic knowledge in the field of energy supply and utilization as well as energy efficiency
  • Expertise in the above mentioned topics
  • At least 5 years working experience in the promotion of energy efficiency
  • Extensive knowledge of the Tanzania energy sector and its institutions
  • Working knowledge of English and Swahili
  • Excellent communication skills
  • Proven project management skills
  • Full command of Microsoft Office software

CV-Form: CV GIZ

Contact Person: Romy Rösner
Contact: Roesner@gfa-group.de

Wigh Fellowships for International Scholars at Harvard University in USA, 2014

Weatherhead Center for International Affairs through the Weatherhead Initiative on Global History (WIGH) offers fellowships for international scholars in the USA. The fellowships are available to support outstanding scholars whose work respond to the growing interest in the encompassing study of global history. Applications are welcomed from qualified persons without regard to nationality, gender, or race. Fellows will receive an annual stipend of up to $50,000, according to fellows’ needs. WIGH Fellows are appointed for one year and are provided time, guidance, office space, and access to Harvard University facilities. Applications should be submitted till January 10, 2014.

Friday, September 27, 2013

Wakuu wa usalama kuhojiwa Kenya.


Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.

Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.

Walipuuza onyo?

Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.

Chanzo: BBC

KIFO CHA MWANDISHI WA HABARI WA MWANANCHI VENANCE GEORGE.

Marehemu Venance George.
Mwandishi wa habari wa Mwananchi Communication Limited Venance George, jana alipoteza maisha akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro alipokuwa amelazwa.
Marehemu alikuwa akisumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa muda mrefu na kifua hali iliyopelekea kwenda kulazwa katika hospitali ya Aga Khan iliyopo jijini Dar es salaam na kupata nafuu, Baada ya kurudi nyumbani hali ilbadilika tena na kupelekea kwenda kulazwa katika hospitali ya Holly Cross Mission iliyopo mkoani Morogoro na baadaye kuhamishiwa katika hospitali kuu ya mkoa wa Morogoro.

Marehemu alipata nafuu na kuruhusiwa kurudi nyumbani , baada ya siku kadhaa hali ilibadilika tena na kupelekea kwenda kulazwa hospitali ya mkoa wa Morogoro hadi umauti ulipomkuta mnamo tarehe 26/09/2013 saa 9:15.
-Marehemu ameacha mjane na watoto wawili wa kike na wa kiume.
 
HISTORIA FUPI YA MAREHEMU VENANCE GEORGE.
Marehemu Venance George Mhangilwa alizaliwa mnamo 8/12/1973 Bukoti wilaya ya Geita.
ELIMU:
-Marehemu alisoma katika shule ya msingi Bugogo kuanzia mwaka 1981 mpaka mwaka 1987 alipohitimu elimu yake ya msingi.

-Mnamo mwaka 1988 alianza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Forest Hill iliyopo Morogoro na kuhitimu kidato cha sita mnamo mwaka 1994.
-Mwaka 1995 alijiunga katika chuo cha uandishi wa habari na kuhitimu mwaka 1996.
AJIRA:
Marehemu alianza kazi ya uandishi wa habari katika kampuni ya,
 -Uhuru Publication Limited, 1996-1998.
-Kuna Entarprises Company Limited, 1998-1999.
-Village Travel And Transport Project (VTTP), 2001-2003.
-Swiss-Contact Tanzania Limited, 2001-2003
-Mwananchi Communication Limited, 2003 mpaka mauti yalipomkuta.
Pia alijiendeleza kimasomo katika chuo kikuu huria cha Tanzania ambapo alitakiwa kuhitimu shahada yake ya mawasiliano ya umma mwezi wa 12 mwaka huu 2013.

Monday, September 16, 2013

ZITTO KABWE AKIHOJIANA NA MAMA ALIYEDAIWA KUWA MUHAMIAJI HARAMU KUMBE SIO.

"Mama huyu kakamatwa kama mhamiaji haramu na kupelekwa Ubalozi mdogo wa DR Congo uliopo Manispaa ya Kigoma. Amezaliwa Tanzania, amesomea Tanzania, Baba yake Mtanzania, Babu yake Mtanzania na Ndugu zake wengine Watanzania na hawakukamatwa. Amekamatwa akitoka kuchota maji ziwani Tanganyika. Malalamiko yake nimeyafikisha kwa Waziri wa Mambo ya Ndani".
Chanzo: Zitto Social media.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...