Tuesday, May 7, 2013

UBUNGE CHADEMA 2015,NAFASI KUTANGAZWA GAZETINI NA WATU KUOMBA KAMA AJIRA.

Katibu mkuu wa CHADEMA Dr.Wilbroad Slaa.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mfumo mpya wa kuwapata wagombea nafasi ya ubunge kuanzia uchaguzi wa 2015. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa alisema kuwa kuanzia uchanguzi ujao wa 2015, nafasi za wagombea ubunge majimbo yote nchini zitatangazwa kwenye magazeti.
Dk. Slaa alisema baada ya waombaji kujitokeza watafanyiwa usaili kwa kufanya mtihani utakaokuwa umeandaliwa kwa kuzingatia nafasi hizo.

“Mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe amekwisha kusema kwamba kuanzia sasa hatupokei makapi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hili naliweka wazi kwamba uchaguzi ujao utakuwa na mfumo mpya na wenye mabadiliko makubwa, tunaamini utaleta uzalendo na kuondoa upuuzi unaojitokeza.

“Kwa wale walio na mipango ya kujitokeza dakika za mwisho kugombea nafasi za ubunge kupitia CHADEMA au nje ya chama, naomba wasahau hilo tunataka mtu anayetetea wananchi, mwenye uzalendo, hoja, ujasiri na mwenye kuitoa Tanzania hapa ilipo na kuisogeza mbele,”alisema.

Akizungumzia suala la mchakato wa katiba mpya alisema CHADEMA haitakubali kuona inakuwa sehemu ya watu walioshiriki kutengeneza katiba isiyo ya Watanzania wote.

“Sasa kwa kuwa Serikali imetoa majibu yake bungeni kupitia kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda tunasubiria mwenyekiti wetu Mbowe awasilishe ripoti kwenye kamati kuu ndipo tutakapoamua.

“Pia suala la mwakilishi wetu katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Profesa Mwesiga Baregu litazungumzwa kwenye kamati kuu, chama kikijitoa hata kama akibaki hayo yatakuwa ni mawazo yake,”alisema.

Hata hivyo alisema kuwa amani ya imevurugwa na viongozi wa Serikili na vyama vya siasa kutokana na kutanguliza ushabiki wa siasa badala ya uzalendo na misingi ya taifa.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iramba Magharibi, Ntundu Emmanuel amehamia CHADEMA akidai kuchoshwa na matusi ya Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba.
 
Source:CHADEMA social media.

RAPA WA KIKE LAURYN HILL AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIEZI 3 KWA KUTOLIPA KODI.



Rapa mkongwe wa kike Duniani Lauryn Hill ahukumiwa kifungo cha miezi 3 kwa kile kinachodaiwa kukwepa kulipa kodi ya kiasi cha $1.8 millioni.

Na hii hapa chini ni wasifu wa msanii huyu.


Background information
Birth name Lauryn Noelle Hill
Also known as Ms. Hill, L. Boogie
Born May 26, 1975 (age 37)
Origin South Orange, New Jersey, United States
Genres R&B, hip hop, soul, reggae fusion
Occupations Singer-songwriter, record producer, rapper, actress
Instruments Vocals, guitar, piano
Years active 1987–present
Labels Columbia, Ruffhouse
Associated acts Fugees, Nas, D'Angelo, Mary J. Blige, Santana
Website www.lauryn-hill.com    

NASHERA HOTEL-KIWANJA CHA KISASA MOROGORO.

Nashera Hotel is a 4-star hotel features an outdoor pool, and is located just over 3km from the centre of Morogoro. It has panoramic views of the Uluguru Moutain and includes free Wi-Fi throughout the property.
All of the rooms at Nashera Hotel are air-conditioned and offer a balcony and a satellite TV. Each has an en suite with a bath and a shower.
Breakfast is served daily, which can also be taken in the room. The restaurant, Udzungwa, serves dishes ranging from American specialties to classic Swahili fare. A number of restaurants serving a range of local and international cuisine can also be found within 5 minutes’ drive of the property.
Guests can relax in the garden with a drink from the bar, or the Nashera’s staff can arrange a tour in the local region. Morogoro Airport is located 5km away.
 

Click Read more to continue.

JESHI LA POLISI LATAKIWA LIVUNJWE,LADAIWA KUTUMIWA VIBAYA NA CCM

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetaka Jeshi la Polisi nchini livunjwe na ligeuzwe kitengo ndani ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Msimamo huo umetolewa jana bungeni na baadhi ya wabunge wa chama hicho walipokuwa wakichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyowasilishwa na Waziri Emmanuel Nchimbi.
Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde, alisema Jeshi la Polisi limeoza, kwa sababu limeshindwa kutekeleza wajibu wake kikamilifu, ikiwamo kuwakamata wahalifu mbalimbali wanaoshiriki kwenye matukio ya kihalifu.
“Napendekeza Jeshi la Polisi livunjwe na liingizwe ndani ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) liwe sehemu ya kitengo katika jeshi hilo.
“Naamini kwa kufanya hivyo tutaboresha utendaji wake, silaha kubwa iliyobaki kulinusuru taifa hili kwa sasa ni kusema ukweli, kwani bila kufanya hivyo miaka sita ijayo hali itakuwa mbaya,” alisema.
Bofya read more kuendelea.

Monday, May 6, 2013

RAIA 4 WA SAUDIA WAKAMATWA KUHUSIKA NA MLIPUKO WA BOMU ARUSHA.

Polisi Mkoani Arusha inawashikilia watu 8 kwa madai ya kuhusika na mlipuko wa jana siku ya jumapili katika kanisa Katoliki la Olasit viungani mwa mji wa Arusha.
Miongoni mwa washukiwa ambao wako mikononi mwa polisi ni raia wanne (4) wa Saudi Arabia, na wengine wanne (4) ni raia wa Tanzania.
Wakati mwandishi wa BBC Baruan Muhuza akuzungumza akiwa hospitalini mjini Arusha amesema idadi ya watu waliofariki dunia kufuatia mlipuko huo ni wawili na wala sio watatu kama ilivyoripotiwa hapo awali.
Polisi mjini Arusha vile vile wamethibitisha kuwa waliokufa wakati wa tukio hilo la kigaidi ni wawili.
Kwa wakati huu polisi wanachunguza ni kilipuzi aina gani kilitumika wakati wa shambulizi hilo.
Lakini Baruan Muhuza ambaye alitembelea eneo la tukio mbali na majeruhi hakuna hasara kubwa iliyotokea mahali hapo pia sakafu na kuta za kanisa hilo hazikuchimbika sana.
Kutoka Dar es Salaam Leornad Mubali anaongezea kuwa watu wawili sana wamethibitishwa kufariki dunia katika mlipuko huo uliotokea majira ya saa tano asubuhi katika kanisa katoliki la Olasit nje kidogo ya mji wa Arusha nchini Tanzania na wengine kadhaa kujeruhiwa huku balozi wa papa na watawa waliokuwa katika shughuli hiyo maalumu ya uzinduzi wa parokia mpya ya mtakatifu Yosefu mfanyakazi wakinusurika pia .
Kwa mjibu wa Padri Festus Mangwangi ambaye ni paroko msaidizi wa kanisa katoliki jimbo la Arusha mlipuko huo unapotokea walikuwa tayari katika hatua ya kubariki maji kwaajili ya uzinduzi wa kanisa ulikuwa ukiongozwa na balozi wa Papa Fransis.
Shambulizi la Arusha
Hata hivyo Padre Mangwangi ameiambia BBC kuwa taarifa walizonazo muda mfupi baada ya majeruhi kukimbizwa hospitali watu kati yao wamefariki huku wengine wakiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Mount Meru mjini Arrusha.
Shughuli zote kuhusiana na ibada hiyo zimesitishwa huku watalaalamu wa milipuko na polisi wakiendelea na uchunguzi kuhusiana na mlipuko huo.
Bado hakuna taarifa zozote kuhusiana na chanzo halisi cha bomu hilo ama kundi lolote linalodaiwa kuhusika na utegaji wa bomu hilo.
Hili ni shambaulio la kwanza la bomu nchini Tanzania japo kuwa mwaka huu pia kulikuwa na mtukio ya mauaji ya Padre wa kanisa hilo visiwani Zanzibar ambaye alipigwa risasi wakati akiwa anajiandaa kuingia kanisani.
 
Chanzo:BBC

International Undergraduate &Masters Scholarships at Australian National University in Australia & Bangor University UK, 2013/2014

Australian National University offers International Undergraduate Scholarships in Australia. International Students can apply for this scholarship. International students who have recently completed secondary school studies off-shore (not in Australia). Students must not have commenced further studies. Applications for Semester 2 2013 will close at midnight on 14th June 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided in all the courses offered by the Australian National University at undergraduate level.
Course Level: This scholarship is available for pursuing undergraduate degree level at Australian National University.

Click read more to continue.

KIPANYA, SERIKALI NA WAFANYAKAZI WA TANZANIA.

Ni ukweli usiopingika kuwa Serikali inawaumiza wafanyakazi hasa kwenye mambo kama Kodi kuwa kubwa ili hali mishahara midogo.
Tafakari,Chukua hatua.

TAIFA STARS KUANZA MICHUANO YA COSAFA JULAI 6.

Taifa Stars imepangwa kundi A la michuano ya Kombe la COSAFA ambapo itacheza mechi yake ya kwanza Julai 6 mwaka huu jijini Lusaka, Zambia dhidi ya Shelisheli.

Upangaji ratiba (draw) wa mashindano hayo ulifanyika juzi (Mei 3 mwaka huu) jijini Lusaka ambapo timu nyingine zilizo na Taifa Stars katika kundi hilo ni Namibia na Mauritius. Kundi la Taifa Stars litachezea mechi zake jijini Lusaka.

Mechi ya pili ya Taifa Stars katika hatua ya makundi itakuwa Julai 8 mwaka huu dhidi ya Mauritius. Mechi ya mwisho katika hatua hiyo itakuwa Julai 10 mwaka huu dhidi ya Namibia.

Kundi B lina timu za Kenya (Harambee Stars), Botswana (Zebras), Lesotho na Swaziland. Hatua itakayofuata baada ya hapo ni ya mtoano (knockout) na kila kundi litatoa timu moja tu.

Iwapo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itafuzu kwa hatua itakayofuata itacheza Julai 13 mwaka huu na Afrika Kusini (Bafana Bafana) ambayo pamoja na timu nyingine tano zimekwenda moja kwa moja katika hatua ya mtoano.

Nyingine zilizokwenda moja kwa moja hatua ya mtoano ni wenyeji Zambia, Angola, Zimbabwe, Msumbiji na Malawi ambazo kwenye viwango vya ubora vya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ziko juu ya zile zilizoanzia hatua ya makundi.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, fainali ya michuano ya Kombe la COSAFA itafanyika Julai 20 mwaka huu.

Source:TFF Website.

MBATIA AZIDI KUIBANA SERIKALI,AMSHANGAA KAWAMBWA KUTOJIUZULU.

SIKU moja baada ya serikali kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne na kuamuru yaandaliwe upya, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, ameshangaa kuona Waziri Kawambwa hajiuzulu na ametaka wazazi wa wanafunzi waliojinyonga kwa matokeo hayo walipwe fidia.
Wakati akitaka wanafunzi hao walipwe fidia, pia Mbatia alimshangaa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, akihoji anasubiri nini kung’atuka wakati kuna wanafunzi wamepoteza maisha kwa uzembe wao.
Alisema Kawambwa anapaswa kujiuzulu kwani Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani nchini, Joyce Ndalichako, hawezi kufanya mabadiliko makubwa ya aina hiyo bila kuishirikisha wizara.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Mbatia ambaye pia ni Mbunge wa kuteuliwa alisema serikali imekuja na majibu rahisi kwenye jambo gumu, kwani uamuzi wa kufuta na kuandaa upya matokeo hayo kwa utaratibu wa mwaka 2011, hauleti ufumbuzi wa mfumo wa elimu.
“Tume imekuja na majibu mepesi sana kwenye tatizo kubwa. Wanafunzi wamejiua kwa msongo wa mawazo, wengine wamekata tamaa na kuamua kuolewa, wengine kupata ujauzito, leo kwa uzembe wao wanataka kuwafaulisha wanafunzi ili kupata sifa kisiasa, haiwezekani,” alisema.
Akichambua maoni ya tume hiyo, alisema imeibua hoja ambazo yeye aliziwasilisha bungeni kupitia hoja yake binafsi ambayo ilizimwa na wabunge wa CCM kwa sababu za kulinda masilahi ya chama chao.
Alilishambulia Bunge kuwa limekuwa chanzo cha matatizo mengi kutokana na ubinafsi wa vyama bila kujali masilahi ya taifa.
“Bunge linaangamiza taifa kwa sababu ya itikadi. Hizi itikadi za vyama zinaliangamiza taifa. Kuna umimi, ubinafsi kwenye mambo ya masilahi ya taifa. Nawataka wabunge watoke usingizini,” alisema Mbatia.
Juzi serikali ilitangaza kufuta matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2012 na kuagiza yaandaliwe upya.
Uamuzi huo mgumu ulitangazwa bungeni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.
Akisoma tamko hilo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Lukuvi alisema uamuzi huo wa serikali umetokana na mapendekezo ya tume ya waziri mkuu iliyoundwa kuchunguza chanzo cha matokeo ya kidato cha nne mwaka jana kuporomoka kwa kiwango cha kutisha.
Matokeo ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2012 yalionesha kuwa kiwango cha ufaulu kimeshuka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na miaka ya hivi karibuni.
Matokeo yaliyotangazwa hivi karibuni, yalionesha kwamba kati ya wanafunzi 367,756 waliofanya mtihani huo, watahiniwa 126,847 ndio waliofaulu.
Katika idadi hii, wanafunzi waliofaulu katika daraja la kwanza hadi la tatu ni 23,520, sawa na asilimia 6.4 na daraja la nne ni 103,327, sawa na asilimia 28.1.
Watahiniwa 240,909, sawa na asilimia 65.5 ya wanafunzi wote, waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, walipata daraja sifuri.

Kuendela,bofya Read More

Friday, May 3, 2013

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI TUNDU LISSU, WIZARA YA KATIBA NA SHERIA.

Mh.Tundu Lissu.
MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA KATIBA NA SHERIA,
MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU (MB.)
KUHUSU
MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KWA MWAKA 2013/2014
(Kanuni ya 99(9) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2013)
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Ofisi ya Waziri wa Katiba na Sheria imeanzishwa kwa mujibu wa kipengele cha 12 cha Nyongeza ya Waraka wa Rais uliochapishwa kama Tangazo la Serikali Na. 494 la tarehe 17 Desemba 2010. Majukumu ya Ofisi hii yameainishwa katika Tangazo la Ukasimishaji wa Majukumu ya Kiuwaziri la mwaka 2010 (The Ministers [Assignment of Ministerial Functions] Notice, 2010) lililochapishwa katika Gazeti la Serikali kama Tangazo la Serikali Na. 494A la tarehe 17 Desemba 2010. Kwa mujibu wa Nyongeza ya Pili ya Tangazo hilo, pamoja na mengine, Ofisi ya Waziri wa Katiba na Sheria imekasimiwa majukumu ya masuala ya kikatiba, uendeshaji na utoaji wa haki, uendeshaji mashtaka na  haki za binadamu. Kwa sababu ya matukio ya hivi karibuni yanayohusu utendaji wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mchakato wa Katiba Mpya na kwa kuzingatia umuhimu wake katika mustakbala wa taifa letu, tunaomba kuanza na masuala yanayoihusu Tume na uendeshaji wake wa mchakato huo.
TUME YA MABADILIKO YA KATIBA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Mheshimiwa Spika,
Katika mwaka wa fedha 2012/2013, Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 33.944 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za Tanzania. Kwa mujibu wa Maelezo ya Makadirio ya Matumizi Mengineyo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 yaliyoletwa mbele ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala mwezi uliopita, hadi kufikia tarehe 25 Februari, 2013 Tume ilishapokea shilingi bilioni 18.473 kutoka Hazina na ilikwishatumia shilingi bilioni 14.968, sawa na 81% ya fedha zilizopokelewa. Kwa mujibu wa Maelezo hayo, shilingi bilioni 3.504 ambazo hazijatumika zimetengwa kwa ajili ya kulipia madeni kutokana na huduma za uchapishaji wa Mwongozo wa Mabaraza ya Katiba, uratibu wa mchakato wa kupatikana Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba na gharama nyingine za uendeshaji wa Ofisi.
Maelezo ya Tume yanaonyesha kwamba shillingi bilioni 15.471 ambazo hazijatolewa na Hazina zitatumika kwa ajili ya kusambaza nakala milioni moja za Rasimu ya Katiba Mpya (shilingi bilioni 3.848); elimu kwa umma juu ya Rasimu ya Katiba Mpya (shilingi milioni 400); kuratibu na kuendesha Mabaraza ya Katiba kwa nchi nzima (shilingi bilioni 4.734); na shilingi bilioni 6.488 kwa ajili ya matumizi mengine pamoja na ‘stahili za Wajumbe na Sekretarieti.’
Mheshimiwa Spika,
Katika Maoni yetu ya mwaka jana, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ililalamikia kile ilichokiita “... matumizi yasiyoelezeka na yasiyokubalika ya fedha za umma hasa hasa katika mazingira ambayo wananchi wanahubiriwa na watawala kwamba miradi ya maendeleo yao ya kiuchumi na kijamii haitekelezeki kwa sababu ya ufinyu wa bajeti ya Serikali.” Aidha, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ilidai kwamba shilingi bilioni 14.633 zilizotengwa kwa ajili ya kuwalipa wajumbe na watendaji wa Tume posho mbali mbali zilikuwa zinatishia kuigeuza “heshima ya kutumikia waliyopewa wajumbe wa Tume kuwa hongo ya Serikali.” Madai ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuitaka Serikali ieleze Bunge hili tukufu gharama zote za kila Mjumbe wa Tume, Sekretarieti na watumishi wengine wote wa Tume “ili Wabunge na wananchi wa Tanzania wafahamu kodi wanazolipa zinavyotumika katika mchakato wa Katiba Mpya” yalikataliwa na Serikali kwa hoja kwamba taarifa hizo ‘ni siri kati ya mwajiri na mwajiriwa.’
Mheshimiwa Spika,

Kuendelea Bonyeza Read More

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...