Waombaji wa fursa za ajira Serikalini kupitia Sekretarieti ya Ajira wametakiwa kuweka kumbukumbu sahihi za matangazo ya kazi wanazoziomba ili kurahisisha kujua ni tangazo gani aliomba pindi matangazo ya kuitwa kwenye usaili yanapotolewa.
Hayo yamesemwa na Bw. Lucas Mrumapili ambae ni Naibu Katibu wa Idara ya Ajira katika Sekretarieti ya Ajira wakati akitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wasailiwa waliofika ofisini kwake ili kujua majina ya kuitwa kwenye usaili wa nafasi za kazi za PPRA utafanyika lini.
Hayo yamesemwa na Bw. Lucas Mrumapili ambae ni Naibu Katibu wa Idara ya Ajira katika Sekretarieti ya Ajira wakati akitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wasailiwa waliofika ofisini kwake ili kujua majina ya kuitwa kwenye usaili wa nafasi za kazi za PPRA utafanyika lini.
Akijibu swali hilo alisema kuwa ofisi yake imejipanga vyema kuhakikisha kila tangazo linalotolewa usaili wake unafanyika kwa wakati. Hivyo kuwataka waombaji wa fursa za ajira kuwa wavumilivu wakati mchakato huo ukiendelea, ambapo alitolea ufafanuzi wa usaili wa matangazo husika akianzia tangazo la kazi la tarehe 28 Desemba, 2013 ambalo mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 14 Januari, 2014 kuwa usaili wake utafanyika mwisho mwa mwezi Aprili mwaka huu.
Mrumapili amesema kwa tangazo la tarehe 30 Desemba, 2013 ambalo mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 13 Januari, 2014 kuwa mchakato wake bado unaendelea kutokana na kuhitaji uchambuzi wa kina kwa kila kada maana baadhi ya waombaji kazi wa tangazo hilo kujirudia zaidi ya mara mbili.
Mrumapili amesema kwa tangazo la tarehe 30 Desemba, 2013 ambalo mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 13 Januari, 2014 kuwa mchakato wake bado unaendelea kutokana na kuhitaji uchambuzi wa kina kwa kila kada maana baadhi ya waombaji kazi wa tangazo hilo kujirudia zaidi ya mara mbili.




