Tuesday, June 4, 2013

REMEDIAL PROGRAMME - SAINT AUGUSTIN UNIVERSITY OF TANZANIA.

  
                                                        TANGAZO
Chuo cha Mtakatifu Agustino Tanzania kinawatangazia nafasi za kujiunga na Remedial Programme kwa mwaka wa masomo 2013/2014.Kozi hii ni kwaajili ya wale wote ambao alama zao hazifiki kiwango cha 4.5 katika kidato cha sita, ili kuwawezesha kupata elimu ya ziada iwasaidie kuendana na wanafunzi wenzao walio pata alama za 4.5 katika kidato cha sita.

Sifa za Muombaji:
1. Awe amemaliza kidato cha sita.

2. Awe na Principal Points kuanzia 2.5 hadi 4 kwenye masomo mawili ya kidato cha sita (mfano: EE, DE, CE, DD, EEE na masomo mengine kuwa na S).

3. Gharama ni Tshs. 390,000/= (Tuition Fee) kwa miezi 3, malazi (accommodation) ni Tshs. 70,000/=, chakula ni kujitegemea.

4. Wale wote wenye sifa hizo watakao chaguliwa na TCU kuja SAUT watatakiwa kufika chuoni miezi mitatu kabla ya tarehe ya kujiunga chuoni kwaajili ya kuanza masomo ya remedial.

5. Kozi hii itaanza tarehe 3/7/2013.

Fomu zinapatikana ofisi ya Admissions na kwenye tovuti (www.saut.ac.tz). Baada ya kumaliza kujaza fomu zirudishwe ofisi ya Admissions-SAUT. Wahitimu wataruhusiwa kujiunga na vyuo vyote vilivyo chini ya SAUT.

Wote mnakaribishwa.

Admissions Officer

TAMKO RASMI LA PUSH MOBILE KUHUSU MAUZO YA NYIMBO ZA MANGWEA


HAYA NDIO MAPOKEZI YA MWILI WA MANGEAR JIJINI DAR.











HOTUBA YA MWENYEKITI WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA, JAJI JOSEPH S. WARIOBA, KATIKA MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UZINDUZI WA RASIMU YA KATIBA TAREHE 03 JUNI, 2013 KWENYE VIWANJA VYA UKUMBI WA KARIMJEE, DAR ES SALAAM

Mhe. Dkt Mohammed Gharib Bilali – Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano,  
Mhe. Mizengo K. P. Pinda (Mb.) - Waziri Mkuu, 
Mhe. Seif Sharif Hamad – Makamu wa Kwanza wa Rais – Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, 
Mhe. Balozi Seif Ali Iddi (Mb.) - Makamo wa Pili wa Rais - Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, 
Mhe. Mathias Chikawe – Waziri wa Katiba na Sheria, 
Mhe. Abubakar Khamis Bakary - Waziri wa Katiba na Sheria wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, 
Mhe. Jaji Frederick M Werema - Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 
Mhe. Othman Masoud Othuman - Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, 
Viongozi wa Vyama vya Siasa, 
Waheshimiwa Wajumbe wa Tume na Wajumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, 
Ndugu Wananchi, 
Wageni Waalikwa, 
Waandishi wa Habari,
Mabibi na Mabwana,


UTANGULIZI 

Ndugu Wananchi,

Awali ya yote namshukuru mwenyezi mungu kwa kutuwezesha kufikia hatua hii ya leo ya kuzindua Rasimu ya Katiba. pia, niwashukuru ninyi nyote mliohudhuria halfa hii ikiwa ni mwendelezo wa mchakato muhimu wa Mabadiliko ya Katiba ya nchi yetu.

Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ilipitishwa Bungeni Novemba, 2011 na kufanyiwa mabadiliko Februari, 2012. Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliundwa kwa mujibu wa Kifungu 6(1) cha sheria hiyo (Cap.83). Wajumbe 34 wa Tume waliteuliwa na kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, mwezi Aprili, 2012. Kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Tume imepewa miezi kumi na minane kukamilisha kazi yake kuanzia siku ilipoanza kazi rasmi ambayo ilikuwa Mei 2, 2012.

Tume iliandaa ratiba ya utekelezaji wa majukumu yake. Kufuatana na ratiba hiyo Tume ilijipanga kukusanya maoni ya wananchi katika kipindi cha miezi mitano kuanzia Mwezi Julai hadi Disemba, 2012. Kazi hiyo ilifanywa kama tulivyopanga. Tume ilijigawa katika makundi na ilitembelea mkoa yote thelathini.

Tume ilifanya mikutano 1,942 ambayo ilihudhuriwa na wananchi wapatao 1,365,337 ambao kati ya hao wananchi 333,537 walitoa maoni ama kwa mazungumzo ya ana kwa ana au kwa maandishi. Tume pia ilipata maoni ya wananchi wengi, wa ndani na nje ya nchi kwa njia mbali mbali kama vile; Mikutano ya hadhara, Fomu maalum za Tume, barua kupitia Masanduku ya Barua ya Tume, Mitandao ya Kijamii ya barua pepe; facebook ya Tume, Tovuti ya Tume; Makala mbalimbali kutoka kwenye magazeti na ujumbe mfupi wa simu.

Tume ilitumia mwezi Januari, 2013 kukusanya maoni ya makundi mbali mbali katika jamii, ikiwa ni pamoja na vyama vya siasa, taasisi za Serikali, taasisi za dini, wakulima, wafugaji, wafanyakazi, asasi za kiraia na kadhalika. Makundi zaidi ya 160 yalikutana na Tume na kutoa maoni. Tume pia ilipata maoni ya viongozi wa juu wa Serikali walioko madarakani na waliostaafu. Kwa jumla viongozi 43walitoa maoni.

Tume ilipanga kutumia miezi mitatu ya Februari, Machi na Aprili kuchambua maoni ya wananchi na kuandaa Rasimu ya Katiba. Lakini tuligundua kwamba maoni tuliyopata yalikuwa mengi sana, na pamoja na matumizi ya teknolojia ya kisasa, tulitambua umuhimu wa kuongeza muda hadi mwisho wa mwezi Mei, Maoni ya wananchi yaligusa mambo yote yanayohusu Katiba na mengi ya maoni hayo yalikinzana. Aidha, baadhi ya maoni yaligusia masuala ya Kisera, Kisheria na Kiutendaji. Tulifanya uchambuzi makini na wa ndani wa maoni hayo na kazi hiyo tumeikamilisha na rasimu imeandaliwa na Tume na leo tupo hapa kwa ajili ya kuizindua, ambapo Wananchi watapata nafasi ya kuisoma. Kwa leo, kwa niaba ya Tume, napenda kutaja maeneo machache tu ambayo tunayapendekeza.

2.0. IBARA ZINAZOPENDEKEZWA KWENYE RASIMU YA KATIBA

Ndugu Wananchi,

Katiba yetu ya sasa ina ibara 152. Tume ilifanya jitihada kubwa sana kuandaa rasimu ambayo siyo ndefu. Lakini katika hali halisi haikuwezekana. Rasimu ya Katiba tunayopendekeza ina ibara 240.

3.0. MISINGI MIKUU YA TAIFA

Utangulizi wa Katiba ya sasa ndio unaobeba misingi mikuu ya Taifa ambayo ni Uhuru, Haki, Udugu na Amani. Tume inaamini kwamba misingi hii ni mizito na inastahili kubaki kwenye Katiba mpya. Hata hivyo, Tume imeona ni busara kuongeza misingi mingine mitatu ya Usawa, Umoja na Mshikamano. Hivyo, Tume imependekeza Katiba iwe na Misingi Mikuu saba ya Taifa;yaani; Uhuru, Haki,

Udugu, Usawa, Umoja, Amani na Mshikamano.

4.0. TUNU ZA TAIFA

Katiba yetu ya sasa haina sehemu inayoelezea tunu za Taifa (National Values). Wananchi wengi walitoa maoni kwamba Katiba itaje Tunu za Taifa. Tume imependekeza Tunu zifuatazo zitajwe ndani ya Katiba. Tunu hizo ni;- Utu,

Uzalendo, Uadilifu, Umoja, Uwazi, Uwajibikaji na Lugha yetu ya taifa ya Kiswahili.

Monday, June 3, 2013

MAPENDEKEZO YA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA HAYA HAPA.

Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania, imependekeza wawepo wagombea huru katika ngazi za uchaguzi mbalimbali . Hayo ni miongoni mwa mapendekezo yaliyotangazwa jijini Dar es salaam na Mwenyeketi wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba wakati wa uzinduzi wa Rasimu ya Kwanza ya Katiba Mpya.
Jaji Warioba amesema pia wapo wananchi waliopendekeza kwamba, wagombea huru waruhusiwe kugombea nafasi zote isipokuwa nafasi ya urais. Jaji Warioba amesema tume ilipitia maoni hayo na kupendekeza kwamba, wagombea huru waruhusiwe kugombea nafasi zote kuanzia ngazi ya Mwenyekiti wa Mtaa hadi nafasi ya Urais.
Kadhalika Jaji Warioba amesema, Tume pia imependekeza kwamba, mgombea yeyote wa Urais ili athibitike kuwa ni mshindi atalazimika kupata zaidi ya asilimia hamsini ya kura, na kwamba endapo mgombea hatafanikiwa kupata asilimia hamsini uchaguzi utarudiwa kwa kuangalia wagombea wawili waliopata kura nyingi.
Mapendekezo mengine yaliyotangazwa na Tume ni pamoja na kuwepo kwa serikali tatu yaani ya Bara,Zanzibar na ile ya Muungano.
Pia tume imependekeza kuwa, Bunge la Muungano liwe na jumla ya Wabunge 75, hamsini kutoka Bara, ishirini kutoka visiwani na watano wateuliwe na Rais kutoka makundi maalum ya walemavu.
Mapendekezo mengine ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ni pamoja na Rais kubakia na madaraka yake ya uteuzi wa viongozi wa ngazi za juu, lakini uteuzi wa ngazi za chini uachiwe Tume ya Utumishi.
Imeeleza kwamba, Rais mara baada ya kufanya uteuzi wa viongozi wa ngazi za juu wakiwemo, mawaziri, manaibu waziri, jaji mkuu na naibu jaji mkuu, viongozi hao watalazimika kuthibitishwa na Bunge.

SASA "SHOW" YA LADY JAYDEE NI JUNE 14.

Msanii muziki Lady Jaydee  ametangaza rasmi tarehe yake ya kufanya show ya miaka13 toka ameanza kufanya muziki kuwa ni siku ya Ijumaa ya Tarehe 14 mwezi Juni, baada ya kuaihirisha show yake kufuatia kifo cha Msanii Albert Mangwea kilichotokea siku ya tarehe 28 huko Afrika Kusini.
 
Lady Jaydee amesema sababu ya kuchagua siku hiyo ni kwamba siku ya Tarehe 13 atakwenda Mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili na siku inayofuta itakuwa show ya Miaka kumi na tatu (13) na tarehe 15 atasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
 
Lady Jay Dee  ametumia akaunti yake ya twitter kuiweka wazi tarehe ya show yake alipokua akijibu swali la fan wake ambae atasherehekea siku moja ya kuzaliwa na msanii huyo (June 15).

JOB VACANCIES - NATIONAL HOUSING CORPORATION.

NATIONAL HOUSING CORPORATION
                                                        JOB OPPORTUNITY
National Housing Corporation (NHC) is inviting applications from suitably qualified candidates to fill the position of manager in its Directorate of Business Development.

BUSINESS DEVELOPMENT MANAGER (1 POST) (Ref.No. DBM/02)
The Business Development Manager (BDM) reports to the Director of Business Development and has overall responsibilities for management and coordination of potential new business opportunities, thus generate information that facilitate decision making process. The decision parameters should be based on real estate market trends, market demands, trends and economic patterns that support strategic and tactical decisions for the National Housing Corporation (NHC).


SCHOLARSHIPS AT BOND UNIVERSITY IN AUSTRALIA, 2013/14.

Bond University offers international scholarships for undergraduate and postgraduate students in Australia. Applicants must currently be or have previously been in the top 5% of their high school or university class. These scholarships are available to international students who have demonstrated outstanding academic ability. International scholarships will cover 25% to 50% of tuition fees of any undergraduate or postgraduate degree (excluding Bond University’s Medical Program, Master’s of Psychology, Doctor of Physiotherapy).

Study Subject(s): Scholarships are provided for studying any one of the courses offered by Bond University in Australia.
 

Sunday, June 2, 2013

YANGA KUANZA MAZOEZI JUMATATU.

Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara 2012/2013 Young Africans  ambao pia ni Mabingwa watetezi wa kombe la Kagame. jumatatu wanatarajia kuanza mazoezi katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola Mabibo kujiandaa na mashindano ya kombe la Kagame yanayotarajia kuanza Juni 18 mwaka huu nchini Sudan.
Katika mashidano ya mwaka huu nchini Sudan , Yanga imepangwa katika kundi C lenye timu za Express FC (Uganda), Vitaloo FC (Burundi) na Ports FC (Djibout) ambapo kundi hili litakua katika mji wa El Fashir Kaskazini mwa jimbo la Darfur.
Yanga itaanza kutetea ubingwa wake Juni 20 dhidi ya timu ya Express ya Uganda, kisha Juni 22 itacheza na Ports ya Djibout kabla ya kumalizia mchezo wake wa mwisho katika makundi dhidi ya timu ya Vitaloo Juni 25 michezo yote ikifanyika katika uwanja wa El Fashir.
Mpaka sasa klabu ya Yanga imefanikiwa kukamalisha usajili wa mchezaji Mrisho Ngasa aliyekuwa akiitumikia Simba SC kwa mkopo akitokea timu ya Azam Fc ambapo mara baada ya msimu kumalizika amejiunga Yanga kama mchezaji huru.
Mara baada ya mchezo wa mwisho wa kukamilisha ratiba Kocha Mkuu Ernie Brandts alitoa mapumziko ya wiki mbili kwa wachezaji na benchi la ufundi kwa ajili ya kupata nafasi ya kujumuika na familia zao, ndugu zao kabla ya kurejea June 3 na kuanza maandilizi ya mashaindano hayo.
Young Africans ambayo ilitwaa ubingwa wa VPL ikiwa na michezo miwili mikononi inaanza mazoezi jumatatu asubuhi kuhakikisha inajiandaa vema kwenda kushindana na kurudi na kombe hilo kwa kulitwaa kwa mara ya tatu (3) mfululizo, ambapo mpaka sasa imeshalitwaa mara 5.

Saturday, June 1, 2013

UJUE UGONJWA WA MNYAUKO WA MIGOMBA.

 

banana xanthomonas wilt (BXW) (Xanthomonas campestris pv. musacearum)

Host plants / species affected
Ensete ventricosum (Abyssinian banana)
Musa (banana)
List of symptoms/signs
Fruit  -  ooze
Fruit  -  discoloration
Inflorescence  -  rot
Inflorescence  -  discoloration (non-graminaceous plants)
Inflorescence  -  premature ripening
Inflorescence  -  dieback
Leaves  -  abnormal colours
Leaves  -  wilting
Leaves  -  yellowed or dead
Leaves  -  ooze
Stems  -  internal discoloration
Stems  -  wilt
Stems  -  ooze
Vegetative organs  -  internal rotting or discoloration
Whole plant  -  plant dead; dieback
Whole plant  -  discoloration
Whole plant  -  wilt
 

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...