Saturday, June 1, 2013

DR.SLAA NA HECHE WAFUNIKA MOROGORO.


Katibu mkuu wa CHADEMA Dr.Wilbroad Slaa akiambatana na Mwenyekiti wa Vijana CHADEMA Ndg.John Heche leo wamehutubia umati mkubwa wa maelfu ya watu waliohudhuria mkutano huo katika viwanja vya Shule ya Msingi Kiwanja wa ndege/Saba saba.

Akiuhutubia umati huo zaidi zaidi ameongelea swala la amani ya nchi yetu ya Tanzania.Akiongea Dr. Slaa amesema kuhubiri majukwaani,makanisani,misikitini,mikutanoni,vikaoni,bungeni au mahala popote kuwa tuilinde amani yetu ya Tanzania na kumuomba mwenyezi mungu ni uongo mtupu ikiwa amani hiyo hujaitengeneza na kuisababisha iwepo.

Akiendelea kuhutubia amesema mfanyakazi,mama lishe/baba lishe, machinga,mwendesha boda boda,polisi au mtu yeyote hawezi kuwa na amani wakati hana uhakika na maisha yake kwa umaskini.

Dr.Slaa akijibu maswali yaliyoulizwa na baadhi ya watu waliohudhuria mkutano huo.

SCHOLARSHIP AT UNIVERSITY OF THE ARTS LONDON IN UK, 2013/14 .

Central Saint Martin’s College of Arts and Design of University of the Arts London is offering six MRes Art International Bursaries in UK. The bursaries cover tuition fees for first year students only. Home/ EU and International students are eligible for MRes funding. Students must be undergraduate and be accepted at the full-time MRes courses at the College for September 2013 academic year. Selection criteria for bursaries are financial need and academic merit. Applications should be submitted by post.

UDOM - Call for Paper,School of Humanities


The school of Humanities University of Dodoma plans to publish a second volume of its journal, the Journal  of humanities (JH) in October 2013.  This is to inform interested authors to submit papers by 15th July 2013.  

About the Journal
Journal of the Humanities (JH) is an international peer-reviewed trilingual broad-focused  Journal which aims to promote the exchange of ideas and foster interdisciplinary research in the human sciences. It publishes scholarly articles and reviews on cultures, history, anthropology, indigenous knowledge, literatures and languages, art and music, and other fields of the humanities that appeal to an international audience. Our primary goal is to generate intellectual dialogues between the traditional boundaries of knowledge and culture; we also seek to redefine, transform, and conflate such boundaries. 

NYARAKA ZINAZOONESHA NIA YA KUMVUA UBUNGE MH.TUNDU LISSU.











Friday, May 31, 2013

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE. SYLVESTER MHOJA KASULUMBAYI (MB) KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2012/13 NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGONA UVUVI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/14 (Inatolewa chini ya Kanuni ya 99 (9), ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Mwaka 2013)

A: UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, dira ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ni kuhakikisha kuwa raslimali za mifugo na uvuvi zinaendelezwa na kutunzwa katika mazingira endelevu kwa ajili ya ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.  Aidha dira inalenga kuhamasisha ufugaji wa kisasa na uvuvi endelevu ili kujenga uchumi endelevu kwa jamii nzima ya wafugaji na wavuvi na taifa kwa jumla.
Mheshimiwa Spika, Licha ya ukweli kwamba wafugaji na wavuvi wana mchango mkubwa katika uchumi wetu, Serikali hii ya CCM imeshindwa kuwapatia maeneo maalum kwa ajili ya malisho kwa maendeleo ya mifugo yao. Wafugaji wamekuwa wakihamishwa na au wakifukuzwa kutoka eneo moja la nchi hadi eneo lingine kama vile hawana haki ya kufanya shughuli za kiuchumi kama ufugaji katika nchi yao. Ni aibu kwa  Serikali kushindwa kuwapatia wafugaji mahitaji muhimu ambayo yangepelekea ufugaji wao kuwa wa kisasa, kibiashara na endelevu kama ilivyobainisha katika dira ya Wizara hii.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA, haioni sababu ya Serikali kuwapatia wafugaji maeneo ya kufugia  kwa kuwa wafugaji wangeweza  kuingia ubia na mashamba makubwa ya mifugo ambayo yalikuwa yanamilikiwa na Ranchi za Taifa, lakini kutokana na ubinafsi na ufisadi uliofichwa kwenye kivuli cha cha sera ya ubinafsishaji,  Serikali ya CCM imesimamia zoezi la  viongozi wa serikali na Chama cha Mapinduzi wakigawiana ranchi hizo na kuwaacha wafugaji wakifukuzwa ovyo na kupewa jina la wachungaji.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa wavuvi hali ni hiyo hiyo,  kwani mapato mengi ya Serikali  yanayokusanywa kutoka katika sekta ya uvuvi yanatokana na wavuvi wadogo ambao mara zote wao ndio waathirika wa mfumo kandamizi wa Serikali.  Zana za uvuvi zinapokamatwa, wao ndio wanapata hasara, lakini wauzaji wa zana hizo za uvuvi  wala hawaulizwi na wala hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi yao.
 Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa inayozikabili sekta hizi za ufugaji na uvuvi ni kwamba sekta  zote mbili hazina bima dhidi ya  majanga ambayo yanaweza kutokea.  Katika mazingira kama haya, dhana ya kuwa sekta za kisasa, kibiashara na endelevu inakuwa ngumu sana.
Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa mwaka wa fedha 2012/2013 liainisha mapungufu makubwa katika ya kiutendaji na kiuwajibikaji kwa wizara hii na kuitaka Serikali kufanya mambo yafuatayo:
1.      Kuwajibika kwa uzembe wa kuitelekeza meli ya uvuvi ya Tawariq iliyokamatwa ikifanya uvuvi haramu katika ukanda wa bahari ya hindi hadi meli hiyo kuharibika kabisa na kuanza kuzama bila faida yoyote?
2.      Kuchukua hatua dhidi ya mwekazaji wa Kagera Sugar kwa kushindwa kuendeleza shamba la ukubwa wa hekta 45,000 (sawa na ekari 112,500) kinyume na mkataba.
3.      Kueleza sababu za kuwapa mashamba makubwa wawekezaji wa kigeni na kuwanyanyapaa wafugaji wa asili kinyume cha sheria.
4.      Kutatua migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji ambayo mara kadhaa imesababisha uvunjifu wa amani na umwagaji damu miongoni mwa wananchi.
5.      Kujenga viwanda vya kusindika nyama katika mikoa ya wafugaji ili kuongeza thamani ya bidhaa ya nyama na hivyo kukuza uchumi.
6.      Kuweka wazi kiasi cha fedha kinachopatika kama mrahaba kutokana na uvuvi katika bahari kuu, pamoja na fedha za leseni kwa meli zinazofanya uvuvi katika ukanda wa bahari kuu.


WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2012.



BARAZA   LA MITIHANI  LA TANZANIA




WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA MTIHANI WA CSEE 2012


 1. Watahiniwa Kumi (10) bora Kitaifa:

NAFASI
NAMBA
JINA
JINSI
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0189-0063
SAID JUMA IRANDO
M
FEZA BOYS'   S  S  (DAR ES SALAAM)
2
S4459-0028
ALEX  ELIFAS
M
JUDE MOSHONO   S   S  (ARUSHA)
3
S0189-0039
JASPER GEOPHREY KAJIRU
M
FEZA BOYS'   S  S   (DAR ES SALAAM)
4
S2549-0086
MOSES J BOSCO
M
ALPHA SECONDARY    S  S (DAR ES SALAAM)
5
S4213-0074
YOHANA L MAYENGA
M
MARIAN BOYS' S   S  (PWANI)
6
S0239-0072
NGUSE  NGULUMBI
F
ST. FRANCIS GIRLS   S   S  (MBEYA)
7
S4213-0044
JOSHUA Z AZZA
M
MARIAN BOYS'  S    S  (PWANI)
8
S0189-0062
SAID ATWAYA NCHIMBI
M
FEZA BOYS'   S  S   (DAR ES SALAAM)
9
S0867-0134
LUPYANA L KINYAMAGOHA
M
PANDAHILL   S   S  (MBEYA)
10
S0101-0350
PETER SEREKA KICHOGO
M
AZANIA    S   S  (DAR ES SALAAM)



2.    Wasichana Kumi (10) bora Kitaifa

NAFASI
NAMBA
JINA
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0239-0072
NGUSE  NGULUMBI
ST. FRANCIS GIRLS   S  S   (MBEYA)
2
S0239-0078
SAMMOTA  CHUNGU
ST. FRANCIS GIRLS   S   S  (MBEYA)
3
S0239-0075
RAHMA  MKWATA
ST. FRANCIS GIRLS   S    S (MBEYA)
4
S0239-0018
DIANA  MGAYA
ST. FRANCIS GIRLS  S  S  (MBEYA)
5
S1060-0066
REBECCA J MWAMBEGELE
ST.MARY'S   S   S (DAR ES SALAAM)
6
S0239-0010
BELDA  THOMAS
ST. FRANCIS GIRLS  S   S  (MBEYA)
7
S0239-0002
AGNES  NTAPARA
ST. FRANCIS GIRLS   S  S  (MBEYA)
8
S0248-0045
JOANGELINE J BAMWENZAKI
MARIAN GIRLS   S  S   (PWANI)
9
S0298-0011
FATMA M MOSHI
FEZA GIRLS' S  S   (DAR ES SALAAM)
10
S0239-0045
JESCA  CHENGULA
ST. FRANCIS GIRLS   S  S  (MBEYA)


3.      Wavulana Kumi (10) bora Kitaifa


NAFASI
NAMBA
JINA
JINA LA SHULE NA MKOA
1
S0189-0063
SAID JUMA IRANDO
FEZA BOYS'   S    S  (DAR ES SALAAM)
2
S4459-0028
ALEX  ELIFAS
JUDE MOSHONO   S  S   (ARUSHA)
3
S0189-0039
JASPER GEOPHREY KAJIRU
FEZA BOYS'S   S   S   (DAR ES SALAAM)
4
S2549-0086
MOSES J BOSCO
ALPHA   S   S    (DAR ES SALAAM)
5
S4213-0074
YOHANA L MAYENGA
MARIAN BOYS'   S  S   (PWANI)
6
S4213-0044
JOSHUA Z AZZA
MARIAN BOYS'   S   S   (PWANI)
7
S0189-0062
SAID ATWAYA NCHIMBI
FEZA BOYS'   S  S  (DAR ES SALAAM)
8
S0867-0134
LUPYANA L KINYAMAGOHA
PANDAHILL   S   S   (MBEYA)
9
S0101-0350
PETER SEREKA KICHOGO
AZANIA     S   S   (DAR ES SALAAM)
10
S0692-0065
NORBERT S KIMARYO
ROSMINI    S   S   (TANGA)

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2013 HAYA HAPA.

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2013

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...