Friday, May 24, 2013

HARUNA NIYONZIMA ASAINI MKATABA WA MIAKA 2 YANGA.

Uongozi wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom  klabu ya Young Africans leo umekata mzizi wa fitina kwa kiungo mchezeshaji kutoka nchini Rwanda Haruna Niyonzima kuendelea kuitumikia timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili kufuatia kumalizika kwa mkataba wake awali.
Akiongea na waandishi wa habari makao ya klabu ya Yanga, katibu mkuu Lawrence Mwalusako amesema wameamua kumuongezea mkataba mchezaji huyo kufuatia kuuhitaji mchango wake kwani katika kipindi chake cha miaka miwili ameonyesha kiwango cha hali ya juu na kutoa mchango mkubwa.
 Mwalusako amesema kumekua yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikitoa taarifa za kupotosha juu yake ukweli leo umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuitumikia kwa miaka miwili.
Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.
Naye Niyonzima amesema anawashukuru wanachama, washabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga kwa kuwa naye muda wote, Yanga ni nyumbani kwangu kwani najisikia furaha kuichezea timu hii na malengo yangu ni kuisadia ili iweze kufanya vizuri katika upatashindano ya kimataifa.
Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu ya Yanga Abdallah BinKleb amesema palikua na propaganda nyingi juu ya Niyonzima, lakini ukweli ndio huu Niyonzima ataendelea kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili.
"Tunautambua mchango wake alioutoa kwa miaka mwili kwani ameweza kutupatia vikombe viwili vya Ligi Kuu ya Vodacom na Kombe la Kagame hivyo tumemuongezea mkataba wa miaka miwili tena ili aendelee kutoa mchango wake na kuisadia timu katika michezo ya kimataifa" alisema BinKleb

Thursday, May 23, 2013

CALL FOR INTERVIEW- IMMIGRATION

http://immigration.go.tz/downloads/TANGAZO%20LA%20KUITWA%20KWENYE%20USAILI-%202013%20-%20KIZUNGU%201.pdf

NAFASI ZA KAZI - UTUMISHI ZILIZOTANGAZWA 22.05.2013..

http://www.ajira.go.tz/index.php?option=com_docman&task=doc_details&Itemid=0&gid=147
Bofya link hapo juu kujua nafasi zilizotangazwa kwenye Taasisi zifuatazo: The Commission for Mediation and Arbitration (CMA), Forestry Training
Institute ( FTI), Eastern Africa Statistical Training Centre (EASTC), National Museum Of
Tanzania (NMT), Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), Dar es
Salaam Maritime Institute (DMI), Tanzania Airports Authority (TAA) and Sokoine
University of Agriculture (SUA) na ni jumla ya nafasi 171 ziko wazi zinahitaji kujazwa.

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA CHUO KIKUU MZUMBE 23-05-2013.

USAILI WA ANA KWA ANA UTAFANYIKA TAREHE 24-05-2013 CHUO KIKUU CHA MZUMBE-MAIN CAMPUS-MOROGORO KUANZIA SAA MOJA NA NUSU ASUBUHI
WASAILIWA WANATAKIWA KUFIKA NA VYETI HALISI (ORIGINAL CERTIFICATES
1. SUPPLIES ASSISTANT
EXAM NUMBER                 SCORES    REMARKS

PSRS SUP ASS MU - 1162     68.00     SELECTED
PSRS SUP ASS MU - 1158     61.20     SELECTED
PSRS SUP ASS MU - 1164     57.20     SELECTED
PSRS SUP ASS MU - 1166     24.00     NOT SELECTED

2. ASSISTANT ACCOUNTANT
EXAM NUMBER             SCORES    REMARKS
PSRS ASS ACC MU-1153     75     SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1105     70     SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1104     60     SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1110     60     SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1155     50     SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1101     45     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1097     45     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1124     45     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1125     45     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1130     45     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1100     40     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1102     40     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1106     40     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1115     40     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1127     40     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1137     30     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1094     20     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1114     20     NOT SELECTED
PSRS ASS ACC MU-1148     20     NOT SELECTED

LADY JAY DEE APOTEZA NAMBA ZA SIMU ZA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA LA FAMILIA 2.

 
Lady Jay Dee amekili kuwa amepoteza namba za waliochaguliwa kujiunga na La Familia 2 na kuwaomba wamtumie namba zao za simu tena ili waweze kuwasiliana kama alivyoandika katika mtandao wake wa kijamii:-

"LA FAMILLE 2

Habari ndugu zanguni.

Kwanza mtaniwia radhi, nimepoteza namba zote za simu mlizonitumia......Kutokana na sababu ambazo ziko nje ya uwezo wangu. Lakini majina ya wote waliochaguliwa kujiunga na La Famille 2 ninayo.

Hivyo basi naomba mniandikie tena e-mail ya namba zenu za simu tu. Ili tufahamishane ni lini tunaweza kukutana kwa mara ya kwanza pamoja...Na kupanga mikakati ya hapo baadae.

Niko katika wakati sio mzuri sana, ki muda na mambo mengine mengine...Hivyo mtanisamahe kwa kupoteza namba zenu za simu...Kichwa kimeelemewa.

Natumaini mtanielewa
Nasubiri kusikia kutoka kwenu, soon.
E-mail ni judyjaydee@yahoo.com
Natanguliza shukrani za dhati

JayDee"

SHORT COURSE - MUHIMBILI.

MUHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES
SCHOOL OF NURSE TEACHERS & SCHOOL OF NURSING MUHAS
PO BOX 65004, DAR ES SALAAM
TEACHING METHODOLOGY COURSE FOR EDUCATIONAL AND HEALH CARE PROFESSIONALS
INTRODUCTION
The school of Nurse Teachers in collaboration with School of Nursing all operating under MUHAS are conducting a course on Teaching Methodology Course for Educational and Health Care Professionals from 5th August to 13th September, 2013. Participants are encouraged to take the course in its totality. However, participants interested in one or two modules may do so by communicating with organizers through the given address below.

The training will be conducted in two separate classes, morning and evening classes of 6 weeks (272 hours) duration each.

Aim
The aim of the course is to prepare health personnel to become providers of quality health care and education services at any health care and educational institution in the country.


DIAMOND PLATNUMZ & NAY WA MITEGO KUFANYA USIKU WA MUZIKI GANI KUWA WA KIPEKEE ZAIDI NDANI YA MAISHA CLUB.

Katika hali ya kuweka matashititi kwa mashabiki wa Bongo Flavour & Hip Hop,Diamond Platnumz na Nay wa Mitego wamejipanga vilivyo kuakikisha wewe shabiki wa pande zote mbili unapata kitu roho inapeda....

Katika Usiku wa Nay wa Mitego & Diamond Platnumz ndani ya Maisha Club kutakuwa na vitu vingi sana vya hatari na vya kinyama sana kwa mashabiki wa Diamond na Nay....!!

Usikose kufika ndani ya Maisha club Siku ya Jumapili ya Tarehe 25.5.2013 kushudia mpambano mkali na kumaliza
utata kati ya watu hawa wawili......

Kama wewe ni Msafi au Mgumu,siku hiyo kutakuwa kuna WHITE CARPET & GREEN CARPET....Kama wewe ni msafiii unajua kuwa Muziki wa Bongo fleva ndio unakukosha na kukuliwaza ukiwa na Mtoto mzuri Nyumbani kwako.....Basi white Carpet itakuhusu sana kwa wale wasafi na warembo,Flowers za mjini watahusika sana pale........

Kwa wale wagumu......watoboa pua na waongeaji sana Basi GREEN CARPET itakuhusu sana kupita pale kutia support kwa Nay a Mitego mahana kura zitahanza kupigiwa pale pale na wahamuzi mtakuwa wenyewe kuona ni wangapi na wingi wa watu ulienda wapi........!!



Baada ya hapo ni ndani kuangalia show kali ambao aijawahi tokea kwa mara ya kwanza ndani ya Maisha club Nay wa Mitego & Diamond Platnumz watashambulia Jukwaa kwa hali ya tofauti kabisa...
USIKOSEEE SIKU HIII.....USISUBIRI KUADIDHIWA
 NJOO USHUUDIE NA KUJUA MUZIKI WA KWELI
BONGOLAND......
Proudly sponsored by Coca cola

EMPLOYMENT OPPORTUNITY - SHUWASA



SHINYANGA URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY (SHUWASA)

EMPLOYMENT OPPORTUNITY.

The management of SHUWASA is looking for qualified, competent, dynamic and committed Tanzanians to fill the following vacancies:-

1. INTERNAL AUDITOR

The successful candidate will be reporting to the Managing Director and will be performing his/her duty according the international Auditing standards.


Wednesday, May 22, 2013

HOTUBA YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI WIZARA YA NISHATI NA MADINI JOHN JOHN MNYIKA (MB) KUHUSU MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI JUU YA MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2012/2013 NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014.

 
 
HOTUBA YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI WIZARA YA NISHATI NA MADINI JOHN JOHN MNYIKA (MB) KUHUSU MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI JUU YA MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2012/2013 NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014 (Inatolewa chini ya kanuni ya 99(9) toleo la mwaka 2013)


A: UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Waziri wa Nishati na Madini ilianzishwa kwa mujibu wa kipengele cha 21 cha Nyongeza ya Waraka wa Rais uliochapishwa kama Tangazo la Serikali Na. 494 la tarehe 17 Desemba 2010. Majukumu ya Ofisi hii yameainishwa katika Tangazo la Ukasimishaji wa Majukumu ya Kiuwaziri la mwaka 2010 (The Ministers [Assignment of Ministerial Functions] Notice, 2010) lililochapishwa katika Gazeti la Serikali kama Tangazo la Serikali Na. 494A la tarehe 17 Desemba 2010.
Mheshimiwa Spika, Katika kujadili Mapitio ya Utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2012/2013 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2013/2014 naomba tuyatafakari maandiko ya katika muktadha wa uongozi wetu wa leo na hatma ya sekta hizi mbili muhimu za nishati na madini.
Mheshimiwa Spika, Mwalimu Nyerere katika kitabu chake cha TUJISAHIHISHE  katika ukurasa wa pili tutafakari  kwamba,  naomba kumnukuu  ‘ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo; haujali adui wala rafiki. Kwake wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa.Ukiniona nataka kulipiga teke jiwe kwa kuwa nafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nitalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa.
Mheshimiwa Spika, Tuendelee kutafakari maandiko ya Nyerere kwamba  Wakati mwingine, mtu tunayempinga huwa anamakosa kweli, lakini hoja tunazozitoa ni za kinafsi na hazihusiani kabisa na hoja zake.Nikisema mbili na tatu ni sita, nakosa. Lakini ni bora kunionyesha kwamba pengine nifikiri tunazidisha kumbe tunajumlisha.Ni kweli mbili mara tatu ni sita;lakini mbili na tatu ni tano, siyo sita. Lakini ukijaribu kuwashawishi wenzetu wakatae mawazo yangu na kukubali yako kwa kusema kuwa meno yangu ni machafu ,au natoa kamasi daima, utakuwa unatumia hoja ambazo hazina maana, Huu ni mfano wa upuuzi; lakini mara nyingi hoja tunazozitumia kuwashawishi watu wakatae mawazo ya wale tusiowapenda,au kukubali mawazo yetu, huwa haziuhusiani kabisa na mambo tunayojadili’.
Mheshimiwa Spika, Tutafakari maandiko ya Mwalimu Nyerere katika kitabu chake cha UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA  uk. 50,  nanukuu Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole, lakini ni kiongozi dhaifu; au upole wake na udhaifu wake unatumiwa na watu ambao wala si wema wala wapole kuhatarisha umoja na amani ya nchi yetu, Kipindi chake cha pili kinakaribia kwisha”.
Mheshimiwa Spika, Tutafakari maandiko mengine ya Mwalimu Nyerere kwamba “lakini hatulazimiki kuendelea na uongozi mbovu wa chama na Serikali. Wala tukiendelea na hali hii, bila kubadili uongozi wa Chama na Serikali, sina hakika kama tutafika huko salama.Masuala muhimu ya nchi yetu hayatashughulikiwa.Viongozi wetu wataendelea na matendo yao ya kuvuruga muungano. Matatizo ya kweli ya muungano hayatashughulikiwa, maana hatuna serikali ya kuyashughulikia.Na masuala mengine muhimu ya uchumi, huduma za umma, rushwa,chuki za uzawa na ukabilana udini yataachwa yajitatue yenyewe.Nasema , katika hili kama hiyo sina hakika kama tutafika salama;na tukifika “salama”,tukiwa na uongozi huu huu wa chama na serikali , mbele yetu kutakuwa ni giza tupu.Majuto ni mjukuu, huja baadaye.Tunaweza tukafikishwa mahali tukilinganisha uongozi wa rais Mwinyi na wa rais wa kesho tukaona kuwa chini ya Ndugu Mwinyi, Pamoja na udhaifu wake wote, tulikuwa peponi”!
Mheshimiwa Spika, Mwalimu Nyerere anaendelea kuandika kwamba  “Waingereza wana msemo  “Nature abhors vacuum”,  “hulka huchukia ombwe” . Hata siasa huchukia ombwe. Kama uongozi ni mbovu, upo kama haupo au upo kwa masilahi ya wenyewe, watatokea watu waujaze uwazi uliopo;hauwezi kuachwa wazi hivi hivi.Lakini uongozi mbovu ni kama mzoga, unatabia ya kukaribisha mafisi na mainzi. Tusidhani kuwa hulka ya siasa yetu ni tofauti na hulka ya siasa ya watu wengine; kwamba sisi tunaweza kuvumilia uongozi mbovu na tusivune matunda ya hulka ya uongozi mbovu”.
Mheshimiwa Spika, Mwalimu Nyerere alikuwa akiandika wakati wa awamu ya Rais Mwinyi kuhusu masuala yanayohusu Muungano; sisi tutafakari maandiko haya katika muktadha wa uongozi wa sasa wa taifa letu na mustakabali wa sekta nyeti kwa uchumi wa nchi na maisha ya wananchi za nishati na madini.
 

Matokeo ya Usaili wa Mchujo-TEA, 21 Mei 2013 .

EXAMINATIONS RESULTS FOR INFORMATION, EDUCATION AND COMMUNICATION OFFICER TANZANIA EDUCATION AUTHORITY (TEA)

Usaili wa ana kwa ana utafanyika tarehe 22-05-2013, saa moja na nusu asubuhi, katika ofisi za Tanzania Institute of Education-(TIE) Dar es Salaam.  
       
SN    EXAM NUMBER                          SCORE        REMARK
1      PSRS INFO ED COMM TEA -1066      82      SELECTED FOR ORAL INTERVIEW
2      PSRS INFO ED COMM TEA -1071      76      SELECTED FOR ORAL INTERVIEW
3      PSRS INFO ED COMM TEA -1058      75      SELECTED FOR ORAL INTERVIEW

4      PSRS INFO ED COMM TEA -1059      69      SELECTED FOR ORAL INTERVIEW
5      PSRS INFO ED COMM TEA -1067      69      SELECTED FOR ORAL INTERVIEW
6      PSRS INFO ED COMM TEA -1069      68      NOT SELECTED
7      PSRS INFO ED COMM TEA -1072      66      NOT SELECTED
8      PSRS INFO ED COMM TEA -1070      64      NOT SELECTED
9      PSRS INFO ED COMM TEA -1064      60      NOT SELECTED
10    PSRS INFO ED COMM TEA -1057      59      NOT SELECTED
11    PSRS INFO ED COMM TEA -1060      58      NOT SELECTED
12    PSRS INFO ED COMM TEA -1062      56      NOT SELECTED
13    PSRS INFO ED COMM TEA -1063      54      NOT SELECTED
14    PSRS INFO ED COMM TEA -1068      46      NOT SELECTED
15    PSRS INFO ED COMM TEA -1061      23      NOT SELECTED

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...