Wednesday, May 22, 2013

RAIS OBAMA KUITEMBELEA TANZANIA

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari ni kuwa Rais Obama anatarajia kuitembelea Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3.Na taarifa hiyo ni hii hapa:-

Tuesday, May 21, 2013

JOB VACANCY - OSHA


MAONI NA MAPENDEKEZO YA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) JUU YA RASIMU MUONGOZO ULIOTOLEWA NA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA KUHUSU MABARAZA YA KATIBA YA ASASI, TAASISI NA MAKUNDI YENYE MALENGO YANAYOFANANA.

1.0. UTANGULIZI
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83 (kifungu cha 18 (3)) imetoa wajibu kwa tume wa kuunda Mabaraza ya Katiba kwa ajili ya kupitia na kutoa maoni juu ya Rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na Tume.
Kifungu cha 17 (8) kinaeleza kuwa, isipokuwa kama mazingira yatahitaji vinginevyo, Tume itabuni utaratibu unaofanana ambao utatumika kila upande wa Muungano.
Kifungu cha 18 (6) kinaeleza aina nyingine ya Mabaraza ya Katiba kwa kueleza kuwa Tume inaweza kuruhusu Asasi, Taasisi au Makundi ya Watu kuwasilisha maoni yao kuhusu Rasimu ya Katiba.

LEO MEI 21,KUMBUKUMBU YA AJARI YA MELI YA MV.BUKOBA.

LEO ni Mei 21 siku ambayo Taifa linaingia kwenye kumbukumbu chungu ya kutimia miaka 17 tangu kutokea kwa ajari mbaya ya Mv Bukoba iliyochukua maisha ya Watanzania zaidi ya 300 waliokuwa wakisafiri kutoka Bukoba kuelekea jijini Mwanza.
Mara kadhaa watu wachache  walionusurika katika  ajari hiyo wamekuwa wakijitokeza kutoa ushuhuda wao jinsi mambo yalivyokuwa wakati  Meli hiyo ilipopinduka ikiwa inakaribia kuingia  Bandari  ya Mwanza.
Kitu cha  ajabu  ni kuwa  mpaka leo  serikali inaonekana bado iko usingizini katika  kuweka umakini  kwa vyombo vya usafiri nchini  jambo linalofanya  kuwepo kwa  ajari za  mara kwa mara  zinazogharimu maisha ya  watanzania wengi  kwa uzembe wa watu wachache.
Siku za hivi karibuni tumekuwa tukishuhudia ajari mbaya za barabarani na majini ambazo zimekuwa zikiacha historia na majonzi kwenye familia mbalimbali,pia kupoteza nguvu kazi ya taifa. 
Makaburi ya pamoja ya Ndugu zetu yaliyo Igoma-Mwanza.

Monday, May 20, 2013

HIVI NDIVYOILIVYOKUWA LEO MAHAKAMANI IRINGA WAKATI MCH.MSIGWA AKIPELEKWA MAHAKANI.




WATU 31 WAUAWA KATIKA SHAMBULIO LA BOMU IRAQ.


Kiasi  watu  20 wameuwawa  katika  wimbi  la  mashambulio  ya mabomu  yaliyowekwa  katika  magari  katika  wilaya  inayoishi waumini  wengi  wa  madhehebu  ya  Shia  katika  mji  mkuu  wa  Iraq , Baghdad, leo.  Watu   wengine  11  wameuwawa  katika mashambulio  katika  mji  wa  kusini  wa  Basra.  Watu  kadha wameuwawa  katika  mashambulio  katika  muda  wa  wiki  moja iliyopita   wakati  hali  ya  wasi  wasi  inaongezeka   kati  ya Waislamu  wa  madhehebu  ya  Sunni  ambao  ni  wachache  nchini humo  na  Washia  waliowengi, ambao  hivi  sasa  wanashikilia madaraka  ya  serikali  ya nchi  hiyo. Idadi  ya  mashambulio imepanda  mno  tangu majeshi  ya  Marekani  kuondolewa  Desemba mwaka  2011.
Polisi  na  wafanyakazi  wa  Hospitali  wamesema  kuwa mashambulio  manane  ya  mabomu  yaliyotegwa  katika  magari katika  wilaya  ya  Washia  mjini  Baghdad , yamesababisha  vifo vya  watu  wapatao  20  leo.

Source: DW

Scholarships - Victoria Doctoral Scholarships New Zealand, 2014


Victoria University of Wellington is offering up to 35 doctoral scholarships for the year 2014. Scholarships are open to New Zealand and international students in any discipline. The award covers $23,500 stipend annually + tuition fees. These Scholarships are intended to encourage and support Doctoral study (PhD) at Victoria University of Wellington. As part of the requirements of this Scholarship, the recipient is expected to contribute 150 hours per annum to the academic life of the School in which they undertake study. The application deadline is 1 July and 1 November 2013.


CCM YAKAA NA WABUNGE WAKE DODOMA

Chama cha Mapinduzi (CCM) jana tarehe 19.05.2013 kilifanya kikao chake na wabunge wa CCM kikiongozwa na Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma .

M/kiti wa CCM Taifa Rais J.K.Nyerere akitoa maelekezo kwa wabunge.

HIZI NDIZO MBWEMBWE ZA YANGA BAADA YA KUWAFUNGA SIMBA JUZI.


WATU 4 WAFA NA 13 KUJERUHIWA KATIKA MSONGAMANO KANISANI.

Waumini wakiwa kanisani.
Watu wane wamekufa na 13 kujeruhiwa katika mkanyagano ndani ya kanisa la kiavengalisti nchini Ghana.
Ajali hiyo ilitokea pale waumini walipoania kufikia maji matakatifu katika tawi la kanisa la Synagogue Church of All Nations (SCOAN) katika mji mkuu, Accra.
Ripoti zinasema maelfu ya watu walikuwa wamekwenda kanisani humo.
Kanisa hilo liloanzishwa na kasisi wa Nigeria, TB Joshua, ambaye anasema yeye ni mtume.
Piya amezusha utata kwa kudai kuwa anaweza kutibu magonjwa yasiyotibika kama HIV na UKIMWI.

SOURCE: BBC

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...