Friday, April 19, 2013

SPIKA AWATOSA CHADEMA,ABARIKI ADHABU WALIYOPEWA.

Leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu Mh Spika ametoa uamuzi kuhusu muongozo ulioombwa na Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni kuhusu uhalali wa kutolewa nje na kisha kufungiwa vikao vitano kwa wabunge sita (6) wa Chadema uliotolewa juzi na Naibu Spika. 
 
Mh Spika anasema kwa kuwa kwa sasa hakuna kanuni kuhusu jambo hilo uamuzi wa Naibu spika utabaki halali na utaingizwa kwenye kumbukumbu za bunge kwa ajili ya kutumika huko mbele kwa ajili ya maamuzi pale itakapotokea tukio kama hilo.
 
Kwa uamuzi huo Wabunge hao watakosekana bungeni kwa siku tano ambazo ni Alhamisi (jana), Ijumaa (leo) pamoja na Jumatatu, Jumanne na Jumatano wiki ijayo.


Uamuzi wa Naibu Spika Mh. Job Ndugai, wa kumtoa nje Mh. Lissu na wengine  watano na kupewa adhabu ya kutoshiriki vikao vitano vya Bunge umebarikiwa na Mheshimiwa Spika..
 Hivyo Basi, maamuzi ya Mh. Ndugai, yatakua kanuni rasmi kwa tukio kama hilo na adhabu iliyotolewa.

KIPANYA NA BUNGE LA TANZANIA

Umeonaehhhhhhh!!!!!!

MWAKYEMBE-SERIKALI HAITAWAVUMILIA WAKANDARASI WABABAISHAJI

 Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amesema Serikali haitawavumilia makandarasi wababaishaji  na wanaokiuka mikataba yao pindi wanapopata zabuni za kutekeleza miradi mbalimbali  nchini.
Pia, alitoa onyo kwa makandarasi wababaishaji ambapo amesema hatavumilia kuona Tanzania inafanywa kichaka cha watu wanaokuja kuchota fedha za bure na kuondoka pasipo kutimiza majukumu yao, ambayo yanakuwa yameainishwa kwenye mikataba wanayoingia na Serikali.
Waziri Mwakyembe alisema hayo  Dar es Salaam jana wakati akishuhudia   Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) ikisaini mkataba wa ujenzi wa jengo  la tatu la abiria kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA).
Akizungumza katika halfa  hiyo, Mwakyembe alisema ujenzi wa jengo hilo ni faraja kubwa kwa Serikali ya Tanzania, kwani litasaidia kuongeza ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa Watanzania.
Alisema licha ya Serikali kupongeza jitihada hizo za TAA asingependa kuona ujenzi wa jengo hilo ukifanywa chini ya kiwango kwani huu ni wakati wa kuhakikisha kila kitu kinachofanyika nchini kinafanywa kwa viwango vya hali ya juu. Mwakyembe aliiagiza TAA kusimamia mradi huo uweze kumalizika kwa muda uliopangwa na kwamba idhibiti ubadhirifu wowote wa mali zitakazotumika katika mradi huo.
Akizungumza baada ya kutia saini mkataba huo Kaimu Mkurugenzi wa TAA, Suleiman Suleiman alisema ujenzi huo utafanyika kwa awamu mbili na kwamba hadi kukamilika kwa jengo  hilo litakuwa na uwezo wa kuchukua abiria milioni sita. “Jengo la abiria lina uwezo wa kuchukua abiria zaidi ya milioni moja lakini tunapata faraja kwamba pindi ujenzi huu utakapo kamilika uwanja wa JNIA utakuwa na uwezo mkubwa wa kuchukua abiria wengi na kwamba ni faida kwa uchumi wa nchi yetu,”alisema Suleiman.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bam International Martin Bellamy alisema wamepata faraja kushinda zabuni hiyo na kwamba wao kama wenyeji hapa nchini watahakikisha wanafanikisha mradi huo. Jengo hilo linajengwa na Kampuni ya Bam Inenationali ya Uholanzi kwa gharama ya Sh275 bilioni ambapo hadi kukamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua abiria milioni sita.

Chanzo, Mwananchi.

HATIMA YA TUNDU LISSU BUNGENI LEO.

Spika wa Bunge,Mh.Anne Makinda.
 Spika wa Bunge, Anne Makinda amesema leo atatoa mwongozo kuhusu tukio la Naibu Spika, Job Ndugai kuwasimamisha wabunge sita wa Chadema.
Juzi, Ndugai aliwasimamisha wabunge hao Tundu Lissu (Singida Mashariki), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiah Wenje (Nyamagana) na Godbless Lema wa Arusha Mjini kutohudhuria Bunge kwa siku tano kutokana na alichokiita kufanya vurugu ndani ya bunge.
Hatua hiyo ya Spika Makinda imekuja baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kumtaka aeleze Ndugai alitumia kanuni gani kuwasimamisha wabunge hao.
Jana, baada ya kipindi cha maswali na majibu, Mbowe alisimama na kuomba mwongozo wa Spika akitumia Kanuni ya 68(7) inayosema; “Hali kadhalika, Mbunge anaweza kusimama wakati wowote ambapo hakuna mbunge mwingine anayasema na kuomba “Mwongozo wa Spika” kuhusu jambo ambalo limetokea bungeni mapema, ili Spika atoe ufafanuzi kama jambo hilo linaruhusiwa au haliruhusiwi kwa mujibu wa Kanuni za Bunge na majibu ya Spika yatatolewa papohapo au baadaye, kadri anavyoona inafaa.”
Mbowe alisema Kanuni ya 73(3) ndiyo inayompa ruhusa Naibu Spika na Spika kuwasimamisha wabunge na aliisoma: “Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa maneno aliyoyasema na hadi kufikia mwisho wa muda alipopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anaweza kumsimamisha mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi vitano.
“Kwa mujibu wa yaliyotokea jana (juzi) ilitokea sintofahamu katika matumizi ya kifungu hiki wakati tulitegemea Kifungu cha 74(1) ndicho kingetumika kwani kama mbunge amedharau mamlaka ya Spika jina lake linaweza kupelekwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,” alisema Mbowe na kuongeza: “Mheshimiwa Spika nataka mwongozo wako kujua Naibu Spika alitumia kanuni gani?”
Awali, Spika Makinda aliahidi kutoa mwongozo wake baadaye jioni kabla ya kuahidi kufanya hivyo leo wakati akiahirisha shughuli za Bunge jana.
Awali, baada ya mwongozo wa Mbowe, Spika Makinda alimruhusu Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kuomba mwongozo wake na aliposimama alisema: “Mwongozo wangu uko palepale katika kanuni ileile iliyoombwa na kiongozi wa kambi ya upinzani.”
Kabla hajamaliza, Spika alimkatisha na kumweleza kuwa hawezi kutoa nafasi ya mwongozo wa kitu hichohicho.
Alimruhusu Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema ambaye alisema: “Waandishi walioandika kanuni hizi kwamba jambo lilitokea mapema hawakumaanisha jana.”
Kabla Jaji Werema hajamaliza, Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika alisimama lakini Spika alimzuia na kuwakatisha wote akisema: “Waheshimiwa wabunge, hakuna kitu kinachowaharibia wananchi kama kilichotokea jana (juzi), jana (juzi) hakuna kitu kilichojadiliwa zaidi ya kuleta zahama.”
Nchemba tena
Alimruhusu Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba kuendelea kutoa mchango wake ambao ulikatishwa kutokana na vurugu za juzi na jana nusura tena tafrani izuke kati yake na Mnyika hasa baada ya Nchemba kueleza suala la mabaraza ya Katiba kuwa utaratibu ulipitishwa bungeni na wabunge wote.
Alisema kinachotaka kujengwa na wapinzani hakipo kwa kuwa katika Jimbo la Karatu lililoko chini ya upinzani, wenyeviti wa mabaraza ya Katiba walichaguliwa wa CCM.
 
Mnyika alisimama akitaka kumpa taarifa Nchemba kwa kutumia Kanuni ya 63(1) akisema Mwigulu kueleza kuwa utaratibu wa kutumia mikutano ya maendeleo ya kata kuchuja wajumbe wa mabaraza WDC ulipitishwa na Bunge ni uongo kwa kuwa utaratibu huo ulipitishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Spika alimruhusu Nchemba kuendelea kuchangia, ndipo aliposema: “Tunapoongea watoto wa kiume watulie.”
Kauli hiyo ilikataliwa na Spika Makinda ambapo alimtaka Nchemba kuifuta... “Naifuta mheshimiwa Spika,” alisema Nchemba.

Chanzo, Mwananchi.

MBOWE AHOJI UHALALI WA NEC KUANDAA MFUMO MPYA WA KUHESABU KURA.

 
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amehoji hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kuandaa mfumo mpya wa kisasa wa uhesabuji kura bila kuwashirikisha wadau.
Kutokana na hali hiyo, Mbowe aliitaka serikali kusitisha mchakato huo wa NEC hadi sheria itakapotungwa na kushirikisha vyama vya siasa.
Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani na Mbunge wa Hai, alitoa kauli hiyo jana wakati akiuliza swali katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Akifafanua zaidi, Mbowe alisema kuna taarifa kwamba NEC imeanza kufanya maandalizi ya uhesabuji kura kutumia mfumo wa kisasa kama ule wa Kenya na Ghana.
Alisema mfumo huo wa kisasa wa uhesabuji kura umeshindwa kufanya kazi nchini Kenya na Ghana na kusababisha msumbufu mkubwa.
“Mheshimiwa Spika, mfumo huo ulifanyika nchini Kenya, lakini ulivurugika na kuamua kutumia mfumo wa zamani wa kuhesabu kura. Wadau wasiposhirikishwa katika hatua za awali, hautaweza kuaminika,” alisema.
Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu, Pinda, alisema ipo mifumo mingi ya uhesabuji kura, lakini hapa nchini kwa muda mrefu mfumo uliokuwa ukitumika ni ule wa kuhesabu kwa mkono.
“Hivi sasa baadhi ya nchi kama Kenya wanatumia mfumo wa kisasa. Nia ya NEC ni nzuri na bila shaka watakuwa na njia mbadala kama huu wa kisasa utashindwa kama walivyofanya wenzetu Kenya,” alisema Pinda.
Akiuliza swali la nyongeza, Mbowe alisema kwa kuwa mfumo huo ulishindwa Kenya na Ghana na kwa kuwa wadau hawakushirikishwa, waziri mkuu atakuwa tayari kutangaza kusitisha mchakato huo hadi sheria itakapopitishwa na kushirikisha wadau?
Akijibu swali hilo, Pinda alisema kuwa swali la Mbowe linatokana na hofu ambayo alisema haipo kwani hata kura zikihesabiwa kwa vidole hofu hiyo ilikuwa kubwa zaidi.
“Mimi nadhani tuamini kabisa kama NEC ina nia njema kwani imesheheni wataalamu wa aina mbalimbali. Ila hili la wadau kushirikishwa nitawasilisha wazo hilo tuone namna ya kuendelea vizuri na jambo hili,” alisema.
Katika hatua nyingine, Pinda alisema kuwa serikali itaruhusu shughuli za kisiasa katika mikoa ya Lindi na Mtwara hadi hapo hali kuhusu mzozo wa gesi itakapokuwa shwari.
Alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mkanyageni, Mohamed Mnyaa (CUF).
Mnyaa alihoji kwanini serikali ilipiga marufuku ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, katika mikoa ya Lindi na Mtwara wakati wengine wanaruhusiwa.
Akijibu swali hilo, Pinda alisema ziara ya Maalim Seif ilikuwa ya kisiasa na ndiyo maana alizuiliwa na viongozi wengine wote wa kisiasa wamezuiliwa.
“Hali itakapokuwa shwari, shughuli za kisiasa zitarejeshwa hivi karibuni na Maalim Seif na wengine wataruhusiwa kwenda kufanya kazi za kisiasa. Kwa sasa hapana,” alisema.

MBOWE AMBANA SPIKA KUWA NI KANUNI IPI ILITUMIKA KUWATOA WABUNGE WA CHADEMA.

WAKATI wabunge sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakianza kutumikia adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge la Bajeti vinavyoendelea mjini hapa, utata mkubwa umeibuka juu ya kanuni alizotumia Naibu Spika, Job Ndugai, kutoa adhabu hiyo.
Utata huo ulibainika jana wakati Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Freeman Mbowe, alipoomba mwongozo wa Spika Anna Makinda, kutaka kujua kanuni aliyotumia Ndugai wakati hakuna kanuni iliyomruhusu kutoa adhabu hiyo.
Baadhi ya wabunge pia walihoji kifungu kilichotumika hata kama wabunge hao walikosea.
Miongoni mwa waliohoji adhabu hiyo, wapo baadhi ya wabunge wa CCM ambao hawakupenda kutaja majina yao, wakisema kuwa uamuzi wa Naibu Spika ulitawaliwa na jazba za kibinadamu badala ya kufuata kanuni zinazoliongoza Bunge.
Katika mwongozo wake jana kwa Spika Makinda, kiongozi huyo wa kambi ya upinzani alihoji kifungu kilichotumika kuwaadhibu wabunge wake.
 
Mbowe alisema juzi wakati Bunge lilipokuwa katika kipindi chake cha jioni, wabunge sita wa CHADEMA waliotolewa nje kwa maelekezo ya Naibu Spika, Job Ndugai.
Aliwataja wabunge waliotolewa kuwa ni Tundu Lissu (Singida Mashariki), Haghness Kiwia (Ilemela), Ezekia Wenje (Nyamagana), Godbless Lema (Arusha Mjini), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini) na Pete Msingwa (Iringa Mjini).
“Na wabunge hawa walipotolewa, walipewa vile vile adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge, adhabu iliyotolewa papo kwa papo na Naibu Spika.
“Kwa mujibu wa kanuni zetu, kanuni inayompa Naibu Spika au Spika mamlaka ya kumtoa mbunge kwa siku tano ni kanuni ya 73 ya kanuni ndogo ya tatu ambayo inahusu mbunge ambaye atashindwa kutoa vielelezo vya aidha kusema uongo ambayo inasema hivi: “Endapo mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha maneno aliyoyasema na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa, ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anaweza kumsimamisha mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi vitano,” alinukuu.
Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA, alisema yaliyotokea bungeni juzi ni sintofahamu kati ya wabunge na kiti cha Spika ambapo katika mambo ya msingi CHADEMA ilitegemea kifungu cha nne cha kanuni za Bunge, kifungu kidogo cha kwanza kingetumika.
Kifungu kinasema: “Spika anaweza kutaja jina la mbunge kwamba amedharau mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya Haki na Maadili ya Bunge.
“Ikiwa kwa maneno au vitendo, mbunge huyo anaonyesha dharau kwa Spika au atafanya kitendo chochote cha makusudi cha kudharau shughuli ya Bunge au mbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo.”
Kutokana na kanuni hiyo, Mbowe aliomba mwongozo wa Spika kutaka kujua wabunge hao walitolewa kwa kanuni gani na ni lini wataweza kurejeshewa haki yao ya kurejea ndani ya Bunge.

Vituko vya juzi
Baadhi ya askari walioamriwa kuingia ndani ya Bunge, walisema hawakuwa tayari kumtoa Lissu kwa nguvu ndio maana walitumia muda mrefu kutimiza agizo hilo.
Askari hao walisema hofu yao ilikuwa ni usalama wa Waziri Mkuu kwani endapo vurugu zingeibuka, angekuwa katika wakati mgumu kiusalama.
Baada ya Lissu na wabunge wenzake kutoka nje ya ukumbi chini ya ulinzi, askari hao walipata wakati mgumu kuwatoa nje ya eneo la Bunge.
“Tulipanda juu hadi kwenye ofisi ya Lissu, alipofika alikaa chini, akafungua kompyuta yake, baadaye akaizima wala hakuwa na haraka na sisi wakati huo tulibaki tumesimama tu.
“Baadaye aliizima, akachomoa waya  na kuziingiza kwenye begi lake, kisha alisimama taratibu na kuondoka kama vile hakuna jambo lililotokea,” alisema askari huyo.
Wenyewe wanena
Lema alisema: “Nimepokea kwa furaha adhabu hii kwa sababu imetokana na kupigania haki na ukweli ndani ya Bunge. Kwa hiyo adhabu hii kwangu ni baraka.”
Alisema uonevu wa wazi uliofanywa na Naibu Spika, Job Ndugai, baada ya muda kidogo Tanzania itashangilia ushindi mkubwa. Kwamba Watanzania watafurahia vijana wao na watoto wao walioshinda hofu.
“Ushahidi nilioombwa kuhusu mwenyekiti wa CCM kuwa mwasisi wa udini ninao, tena wa uhakika wa nguvu na imara na niko tayari kuutoa mbele ya Bunge kwa kuwa nilitoa maneno hayo mbele ya Bunge.
“Sitapeleka tena ushahidi wangu vichochoroni kwa kuwa nilipeleka ushahidi wangu kwa Spika kuhusu uongo wa Waziri Mkuu, walipiga chenga hadi wakanivua ubunge,” alisema.
Lema alidai kuwa ametumiwa meseji za vitisho kwamba wangelimuonyesha tena mahakamani, lakini akasema wafanye wafanyavyo ila moyo wake una furaha kuwa amesema yale ambayo wengine wameogopa kuyasema.
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, alisema: “Bunge letu lina matatizo, halina mwelekeo. Job Ndugai anajidai yeye ndiye kiongozi wa serikali.”
Alisema kama Ndugai ana sifa hizo na anajiandaa kuwa Spika wa Bunge lijalo, anamwomba Mungu asiwe mbunge katika Bunge hilo.
“Tusi lililotolewa na Peter Serukamba wa CCM, lilikuwa kubwa kuliko matusi yote yaliyowahi kutolewa ndani ya Bunge katika mabunge ya Jumuiya ya Madola.
“Hili lilihitaji adhabu, lakini kitendo cha Naibu Spika kumtimua Lissu ambaye alikuwa anafuata kanuni ni cha kusikitisha sana,” alisema.
Mbilinyi alisema wananchi wa Mbeya Mjini hawakumtuma kushangilia bungeni.
Kwa upande wake Mchungaji Msigwa alisema: “Adhabu hii ni ya hovyo kwa sababu haikufuata taratibu; wamegeuza Bunge kama sehemu ya serikali.”
Alifafanua kuwa kama angepata adhabu iliyofuata kanuni asingekuwa na shida, angeipokea kwa furaha.
“Naibu Spika ana jazba, anapaswa apate mafunzo ya jazba zake. Viongozi wa Bunge wamejaa u-CCM zaidi kuliko utaifa. Binafsi sitajali kufukuzwa, ninachotaka haki itendeke,” alisema.
Mbunge wa Ilemela, Kiwia, alisema adhabu waliyopewa ni kinyume cha kanuni.
“Adhabu hiyo anapaswa apewe mtu aliyesema uongo na kushindwa kuthibitishwa, pamoja na hayo kanuni zifanye kazi kwa wabunge kwa usawa,” alisema.
Kiwia aliongeza kuwa kanuni hazipaswi kuwaona wabunge wengine wana haki na wengine hawana; kwamba hoja za msingi zijibiwe, maamuzi bungeni yasifanyike kwa mabavu.
Naye Lissu ambaye ni mwanasheria kitaaaluma, alisema hajui ni kanuni gani iliyotumika na kumwadhibu na kwa kosa gani.
 
Chanzo, mtando wa kijamii wa CHADEMA

Thursday, April 18, 2013

REAL MADRID KLABU TAJIRI DUNIANI, YA PILI MAN UNITED

 Manchester United wameondolewa kwenye nafasi ya kwanza ya klabu yenye utajiri na thamani kubwa inayotolewa na jarida la Forbes.

United wamekuwa wakishika nafasi ya kwanza kila mwaka tangu Forbes walipoanza kutoa list ya vilabu vye thamani kubwa zaidi duniani mwaka 2004, lakini mwaka huu wameondolewa kileleni na Real Madrid - klabu ambayo iliitoa kwenye michuano ya champions league hive karibuni.

Barcelona wanashika nafasi ya tatu nyuma ya United, Arsenal wapo nafasi ya nne na mabingwa wa Bundesliga Bayern Munich wakikamilisha nafasi ya tano.

Real Madrid wanatajwa kuwa na thamani ya £2.15billion - na kwa namba hizo klabu hiyo ya Spain inakuwa ndio klabu ya michezo yenye thamani kubwa zaidi duniani - huku Manchester United wakiwa na thamani ya  £2.07billion.

Kwa upande wa wachezaji wa soka, David Beckham bado anaongoza kwa utajiri akiwa ameingiza kiasi cha kati ya £33m - £29m ambazo zimetokana zaidi na mikataba ya kibiashara ya matangazo.

Staa wa Real Madrid Ronaldo ameingiza kiasi cha (£28.8m) akishika nafasi ya pili, wakati mwanasoka bora wa dunia Lionel Mess akishika nafasi ya 3 kwa kuingiza jumla ya £26m mwaka jana kwa kupitia mshahara na mikataba ya kibiashara.

MAKOCHA WA AZAM, FAR RABAT KUNENA KESHO



Makocha wa timu za Azam, Stewart John Hall na AS FAR Rabat ya Morocco, Abderazzak Khairi watakutana na waandishi wa habari kesho (Aprili 19 mwaka huu) kuzungumzia mechi yao itakayofanyika Jumamosi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mkutano huo ambao pia utawahusisha manahodha wa timu hizo mbili utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Barabara ya Uhuru na Shaurimoyo.

Timu hizo zitakutana katika mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho itakayoanza saa 10 kamili jioni. Mechi ya marudiano itachezwa nchini Morocco wiki mbili baadaye.

KIPANYA AZIDI KUKOMAA NA MATUSI YA BUNGENI

Tafakari na chukua hatua.

JOB VACANCIES TBC.

Director General Clement Mshana
  TANZANIA BROADCASTING CORPORATION (TBC)
The Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) is a Public Service Broadcaster established by Government Order in 2007 and became operational on 1st July, 2007 replacing the then Tanzania Broadcasting Services which was established in the year 2002 pursuant to Public Corporation Act No 2 of 1992, Government Notice No 20 of 14th June 2002.
7.1
GRAPHIC DESIGNER AND ASSISTANT IT OFFICER
GRADE I
-  1 POST-
RE-ADVERTISED
7.1.1
DUTIES AND RESPONSIBILITIES
·         Design graphics for promo, commercials and various programmes,
·         Edit video and audio materials for programmes,
·         Setting up and maintains servers, workstations and peripherals,
·         Providing IT support services to users,
·         Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor.
7.1.2
QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
·
Diploma  in  IT,  Fine  Art  and  specialised  training  in  Graphic  Design,  Computer
Engineering  or  its  equivalent  from  a  recognized  Institution  with  3  years  relevant
working experience in a reputable organization.
7.1.3
REMUNERATION
Attractive remuneration package in accordance with the Institution’s salary scale PGSS 7.


Ref. Na EA.7/96/01/D/29                                                                  
 
SOUNDMAN - 1 POST- RE-ADVERTISED
7.2.1      DUTIES AND RESPONSIBILITIES
·         Recording sound and music on location and in the studio with optimum sound quality and effects,
·         Deal with all sound transfers as may be requested by the producer,
·         Perform integration of music into the broadcast,
·         Ensure proper maintenance and operation of all sound recording devices,
·         Ensure optimum quality of sound at recording/dubbing sessions and proper blending of sound effects with music tracks into single cohesive unit,
·         Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor.
7.2.2      QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
·         Diploma in Sound Recording or its equivalent from a recognised Institution with good command of Swahili and English language.
·         Computer skills are essential.
7.2.3      REMUNERATION
Attractive remuneration package in accordance with the Institution’s salary scale PGSS 5.



Ref. Na EA.7/96/01/D/29                                                                  
MARKETING OFFICER II:  1 POST
7.3.1      DUTIES AND RESPONSIBILITIES
· Seeking for advertising revenue,
· Marketing TBC airtime for Radio and TV · Promote sponsorship of programmes
· Provide marketing information for TBC services
· Perform any other related duties as may be assigned by the supervisor.
  
7.3.2      QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
Hold of Bachelor Degree in Commerce or Advanced Diploma in Business Administration, Marketing, Economics/Economic Planning or its equivalent from a recognized Institution. Computer Skills are essential.
 7.3.3   REMUNERATION
Attractive remuneration package in accordance with the Institution’s salary scale PGSS 10


Ref. Na EA.7/96/01/D/29                                       
NB: GENERAL CONDITIONS
i.        All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 45 years old, however, should also observe the age limit for each position where indicated.
ii.       Applicants must attach an up-to-date current Curriculum Vitae (CV) having reliable contact postal address, e-mail address and telephone numbers.
iii.      Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv.      The title of the position and institution applied for should be written in the subject of the application letter and marked on the envelope; short of which will make the application invalid.
v.       Applicants must attach their detailed relevant certified copies of Academic certificates:
-       Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
-       Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma transcripts.
-       Form IV and Form VI National Examination Certificates.
-       Computer Certificate
-       Professional certificates from respective boards
-       One recent passport size picture and birth certificate.
vi.      FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS ARE STRICTLY NOT ACCEPTED
1

vii.    Testimonials, Partial transcripts and results slips will not be accepted.
viii.   Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action
ix.     Applicants for senior positions currently employed in the public service should route their application letters through their respective employers.
x.      Applicants for entry levels currently employed in the Public Service should
not apply, they have to adhere to Government Circular Na. CAC. 45/257/01/D/140 dated 30th November 2010.
xi.     Applicants who have/were retired from the Public Service for whatever reason should not apply.
xii.    Applicants should indicate three reputable referees with their reliable contacts.
xiii.   Certificates from foreign Universities should be verified by Tanzania Commission for Universities (TCU)
xiv.   Dead line for application is 02nd May, 2013 at 3:30 p.m
xv.    Applicants with special needs/case (disability) are supposed to indicate
xvi.   Women are highly encouraged to apply
xvii.  Only short listed candidates will be informed on a date for interview
xviii.   Application letters should be written in Swahili or English
xix.   APPLICATION LETTERS SHOULD BE POSTED TO THE FOLLOWING ADDRESS. HAND DELIVERY IS NOT ACCEPTABLE:
Secretary
OR
Katibu
Public Service Recruitment
Sekretarieti
ya
Ajira
katika
Secretariat,
Utumishi wa Umma
P. O. Box 63100
S. L. P 63100,
DAR ES SALAAM.
DAR ES SALAAM.
























LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...