Monday, July 28, 2014

Ukrain kujibu mapigo

Wanajeshi wa Ukrain
Jeshi la Ukrain limeanza kujihami mashariki mwa nchi hiyo dhidi ya mashambulizi ya waasi wa Urusi kufuatia kutunguliwa kwa ndege ya Malaysia katika eneo hilo.
Msemaji wa serikali ya Ukrain Andriy Lysenko amesema jeshi la nchi hiyo lilidhamiria kulifunga eneo hilo ili kupisha uchunguzi wa watalaamu kuhusiana na chanzo cha kuanguka kwa ndege hiyo.
Ndege ya Malaysia iliyokuwa imebeba watu 300 iliangushwa katika eneo hilo lililo chini ya udhibiti wa waasi.
Waangalizi wa kimataifa wanasema mapigano hayo yataadhiri uchunguzi wa ajali hiyo ya ndege, mapigano makali yameripotiwa katika amaeneo yanayozunguka mji wa Horlivka na Shakhtarsk.

SOURCE : BBC

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...