Tuesday, March 25, 2014

SERIKALI YAVUNJA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA.

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

TANGAZO LA SERIKALI KUHUSU KUVUNJWA KWA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA

Mhe. Rais aliunda Tume ya Mabadiliko ya Katika kwa mujibu wa kifungu cha 5 na 6 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 kwa Tangazo la Serikali Na.110 la Mwaka 2012. Tume ilikusanya maoni na kuandaa Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo imewasilishwa kwenye Bunge Maalum. Kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 3, Rais amepewa mamlaka ya kuvunja Tume ya Mabadiliko ya Katiba baada ya Rasimu ya Katiba kuwasilishwa Bungeni.

Mnamo tarehe 18 Machi, 2014 Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba aliwasilisha Rasimu ya Katiba kwenye Bunge Maalum. Kutokana na hatua hiyo, na kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Rais wa Jamhuri ya Muungano alivunja rasmi Tume ya Mabadiliko ya Katiba tarehe 19 Machi,2014 kwa Tangazo la Serikali Na.81 la tarehe 21 Machi, 2014.

Hivyo kwa Tangazo hilo, shughuli zote za Tume ya Mabadiliko ya Katiba zimemalizika rasmi tarehe 19 Machi, 2014.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, 
Ikulu, Dar es Salaam.

25 Machi,2014

Monday, March 24, 2014

MVUA ZALETA MAAFA BUKOBA.

L
Usiku wa kuamkia leo mji wa Bukoba umepata mvua ya kutosha iliyosababisha migomba na mazao mengine kuharibika vibaya sana. Hali hii imesababisha hata na baadhi ya makazi kuhezuliwa. Camera yetu imetembelea kata ya Bakoba katika mitaa ya Bunena na kujionea hali ilivyo baada ya kuanguka migomba na wananchi wakiendelea kukata baadhi iliyoangukia mazao mengine na baadhi ya maeneo ya Kashenye.


ORODHA YA WATUMISHI WA AFYA WATAKAOFANYA MITIHANI YA KUJIENDELEZA – MWAKA 2014

BOFYA HAPA.

TANGAZO LA KAZI UTUMISHI (TANZANIA TEA BOARD) 21 MARCH 2014.

Friday, March 21, 2014

ROBO FAINALI YA UEFA, MAN U vs BAYERN.

QUARTER-FINALS-1/2 AND 8/9 APRIL


BarcelonaBarcelona(ESP)
v
AtléticoAtlético(ESP)

Real MadridReal Madrid(ESP)
v
DortmundDortmund(GER)

ParisParis(FRA)
v
ChelseaChelsea(ENG)

Man. UnitedMan. United(ENG)
v
BayernBayern(GER)

JOB VACANCY MANAGING DIRECTOR - TPDC.

SERIKALI KUFUFUA KIWANDA CHA MATAIRI CHA GENERAL TYRE.

Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Tume ya Mipango wakitazama bidhaa zilizokuwa zikitengenezwa na kiwanda cha matairi cha General Tyre. Serikali ina mpango wa kufufua kiwanda hicho ambacho kilisimama uzalishaji tangu mwaka 2007.
Timu ya wakaguzi wa miradi wa maendeleo wakiangalia mitambo ya kiwanda cha matairi cha General Tyre jijini Arusha

Short Course in Traditional Medicine Development - MUHAS.

Thursday, March 20, 2014

NEEMA KWA WANAMTWARA, UWANJA WA NDEGE KUBORESHWA.

Mmoja wa viongozi wa Timu Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (aliyevaa fulana nyeusi) akihoji uimara wa sehemu ya kutulia ndege wakati walipofanya ziara ya kujionea maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mtwara.
Katika kukabiliana na kasi ya maendeleo ya ukuaji wa uwekezaji katika maeneo ya viwanda vikubwa na biashara za huduma mkoani Mtwara, Serikali imesema kuwa kuna haja ya kuuimarisha Uwanja wa Ndege wa Mtwara ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa watumiaji wa uwanja huo, hasa kufuatia kugundulika kwa gesi mkoani humo,
Hayo yamebainishwa mmoja wa viongozi wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri  wakati ilipofanya ziara kwa ajili ya kujionea maendeleo ya uwanja wa huo.
Bibi Mwanri alisema kuwa Serikali inaendelea kufanya tathmini na mikakati mbalimbali itakayopelekea kuuimarisha uwanja wa ndege wa Mtwara ili kuweza kuhudumia uwekezaji mkubwa unaofanywa na makampuni mbali mbali ya ndani na nje ya nchi mkoani humo. Aliongeza:
“Tathmini ya awali inaonesha kuwa miradi mingi ipo mkoani Mtwara kufuatia kugundulika kwa gesi hivyo kuna haja ya dhati ya kuuimarisha uwanja wa ndege wa Mtwara kwa lengo la kutoa huduma za uhakika wakati huu wa mfumuko wa kiuchumi mkoani Mtwara,” alisema Bibi Mwanri.
Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mtwara, Mhandisi Mugasa Mlondo akitoa maelezo juu uimara na ubora wa uwanja wake wakati Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ilipofanya ziara kwa ajili ya kujionea maendeleo ya uwanja huo.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...