Thursday, September 5, 2013

KATIBU MKUU WA CCM TAIFA KUFANYA ZIARA KATIKA MIKOA YA SHINYANGA,MARA NA SIMIYU.



Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana septemba 10 anatarajiwa kuanza ziara ya kawaida katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara.

Ziara hiyo itaanzia katika mkoa wa Shinyanga septemba 10 mpaka 13 mwaka huu, kwa kutembelea wilaya zote nne za mkoa huo na kufuatiwa na mkoa mpya wa Simiyu kuanzia Septemba 14 mpaka septemba 19 kwa kutembelea wilaya zote tano Kabla ya kuhitimisha ziara hiyo kwa kutembelea wilaya Sita za mkoa wa Mara kuanzia Septemba 20 Mpaka 25 mwaka huu.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa CCM ataambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye.

Kwa mujibu wa Ratiba ya ziara hiyo, Wajumbe hao wa sekretarieti watakagua uhai wa Chama ikiwa ni pamoja na kupokea wanachama wapya sanjari na kuhamasisha wananchi kujituma katika shughuli za uzalishaji ili Kuleta tija katika maisha Yao na ya taifa kwa ujumla.

Aidha watakagua maendeleo ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010/2015 hasa katika miradi ya kimaendeleo Kama vile Ujenzi wa majosho kwa ajili ya wafugaji, maendeleo ya maboresho ya kilimo cha Pamba, uvuvi wenye tija pamoja na maboresho ya sekta za Afya, elimu na miundombinu zikiwemo Barabara.

Katika ziara hiyo Katibu Mkuu  atapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kwa kushauriana na serikali kutafuta namna ya kuzitafutia ufumbuzi.Katibu mkuu pia atafanya mikutano ya ndani, na ya hadhara katika kila wilaya za mikoa hiyo.
 

Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
05/09/2013

ALICHOKISEMA ZITTO KABWE JUU YA WAHAMIAJI HARAMU KUTOKA KIGOMA.

 
Watanzania kutoka mkoa wa Kigoma waliokamatwa jana huko Tegeta wameachiwa baada ya kuingilia kati. Tumepata taarifa kuwa kuna wengine kutoka maeneo ya Kitunda pia walikamatwa jana. Tunaendelea kufuatilia. Tutaweka hapa jina la kila aliyekamatwa, kijiji anachotoka na alikamatwaje.
Tunaunga mkono juhudi zozote za kuzuia wahamiaji haramu. Hata hivyo lazima zoezi hili liendeshwe kwa umakini mkubwa sana. Nchi yetu inapakana na nchi 8. Ni dhahiri kama kila mtu anayetoka mkoa wa pembezoni ni 'suspect' wa uraia, tutagombana sana. Ni vema vitambulisho vya Taifa vitoke haraka kwa watu wa mipakani ili kuondoa hizi 'harassment'

MAONI YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA SHERIA NA KATIBA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, YA MWAKA 2013

(Kanuni ya 86(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2013)
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Huu ni Muswada wa marekebisho ya pili ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za Tanzania. Kama Bunge lako tukufu litakavyokumbuka, Sheria hii ilifanyiwa marekebisho ya kwanza kwa kupitishwa kwa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Na. 2 ya mwaka 2012, mwezi Februari ya mwaka jana. Mabadiliko hayo ya kwanza yalihusu Sehemu ya Tatu na ya Nne ya Sheria hii, na yalilenga vifungu mbali mbali vinavyohusu Tume ya Mabadiliko ya Katiba na utekelezaji wa majukumu yake.
Muswada huu wa sasa unalenga kufanya marekebisho katika Sehemu ya Tano ya Sheria inayohusu ‘Kuitisha Bunge Maalum.’ Sambamba na mapendekezo haya, kuna mapendekezo ya kufanya marekebisho katika Sehemu ya Sita kwa kufuta vifungu vya 32 hadi 36 vya Sheria vinavyohusu utaratibu wa kura ya maoni kwa ajili ya kuhalalisha ‘Katiba Inayopendekezwa.’ Marekebisho haya yamewekwa katika aya ya 57 ya Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni, 2013. Mapendekezo ya Muswada huu ni muhimu lakini yana utata mkubwa.
Mheshimiwa Spika,
Katika kutekeleza majukumu yake ya kuuchambua Muswada huu, Kamati ya Bunge lako tukufu ya Katiba, Sheria na Utawala ilikutana na wadau wengi mbali mbali. Hivyo, kwa mfano, Kamati ilipata maoni ya taasisi za kidini na za kiraia; taasisi za elimu ya juu na za kitaaluma; vyama vya siasa na asasi nyingine. Kwa sababu ambazo Kamati haikuelezwa vizuri na uongozi wa Bunge hili tukufu, mapendekezo ya Kamati kwenda Zanzibar kwa lengo la kukusanya maoni ya wadau wa Zanzibar juu ya Muswada huu muhimu kwa mustakbala wa Jamhuri ya Muungano yalikataliwa.
Kwa maana hiyo, ni muhimu Bunge lako tukufu lifahamu ukweli huu kwamba wadau pekee walioshirikishwa kutoa maoni yao juu ya Muswada ni Watanzania Bara tu. Wazanzibari hawakupatiwa fursa hiyo na hawakushirikishwa kabisa, licha ya Sheria yenyewe kuwa na mambo mengi yanayoihusu Zanzibar. Kwa vile wadau wa Zanzibar walishirikishwa kikamilifu kutoa maoni yao kuhusu Muswada uliopelekea Sheria hii kutungwa mwaka 2011, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inataka kujua ni kwa nini uongozi wa Bunge na wa Serikali umeona si busara na sahihi kuwapatia Wazanzibari fursa ya kutoa maoni yao kuhusu Muswada huu wa kurekebisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inawahusu pia Wazanzibari na nchi yao.
URAIS WA KIFALME KWA MARA NYINGINE TENA!!!!
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imepigia kelele jitihada za serikali hii ya CCM kudhibiti mchakato wa Katiba Mpya kwa kuendeleza kile tulichokiita miaka miwili iliyopita, “... kivuli kirefu cha Urais wa Kifalme katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya.[i] Hapo tulikuwa tunazungumzia mamlaka ya Rais ya uteuzi wa Wajumbe na watendaji wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, na tulisema kwamba mamlaka hayo yalikuwa na lengo moja tu: “kuhakikisha kwamba matokeo ya kazi ya Tume hiyo ni yale tu yanayotakiwa na Rais na Serikali yake na chama chake cha CCM.
Mheshimiwa Spika,
Katika Maoni yetu wakati wa kutungwa kwa Sheria hii mwezi Novemba mwaka 2011, Kambi Rasmi ya Upinzani ilipinga vikali mapendekezo ya kumwezesha Rais kuteua Wajumbe wa Bunge Maalum wasiotokana na Bunge lako tukufu na Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Tulisema yafuatayo kuhusiana na jambo hili: “... wajumbe ... wanaopendekezwa kuteuliwa kwenye Bunge la Katiba kwa mujibu wa ibara ya 20(2)(e) na (4) ya Muswada Mpya sio, na hawawezi kuwa, wawakilishi wa wananchi. Kwanza, hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala taasisi zao kuwawakilisha katika Bunge la Katiba kwa sababu Muswada Mpya unapendekeza wateuliwe na Rais.
Kwa sababu ya upinzani huo, mapendekezo ya kumfanya Rais kuwa mteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum wasiokuwa wabunge na Wawakilishi yaliondolewa katika Muswada huo wa Sheria hii. Badala yake, kifungu cha 22(1)(c) cha Sheria iliyotungwa na Bunge lako tukufu kiliweka wazi kwamba “wajumbe mia moja sitini na sita [watateuliwa] kutoka ...” taasisi zilizotajwa katika kifungu hicho.
Mheshimiwa Spika,
Ni kweli kwamba kifungu cha 22(1)(c) kama kilivyotungwa kilileta giza badala ya mwanga katika suala la uteuzi wa wajumbe hao. Kama tulivyoieleza timu ya wataalamu wa Serikali kufuatia mkutano wetu na Rais Jakaya Kikwete uliofanyika Ikulu tarehe 26 Novemba, 2011: “Toleo la Kiswahili la Sheria linasema kwamba wawakilishi wa makundi mengine ‘watakaoteuliwa kutoka’ kwenye makundi yaliyoorodheshwa. Toleo la Kiingereza linasema wajumbe hao watakuwa ‘drawn from’ (kwa tafsiri ya Kiswahili ‘watachukuliwa kutoka’). Maana za maneno haya hazifanani na wala hayako wazi kuhusu nani ‘atakayewateua’ au ‘kuwachukua’ wajumbe hao kutoka kwenye taasisi zao.[ii]
Kwingineko katika mkutano wetu na Rais Kikwete tulimweleza kwamba: “Wajumbe 166 wengine wanaowakilisha taasisi nje ya Wabunge na Wawakilishi hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala na taasisi zao kwani Sheria haisemi ni nani atakayewateua na/au kuwachagua.” Kwa sababu hiyo, tulipendekeza kwamba “Sheria iweke wazi kwamba wajumbe hawa ‘watateuliwa na’ taasisi zilizotajwa. Hii itaondoa utata juu ya uwakilishi wao na juu ya mamlaka yao ya uteuzi.[iii]


Wednesday, September 4, 2013

14th BIENNIAL CONGRESS OF THE ASSOCIATION FOR HEALTH INFORMATION AND LIBRARIES IN AFRICA (AHILA14).

14th BIENNIAL CONGRESS OF THE ASSOCIATION FOR HEALTH INFORMATION AND LIBRARIES IN AFRICA (AHILA14)

 20th – 24th OCTOBER, 2014
DAR ES SALAAM, TANZANIA
Theme:
ICTs, Access to Health Information and Knowledge: Building Strong Knowledge Societies for Sustainable Development in Africa
Background 
The Association for Health Information and Libraries in Africa (AHILA) is pleased to announce its 14th Biennial Congress scheduled to take place in Dar es Salaam, Tanzania. AHILA was founded in 1984 with the aim of improving provision of up-to-date and relevant health information; encourage professional development of health librarians; promote information resource sharing in Africa and exchange of experiences as well as promoting the development and standardization and exchange of health databases in Africa. The main theme of the 14th AHILA Congress is:ICTs, access to health information and knowledge: building strong knowledge societies for sustainable development in Africa”.
The sub-themes of the Congress are:
  1. ICT’s and health information and knowledge management systems for  sustainable development
    1. Use of ICT to enhance access to health information for gender empowerment and poverty reduction
    2. Qualitative and quantitative studies of knowledge management systems for health
    3. ICTs and evidence based health care practices
    4. ICTs and knowledge management practices for health care services
    5. The design of appropriate ICTs to meet information needs of various stakeholders in health care setting, such as health professionals, patients and health consumers
    6. ICT and indigenous knowledge management
    7. Security, privacy, and risk management through ICT
    8. Mobile health applications and access to health information
    9. Emerging technologies for disseminating health information
    10. Information discovery: portals, databases, gateways
  1. Health information literacy and information behaviour
    1. Health information literacy seeking behavior: theories and models
    2. Research approaches and methodologies for health information literacy, information needs and information seeking behavior
    3. Information seeking, searching, use and sharing in health care context
    4. Information literacy and health libraries
  1. Social media networking and dissemination of health information and knowledge: its contribution to creating knowledge societies
a.       Social media, Web 2.0 and Information Literacy 2.0 approaches for health library and information services
b.      Role of libraries in supporting web2.0-based medical education and learning
c.       Qualitative and quantitative studies of social media for health information
d.      Application of social media/networks applications, interfaces and interactions techniques in library and information centers setting
e.      Developing social media tools/ applications for health professionals, patients and health consumers
f.        Role of libraries in supporting collaborative biomedical research
g.       Ethical & legal issues, confidentiality and privacy in information delivery services
  1. Capacity building of Health Information Professionals: the role of LIS education in Africa
    1. Curriculum development for LIS education
    2. LIS education and innovative teaching techniques and methods
    3. LIS education and e-learning technologies
    4. LIS education, information literacy and ICTs
    5. LIS education and knowledge management
    6. LIS education, networking and collaboration
    7. LIS education continuing education and professional development programmes
    8. LIS job market in Africa: current trends
    9. Information literacy instruction, including curriculum development, instructional design, teaching techniques and methods, and evaluation
    10. Information literacy, online learning, distance learning and lifelong learning
  1. Bringing health information and knowledge to Africa’s rural communities through partnership and community engagement
a.       Access of health information to patients and health consumers: strategies and approaches
b.      Indigenous knowledge management
c.       Innovative rural health information services delivery
d.      Partnership and community engagement approaches for rural information provision
The Congress will incorporate the 2nd HIFA International Conference (Healthcare Information For All, HIFA.org), where delegates will review progress made since the launch of HIFA at AHILA 10 (Mombasa, Kenya, 2006) and ways forward to accelerate progress towards Healthcare Information For All in Africa and worldwide.
Abstract details:
·         Abstract should be in English with a maximum of 500 words.                                                                                          
·         Deadline for submission of abstracts is 1st March 2014
·         All abstracts should be submitted as an attachment and sent to the following:
1. Prof. Frankwell Dulle, Email address:  dullefw2011@gmail.com OR nzengamshe@yahoo.com  
2. Dr. Alfred Sife, Email addresssifesas@gmail.com OR sifesas@yahoo.com   
3. Dr. Edda.T. Lwoga, Email address: tlwoga@gmail.com  
4. Copy to Ms Rehema Chande-Mallya, Secretary Organising Committee: email address: rchandemallya@gmail.com
  http://www.ahila.org

BEI KIKOMO ZA MAFUTA AINA YA PETROLI KUANZIA JUMATANO, TAREHE 4 SEPTEMBA 2013.

Tuesday, September 3, 2013

MILA ZINGINE SI MCHEZO

Clarendon Scholarships for International Students at Oxford University in UK, 2014/15.

The Clarendon Fund offers over 100 full scholarships every year to academically excellent graduate students from all around the world. Clarendon Scholarships are awarded on the basis of academic excellence and potential across all degree-bearing subjects at the graduate level at the University of Oxford. The scholarships cover tuition and college fees as well as a generous grant for living expenses. Application deadline is 13th September 2013.
Study Subject(s): All subjects can be funded by a Clarendon Scholarship. There is no quota by subject or preference for any particular course type.
Course Level:
-
All degree-bearing courses at the graduate level are eligible.
-This encompasses all full-time and part-time Master’s courses (MSt, MSc, BCL/MJur, MBA, MFE, MPhil, BPhil, MSc by Research, MTh, MPP) and all DPhil programmes. A list of all the graduate courses offered by the University of Oxford can be found on the Graduate Course Guide.
Postgraduate Certificate or Diploma courses are not eligible for this scholarship.
Scholarship Provider: The Clarendon Fund, UK
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: -Clarendon Scholarships are awarded on the basis of outstanding academic merit and potential to graduate students from all around the world.
-Candidates applying to start a new graduate course at Oxford are eligible. This includes students who are currently studying for a Master’s degree at Oxford but who will be re-applying for a DPhil (you would be eligible for funding for the DPhil).
-Candidates who already have a place but who deferred entry from a previous year are not eligible to apply (as you can apply for Clarendon in the year that you applied for your place and then, if you are successful, you can apply to defer your funding if you need to defer your place).
-Students who will continue to study for the same degree at Oxford in the next year are not eligible for this scholarship.

VACANCIES - THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA.

Monday, September 2, 2013

SELECTED CANDIDATES FOR DEGREE PROGRAMS 2013 MZUMBE UNIVERSITY.

2014/15 Chevening Scholarships for Postgraduate Students in UK.

Foreign and Commonwealth Office (FCO) and partner organisations offer Chevening scholarships for masters students. The programme provides full or part funding for full-time courses at postgraduate level, normally a one-year Master’s degree in any subject and at any UK university. Chevening scholarships cover tuition fees, a living allowance at a set rate (for one individual), an economy class return airfare to the UK and additional grants to cover essential expenditure. Some Scholarships cover part of the cost of studying in the UK; for example, tuition fees only or allowances only. The application deadline varies from country to country.
Study Subject(s): Scholarships are provided to study any subject at any UK university.
Course Level: The programme provides full or part funding for full-time courses at postgraduate level, normally a one-year Master’s degree at any UK university.
Scholarship Provider: Foreign and Commonwealth Office (FCO) and partner organisations
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: Applicants must:
-Meet the academic requirements for their chosen course(s) of study;
-Have a good standard of written and spoken English, and meet the Chevening Scholarships language requirements as well as the language requirements of their chosen course(s) of study;
-Be a citizen of a Chevening country
-Have a minimum of two years’ work experience;
-Not be employees, relatives of employees, or former employees (who left within the past two years) of Her Majesty’s Government (including British Embassies and High Commissions), a partner (sponsor), a sponsoring UK university, or a staff member of the Association of Commonwealth Universities;
-Not have previously studied in the UK under a UK Government-funded scholarship;
-Not have dual British nationality (unless you are a Citizen of a British Overseas Territory).

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...