Tuesday, April 29, 2014
Monday, April 28, 2014
Thursday, April 17, 2014
JUKWAA LA KATIBA LA LAANI KAULI ZA LUKUVI ALIZOTOA BUNGENI
Mchana huu jukwaa la katiba limetoa tamko kulaani kauli alizotoa Waziri William Lukuvi Jumamosi kuhusu jeshi kuchukua nchi kama serikali 3 zikiridhiwa.
Hata hivo, leo tena Waziri Lukuvi akiongea Mjini Dodoma ameonesha hofu yake juu ya udini. ." Uamsho ni taasisi ya kidini inayotekeleza sera za kisiasa za CUF, latia hofu kuibuka chokochoko za kidini nchini" asema Lukuvi.
Updates: AJALI YA MELI KOREA KUSINI, 179 WAOKOLEWA.
Watu 179 waokolewa mpaka sasa huku karibu watu 300 hawajulikani walipo baada ya meli iliyobeba abiria 470 kuzama jana. Maofisa wasema watu 9 wamepoteza maisha mpaka sasa.
Kwa habari zaidi endelea kutembelea blogu hii.
Wednesday, April 16, 2014
WATU 25 WATHIBITISHWA KUFA KWA MAFURIKO DAR.
Watu 25 wamethibitika kufa mkoani Dar es Salaam kutokana na mvua kubwa zilizonyesha kwa siku tatu mfululizo kuanzia Ijumaa hadi Jumapili wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Sadik Meck Sadik amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo akisema watu wengine 14 wanadaiwa kufa, lakini hawajathibitishwa na polisi.
Taarifa kutoka wilaya ya Temeke imesema watu saba wamethibitishwa kufa kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha.Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaam wenye wilaya tatu, amesema watu 11 wamekufa katika wilaya ya Ilala, huku wengine wawili hawajaonekana mpaka sasa.
Pia kuna taarifa za watu 21 kufariki dunia katika wilaya ya Kinondoni, japo hawajathibitishwa.
Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaam Bwana Sadik amesema miundombinu ya barabara na madaraja imeanza kurejeshwa baada ya kuharibiwa na mafuriko na kusababisha mkoa wa Dar es Salaam kukosa mawasiliano ya ndani na pia kukosa mawasiliano na mikoa jirani.
Chanzo: BBC
Updates: WALIONUSURIKA KATIKA MELI ILIYOZAMA KOREA WASIMULIA.
![]() |
| Meli ya Korea Kusini ikizama |
Watu walionusurika wamekuwa wakielezea hali ilivyokuwa ya kutisha ndani ya meli ya Korea Kusini ilipoanza kusimama kwa kuyumba, akiegemea upande mmoja na haraka kuanza kuzama.
"Kwa kweli kulikuwa na sauti kubwa na meli ghafla ikanza kuegemea upande mmoja," amesema abiria aliyeokolewa, Kim Song-Muk.
Bado haijafahamika kilichosababisha kuzama kwa meli hiyo, ambayo kwa kiasi kikubwa iliwabeba wanafunzi wa shule, lakini watu walionusurika katika ajali hiyo wanatoa maelezo sawa kuhusu tukio hilo la kutisha."watu walikuwa wakihangaika kukimbilia maeneo ya juu ya meli, lakini ilikuwa vigumu kufanya hivyo kutokana na meli kupinduka."
Kikosi cha Walinzi wa Pwani ya Korea Kusini kimesema abiria wapatao mia tatu hawajulikani walipo baada ya meli kupinduka na kuzama.
Watu wawili wamefahamika kupoteza maisha na watu mia moja na sitini na wanne wameokolewa. Kikosi cha wapiga mbizi kwa sasa wanatafuta meli iliyozama. Wengi wa abiria wa meli hiyo ni wanafunzi wa sekondari wakiwa katika safari ya masomo kuelekea kisiwa cha Jeju, nchini Korea Kusini.
Meli hiyo ilikuwa na watu 460.
Chanzo: BBC
NAFASI ZA KAZI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MAGAZETI YA MWANANCHI NA DAILY NEWS.
PERSONAL SECRETARY III - 2 POSITIONS
Qualifications: Holder of Secondary Education Certificate who has attained a Certificate in Secretarial Duties stage III, having a minimum shorthand speed of 100/120 w.p.m and pass in basic computer skills
Apply: Chief Government Chemist,Government Chemist Laboratory Agency
P. O. Box 164,Dar es Salaam
Details: Daily News, 9 April 2014
Deadline: 23 April, 2014
LOAN SUPERVISOR
Qualifications: University degree in Economics, Accounting,
Business Administration
Apply: The Chief Executive Officer,Visionfund Tanzania
P. O. Box 1546,Arusha
Details: Daily News, 9 April 2014
Deadline: 10 May, 2014
BRANCH MANAGER
Qualifications: University degree in Economics, Accounting,
Business Administration
Apply: The Chief Executive Officer,Visionfund Tanzania
P. O. Box 1546,Arusha
Details: Daily News, 9 April 2014
Deadline: 10 May, 2014
MAINTENANCE TECHNICIAN II
Qualifications: Holders of Full
Technician Certificate (FTC) in Electrical Engineering from
recognized institutions
Apply: Director General,
Tanzania Bureau of Standards,
P. O. Box 9524,Dar es Salaam
Details: Mwananchi, 9 April 2014
Deadline: 22 April, 2014
Subscribe to:
Comments (Atom)




