Sunday, April 21, 2013

TETEMEKO KUBWA LAITIKISA CHINA,WATU 150 WAFA

 Shirika la habari la taifa la Uchina linasema kuwa watu 150 wamekufa katika tetemeko kubwa la ardhi ambalo limeporomosha majengo na bara-bara katika jimbo la Sichuan, kusini-magharibi mwa nchi.

Wanajeshi kama 6000 wamepelekwa kwenda kusaidia katika uokozi zaidi ya kilomita 100 kutoka Chengdu, mji mkuu wa jimbo la Sichuan.
Shughuli za uokozi zinatatanishwa na bara-bara zilizovunjika na simu zilizokatika.
Waziri Mkuu, Li Keqiang, aliwasili huko haraka kuongoza shughuli hizo.
Tetemeko lilotokea katika jimbo la Sichuan mwaka wa 2008 liliuwa watu 90,000.

CHANZO:BBC

CHADEMA: WABUNGE WALIOFUKUZWA NI MASHUJAA

 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewasifu wabunge wa chama hicho waliosimamishwa huku akimshambulia Spika wa Bunge, Anne Makinda na Naibu wake, Job Ndugai kuwa wanaliendesha Bunge kiharamia.
Akizungumza jana katika uzinduzi wa M4C ya CCADEMA kwa Kanda ya Kati, Mbowe alisema Spika Makinda amekuwa ni mwongo hata kuidanganya dunia kuwa uamuzi wao ni sahihi jambo ambalo si kweli.
“Spika Makinda ni mwongo, ameidanganya dunia na amekuwa akitumia maneno ya uongo kuhalalisha uharamia uliofanywa na Naibu Spika wa Bunge kwa kuwatoa ndani wabunge watano wa Chadema,”alisema na kuongeza:
“Uhuni kama huu ndugu zangu haukubaliki, tutaendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha tunatetea masilahi ya nchi hii na watu wake. Na hapa natangaza mbele yenu kuwa wabunge walioondolewa ndani ya Bunge ni mashujaa,” alisisitiza Mbowe.
Mbowe ambaye ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, aliwaambia wanachama na mashabiki wa Chadema kuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu ndani ya Bunge na kwamba wanatakiwa kuwa majasiri wakiwa bungeni.
Alisema kwamba wakati wote wamekuwa wakishutumiwa kuwa wanafanya fujo ndani ya Bunge, jambo alilosema siyo kweli bali wao wanasimamia Kanuni za Bunge ambazo zimekuwa zikivunjwa na Spika na Naibu wake kila wanapokuwa ndani ya viti vyao.
Alisisitiza kuwa hawako tayari na kamwe hawatakuwa tayari kutii mamlaka yoyote wanayoamini kuwa inawakandamiza na kuwaondolea haki yao, zaidi ya kupambana.
Kiongozi huyo alinukuu baadhi ya vifungu vya Kanuni za Bunge alivyosema kuwa vingetumika kwa kumaliza tatizo la Lissu, aliyemwelezea kuwa alikuwa sahihi, hata angesimama mara mia moja kwa sababu alikuwa akipinga upuuzi.
Kuhusu Katiba
Akizungumzia masuala ya mchakato wa Katiba Mpya, Mbowe alisema kuwa uamuzi uliotolewa ndani ya Bunge katika hotuba yake ndiyo msimamo wa Chadema, akatahadharisha kuwa ikiwa Serikali haitakubali kufanya marekebisho waliyopendekeza, chama hicho kitajitoa.
“Ule ulikuwa ni msimamo wa Kamati Kuu ya chama chetu na bado tunasisitiza kuwa wasipokuwa makini tutajitoa. Kama noma na iwe noma, hata kama uchaguzi, tutashinda kwa nguvu ya Mungu,” alisema na kushangiliwa na umati wa watu.
Hata hivyo, alionya kuwa kama Serikali itapuuza ushauri wao, itaisoma namba kwa kuwa wanajua kinachotaka kufanywa na tayari wameshajipanga kukabiliana nacho.
Dk Slaa ammwagia sifa Lissu
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama hicho Dk Wilbrod Slaa alimwagia sifa Mbunge wa Singida Mashariki ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu, kuwa yeye na wenzake watano waliondolewa kishujaa na wanatakiwa kusonga mbele zaidi.
 CHANZO:Mtandao wa kijamii wa CHADEMA

WARAKA WA NDUGU GOLDEN CHARLES MARCUS KWA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA



GOLDEN CHARLES MARCUS
WARAKA WANGU KWA SERIKALI, TUME YA MABADILIKO YA KATIBA NA WANANCHI KWA UJUMLA
(Kwenye Mitandao ya Kijamii:- Gmail, Yahoo, Facebook, YouTube, Amazon, Twitter na AOL)
Mwanzo Kabisa, kabla hata ya kuanza Mchakato wa Kupata Katiba Mpya, Tume ya Mabadiko ya Katiba ilitafuta na kupata na kutumia Kaulimbiu isemayo TOA MAONI, TUPATE KATIBA MPYA, na Dira yake ilikuwa KUFANIKISHA KUPATIKANA KWA KATIBA MPYA huku Dhamira yake ikiwa ni KURATIBU, KUKUSANYA NA KUTHAMINI MAONI YA WANANCHI ILI KUPATA KATIBA MPYA.

Tume hiyo ya Katiba ikaanza Kazi mara moja kwa Ukusanyaji wa Maoni ya makundi mbalimbali mnamo tarehe 7 – 25 January, 2013, baada ya hapo ilichambua Maoni ya Wananchi mnamo 3 Februari – 4 Machi, 2013, Mnamo tarehe 4 Aprili ikaanza Uandishi wa Rasimu ya Katiba ambayoitashia 2 Mei, 2013.
Lakini licha ya Mipango hiyo mizuri ya Tume, kuna baadhi ya vitu vinafanyika / vimefanyika bila mtazamo mkubwa na wakina na wandani zaidi kwa sababu Wananchi ndiyo watoa Maoni na ndiyo wapendekezaji wakubwa katika hatua hizo za Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Tume ilianzisha mchakato wa kuandaa mabaraza bila kufikilia kwa mapana zaidi kuwa, kilichotakiwa kufanyika ni:-
Kutoa tangazo kwa Wananchi ili watume maombi – hili lilifanyika Vizuri
WDC (Baraza la Maendeleo la Kata la Wenyeviti wa Mitaa na Madiwani husika) walitakiwa wachambue maoni na kupitisha watu wenye sifa husika kwenda kuhakikiwa na Wananchi, kisha Wananchi ndiyo watoe maamuzi ya nani atakayekuwa muwakilishi wao au Uteuzi wa moja kwa moja kutoka kwa Wananchi, sasa mambo yakawa kinyumenyume ikaanza kwa Wananchi nao kwakuwa hawajui kinachoendelea Wakateuwa na kuwaamini Watu watakao wawakilisha, baada ya Wananchi kuchagua watu watakao wawakilisha, Baraza hilo la WDC likatengua maamuzi ya Wananchi na kufanya Uchaguzi upya bila Wananchi kujua (Mchuujo), huku Wananchi wakiamini wamemaliza kupeleka Wawakilishi wao!! kwa namna hii unafikili DIRA na DHAMIRA ya TUME YA KATIBA itafikia malengo?
Mbali na hayo, kazi hii ya Uchaguzi au Muundo wa Mabaraza ulikuwa ni wa KITAIFA badala yake umefanyika kwa UDINI, UCHAMA, RUSHWA na UDANGANYIFU MKUBWA, kwa jinsi hiyo imepelekea Wananchi wengi kupoteza Imani na Tume, kwa mfano Kata ninayotoka mimi GOLDEN CHARLES MARCUS Kata ya Kitaji Musoma Mjini hayo yalijionesha wazi wazi na nilijaribu kuomba Muongozo wa Tume kama yanayofanyika ni sahihi kwa kutuma sms kwenye Namba 0715 081508, 0767 081508, 0787 081508, 0774 081508 (namba hizi ni za Tume) bila majibu yoyote.
Katika Kata yangu kuna Mitaa minne yaani Kitaji ‘A’, ‘B’, ‘C’ na ‘D’ pamoja na Madiwani watatu, wakuchaguliwa mmoja, viti maalum wawili, 02/04/2013 ulifanyika Uchaguzi wa Wawakilishi wa Mabaraza katika Ngazi ya Mtaa, kwenye kundi langu nililoomba la kuwakilish Vijana nilichaguliwa na Wananchi kutoka Mtaa wa Kitaji ‘C’ kwa Kura 120 huku aliyenifuatia alikuwa na kura 97, baada ya Uchaguzi huo wa Tarehe 02/04/2013, tulikutana tena kwenye Mchuujo wa Ngazi ya Kata (WDC) 08/04/2013 lakini kulikuwa na mama mmoja ambaye ni Mwl. Wa shule ya Msingi Azimio na anaishi hapo hapo shule ina maana ni 

Mtumishi wa Serikali kadhalika Mme wake ni Trafki (Polisi wa Usalama Barabarani) na si Mkazi wa kudumu wa Kata husika kama Tangazo la Maombi lilivyoahinisha, kwa jinsi ninavyojua kuwa Mtumishi wa Serikali haruhusiwi kuwania nafasi kama hiyo nakama angekuwa mkazi wa kawaida, kwa sehemu anayoishi ilimpasa mama huyu kugombea Kitaji ‘C’ sababu shule anayoishi hiko Kitaji ‘C’, lakini alitumia pesa kwa M/kiti wa Kitaji ‘C’ na Kitaji ‘B’ akafanyiwa mpango na kapita kwa mabavu na ujanja ujanja mwingi na udanganyifu Mkubwa akawa ameshindia Kitaji ‘B’ ambayo kitaratibu shule anayoishi haiku huko ina maana si Mkazi wa ‘B’.
Wakati tunasubiri Kikao hicho cha kutengua maamuzi ya Wananchi cha 08/04/2013 mama huyo na Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata hii kilitangaza Uchama sana na hata kufanya Vikao vya Usiku na Mchana kupanga safu yao waliyoitaka, huku Wagombea kutoka Chama hicho wakifanya Kampeni chafu za Rushwa na Uchama Usiku na Mchana mpaka nikajuta kugombea, nanikajiuliza kama hali ilikuwa hivyo kwanini kazi hii wasingewapa watu wa CCM au Watu ambao wamewaanda kuliko kutangazia UMMA halafu wao wanapanga Orodha ya Majina ya Watu ambao wanawataka na kweli inakuwa hivyo huku Wananchi wakiwa wameduwaa kwa Matokeo ya Mchuujo.

Kwa Upande wangu nilishangaa sana na kwa hatua hiyo Wananchi walio wengi itakuwa ngumu kwao kuamini Kaulimbiu, Dira na Dhamira ya Tume, Hivyo kwa Waraka huu Tume iangalie chakufanya mapema, kama kubatilisha Uchaguzi huu, ama vinginevyo kwa kadri ya Maamuzi ya Wananchi wengi, waliopiga kura na kubatilishwa na Wachache (WDC) kwa manufaa yao, itakuwa Ngumu kwa Wananchi, hii imeonekana wazi kuwa, ni namna gani Uongozi mdogo wa Chini unavyochonganisha Wananchi na Viongozi wa Juu wa Taifa kama Mchezo huu utakuwa hahukusukwa toka juu, kwa Uchaguzi huu wa wawakilishi wa Mabaraza katika Kata yangu ya Kitaji – Musoma, hauko mbali na Matokeo ya Kidato cha Nne, yaani waliofanya Mahojiano yaani kujieleza mbele ya Baraza (WDC)  hawakuchaguliwa (wamefeli) lakini ambao hawakuwepo na walikuwa wameshatengeza Mazingira Mazuri (Kampeni + Rushwa + Uchama) na hawakujieleza, wameshinda!!!!   
 hii nini au Hili ni Taifa gani tunaloliandaa?.
MWISHO:
Wananchi ndiyo watumiaji wa Katiba na ndiyo wenye maamuzi makubwa, Waheshimiwe na kusikilizwa katika maamuzi yao.
GOLDEN CHARLES MARCUS
Mteule wa Wananchi – Kitaji ‘C’
0767 328202 / 0784 328202 / 0777 328202 / 0658 284625
(Kijana Mwenye Uchungu na Taifa

CHANZO,Mtandao wa kijamii wa CHADEMA

Saturday, April 20, 2013

JOB VACANCIES - JoKUCo (UNIVERSITY)

           

        JOSIAH KIBIRA UNIVERSITY COLLEGE OF TUMAINI
                              UNIVERSITY MAKUMIRA
                    P.O.BOX 1023 BUKOBA, TANZANIA
              TEL.+255732983642;+255732983643; FAX +255732983644
                       Email: jokuco@jokuco.ac.tz; website:www.jokuco.ac.tz
                                                                                                                                    18.03.2013

THE JOSIAH KIBIRA UNIVERSITY COLLEGE (JoKUCo) OF TUMAINI UNIVERSITY
MAKUMIRA (TUMA) INVITES APPLICATIONS FOR LECTURERS WHO CAN TEACH
HISTORY, GEOGRAPHY, ENGLISH, KISWAHILI, FRENCH, EDUCATION, INFORMATION
AND COMPUTER TECHNOLOGY, BUSINESS ADMINISTRATION, PHYSICS, CHEMISTRY,
BIOLOGY AND MATHEMATICS.

APPLICANTS SHOULD HAVE MASTERS DEGREE WITH A MINIMUM PASS OF B+ (GPA
OF 3.5) OR Ph.D. APPLICATIONS SHOULD BE SENT TO THE PROVOST, JOSIAH KIBIRA
UNIVERSITY COLLEGE, P.O.BOX 1023, BUKOBA AND THROUGH THE EMAIL ADDRESS:
jokuco@jokuco.ac.tz THE DEADLINE IS 31ST OF MAY, 2013.
By DEPUTY PROVOST FOR ACADMIC AFFAIRS
FOR PROVOST

AZAM YABANWA MBAVU NYUMBANI NA RABAT

 AZAM FC imelazimishwa sare ya bila kufungana jioni hii na AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu, Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yanaifanya Azam iwe na mtihani mgumu katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo Morocco, wakitakiwa lazima kushinda au kutoa sare ya mabao ili kufuzu.



Pamoja na sare hiyo, Azam watakumbuka sana mabao matatu ya wazi waliyokosa kupitia kwa washambuliaji wao wa pembeni, Kipre Herman Tchetche mawili na Khamis Mcha ‘Vialli’ moja,
Kipre aligongesha mwamba mashuti mawili katika dakika za 51 pembeni kushoto katikati  na dakika ya 90+1 mwamba wa juu katikati baada ya jitihada za kuwatoka mabeki wa AS FAR Rabat.


Khamis Mcha naye alimtoka vizuri beki wa pembeni wa AS FAR Rabat dakika ya 52 lakini akapiga nje shuti lake.


Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Emile Fred wa Shelisheli, aliyesaidiwa na nduguze Steve Maire na Jean Ernesta pembeni, kipindi cha kwanza Azam walionekana kucheza kwa tahadhari zaidi na kufanya mashambulizi machache.


Lakini kipindi cha pili, walifunguka na kuanza kushambulia moja kwa moja jambo ambalo liliweka kwenye misukosuko lango la AS FAR Rabat kwa muda mrefu hadi wachezaji wa timu hiyo kuanza kufanya hila za kupoteza muda ili kupunguza kasi ya wenyeji.


John Raphael Bocco ‘Adebayor’ naye alilitia misukosuko mara kadhaa lango la wageni kila ilipoingizwa mipira ya juu kutokea pembeni hususan kona japokuwa alikuwa chini ya ulinzi mkali leo.


Kikosi cha Azam FC leo kilikuwa
; Mwadini Ally, Himid Mao, Waziri Salum, David Mwantika, Joackins Atudo/Luckson Kakolaki dk7, Kipre Balou, Kipre Tchetche, Salum Abubakar, John Bocco ‘Adebayor’, Humphrey Mieno na Kahmis Mcha ‘Vialli’/Mwaikimba dk78.


AS FAR Rabat; Ali Grouni, Mustafa Mrani, Younes Hammal, Younes Belakhdar, Yassine El Kordy, Abdelrahim Achchakir/Mostafa El yousfi dk74, Salaheddine Said, Mohamed El Bakkali, Salaheddine Aqqal/Souffiane Alloudi dk80, Mustafa Allaoui na Hicham El Fathi/Youssef Anouar dk69.

MBOWE - SPIKA ANAENDESHA BUNGE KIDIKTETA

KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amesema kuwa Spika wa Bunge, Anne Makinda analiendesha Bunge kidikteta.
Alisema vurugu na ghasia zinazotokea bungeni wakati wa mijadala mbalimbali zinatokana na spika na naibu wake Job Ndugai kutaka kuliendesha Bunge kidikteta kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai alitoa kauli hiyo jana kupinga uamuzi wa spika wa kuridhia adhabu iliyotolewa na Ndugai dhidi ya wabunge sita wa CHADEMA.
Wabunge hao ambao walitolewa bungeni na kuzuiliwa kuhudhuria Bunge kwa siku tano ni Tundu Lissu (Singida Mashariki), Godbless Lema (Arusha Mjini), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiel Wenje (Nyamagana) na Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini).
Awali akisoma uamuzi wake jana bungeni kufuatia mwongozo alioombwa na Mbowe, Spika Makinda alisema uamuzi uliofanywa na naibu wake, Ndugai ni sahihi.
Ndugai aliamuru Lissu atolewe nje kwa kukiuka kanuni ya 60 (12) wakati aking’ang’ania kutoa mwongozo wakati naibu spika akimzuia.
Makinda alisema adhabu hiyo ilitokana na kukaidi agizo la kiti la kumtaka kukaa wakati alipompatia nafasi Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Kiwanga (CHADEMA).
Alisema wabunge wengine watano walipewa adhabu hiyo kwa kosa la kuwazuia wapambe wa Bunge kutekeleza agizo la naibu spika la kutaka kumtoa nje Lissu na kusababisha fujo.
“Waheshimiwa wabunge, kanuni zetu na hasa ya 2 (2) na kanuni ya 5(1) ya kanuni za Bunge imempa mamlaka spika kufanya uamuzi pale ambapo hakuna utaratibu wa kanuni.
“Aidha uamuzi unaofanywa na spika ambao unaruhusu uendeshaji bora wa shughuli za Bunge wa kuleta amani na utulivu bungeni, unaingizwa kwenye kitabu cha maamuzi ili kuongoza mwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa Bunge.
“Kwa kitendo kilichotokea Aprili 17 bungeni, hakiwezi kupuuzwa kwa kuwa ni kitendo dhahiri cha kudhalilisha mamlaka ya spika na kilikuwa kitendo cha utovu wa nidhamu wa hali ya juu. Watanzania wote waliushuhudia na wanalaani kilichokuwa kinaendelea ukumbini,” alisema Makinda.
Alifafanua kuwa mbunge yeyote aliyekuwa anaongoza Bunge wakati huo, angeweza kutoa uamuzi huo.
“Ninatumia kanuni ya 5(1) na kanuni ya 2 (2) ya Bunge inayompa mamlaka spika kufanya maamuzi ambapo jambo ama shughuli yoyote haikuwekewa masharti katika kanuni hizi.
“Uamuzi uliofanywa na mheshimiwa Job Ndugai, naibu spika wa kuwatoa nje Mheshimiwa Tundu Lissu…na kubaki nje kwa kutohudhuria vikao vya Bunge siku tano ni halali,” alisema na kuongeza:
“Na sasa utaingizwa katika kitabu cha maamuzi ya spika, na mbunge yeyote atakayefanya vitendo hivi apewe adhabu hii.”

Kauli ya Mbowe
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa mara baada ya uamuzi wa Spika Makinda, Mbowe alisema kama kiti cha spika hakitakuwa tayari kusimamia haki, wabunge wa CHADEMA hawataacha kusimama kuomba utaratibu wa kuzungumza kupinga hoja za upotoshaji za mawaziri na wabunge wa CCM na uendeshaji mbovu wa Bunge.
Alisema kanuni ya 2(2) na kanuni ya 5(1) ya kanuni za Bunge kweli inampa mamlaka spika kufanya uamuzi pale ambapo hakuna utaratibu wa kanuni.
“Kosa la wabunge wetu adhabu yake iko kwenye kanuni. Kanuni aliyotumia inahusu kwa mfano, wewe mwandishi wa habari umetoka sehemu yako, ukaingia ndani ya ukumbi wa Bunge na kuanza kupigana.
“Hapo hakuna kanuni ya kukuadhibu na ndiyo spika anaweza kutumia hiyo kanuni na kisha kuingiza kwenye kumbukumbu ili iweze kutumika baadaye, lakini sio katika kosa la wabunge wetu,” alisema Mbowe.
Alisema uamuzi wa spika ni wa kitoto kwani amezidi kukoroga kanuni kwa ajili ya kumlinda naibu wake.
“Hatutangazi vita na Bunge, lakini kama Bunge halitakubali kufuata haki, wategemee hali hii kuendelea kujitokeza kwani hatutaogopa kufukuzwa kwa kupigania haki,” alisema.
Alisema Lissu alipata adhabu ya kutolewa nje na kufungiwa vikao vitano kwa sababu alisimama mara nyingi kuomba mwongozo na kutoa ufafanuzi wa hoja za kupotosha.
“Lissu au mbunge mwingine yeyote atasimama hata zaidi ya mara 100 kuomba kuzungumza, na tunafanya hivyo kutokana na wingi wa hoja za hovyo za serikali na wabunge wa CCM, na hakuna kanuni inayozuia kuzungumza mara nyingi, na katika hilo tuko tayari kufukuzwa wote,” alisema.
Mbowe alirejea kauli aliyoitoa juzi wakati akiomba mwongozo kuwa kilichotokea bungeni ni sintofahamu kati ya wabunge na kiti cha spika ambapo katika mambo ya msingi, CHADEMA ilitegemea kifungu cha nne cha kanuni za Bunge, kifungu kidogo cha kwanza kingetumika.
“Kifungu hicho kinasema hivi: ‘Spika anaweza kutaja jina la mbunge kwamba amedharau mamlaka ya spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya Haki na Maadili ya Bunge, ikiwa;
Kwa maneno au vitendo, mbunge huyo anaonesha dharau kwa spika au mbunge huyo atafanya kitendo chochote cha makusudi cha kudharau shughuli ya Bunge au mbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo’.
“Kosa la wabunge wetu linaangukia kwenye kanuni hii kwamba wameonyesha dharau pale walipokaidi kutoka nje. Kanuni iko wazi kwamba spika atapeleka majina ya wabunge hao kwenye Kamati ya Haki na Maadili ya Bunge ambako watapewa nafasi ya kusikilizwa na kutoa ushahidi kabla ya kuhukumiwa,” alisema.
Mbowe alieleza kushangazwa na hukumu hiyo kwani hakuna mbunge wala kiongozi yeyote wa CHADEMA aliyeitwa kusikilizwa, na hata uamuzi wa spika nao haukuzingatia kuwahoji wahusika.
Aliitaka jamii kujiuliza kwanini wabunge hao wanapokutana nje ya Bunge ni marafiki wa karibu, lakini wakiingia ndani ya Bunge vurugu za kurushiana maneno hujitokeza.
“Huwezi kukuta wabunge nje wanagombana kwa sababu wanaheshimiana. Ndani ya Bunge chanzo cha hao wanaopatana nje kurushiana maneno ni kiti cha spika kushindwa kusimamia haki na kanuni,” alisema.
Hatua za kuchukua
Pamoja na Spika Makinda kuridhia adhabu ya Ndugai dhidi ya wabunge wa CHADEMA, Mbowe alisema wanatarajia kukata rufaa kwenye Kamati ya Kanuni kupinga uamuzi wa spika.
Alisema anajua CHADEMA itashindwa katika kesi hiyo, lakini wanataka kuweka rekodi na kumbukumbu kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Alisema Spika Makinda kama ilivyokuwa kwa Ndugai, amekosea kuridhia adhabu hiyo.
Katika hatua nyingine, Mbowe alisema kuwa Bunge limenajisiwa kwa kuruhusu watu wasiotakiwa kikanuni kuingia bungeni kiholela kwa nia ya kutaka kumtoa Lissu.
Akifafanua, alisema kisheria wanaoruhusiwa kuingia bungeni ni wabunge, uongozi wa Bunge na watumishi wao, na kama kuna mtu mwingine anataka kuingia lazima kanuni itenguliwe.
“Ukiacha rais ambaye ni sehemu ya mbunge, mtu yeyote haruhusiwi kuingia bila kutengua kanuni. Juzi Ndugai alivunja kanuni kwa kuruhusu askari kuingia bungeni wakati siwa iko mbele na hadi sasa hakuna taarifa iliyotolewa,” alisema.
Chanzo,Mtandao wa kijamii wa CHADEMA .

Friday, April 19, 2013

TANGAZO KUTOKA KWA DIAMOND JUU YA WATU WANAOTUMIA SOCIAL NETWORK KUFANYA UTAPELI KUPITIA JINA LAKE

Katika mtandao wa kijamii wa Msanii maarufu Diamond,ametoa tangazo linalotaadhalisha wanachi wasije tapeliwa.
Tangazo lenyewe hili hapa:-
 
"Napenda kuwataharifu fans wangu kuwa...kuna tabia imekuwa
 ikijotekeza kwenye social networks.
Tabia hiyo imekuwa ya kitapeli ya kufungua account
mbalimbali kupitia social networks
na kuanza kutuma massage za ajabu.....jambo ambalo
mimi binafsi sipendezwi nalo.....
nimelivumilia lakini nikaona isiwe vibaya nikiwajuza tena
 kuwa mkipata ujumbe wowote
kupitia social network kupitia jina langu kuomba
 msaada mtambue kabisa
si kweli......Jambo lolote kuhusiana na mimi binafsi utapata
 updates zangu kupitia
Account yangu ya facebook by Diamond platnumz ambayo ipo
 connected na tweeter
&Instangram pekee......lakini vinginevyo
sintousika na tuhuma zozote.....

Binafsi nimeshangzwa na ujumbe huu wa mtu ambae anatumia account facebook kwa jina
la Diamond platnum,kwa kuwasambazia ujumbe ufuatao:

KARIBU KTK PARTY YA KIMYA KIMYA YA KUMSHUKURU MAMA YANGU MPENDWA MAMA NASEEB.
KADI YA MWALIKO INAPATIKANA ATRIUM HOTEL BAADA YA KUTOA MCHANGO WAKO
ITAFANYIKA KTK MJENGO WANGU MPYA WA KISASA ULIOPO TEGETA NEXT WEEK.
THIS PARTY IS 4 ONLY INVITED PEOPLE..COZ IS SUPRIZING CELEBRATION PARTY
KADI ZINATOLEWA KUANZIA SAA 10JIONI HADI SAA3 USIKU MARA BAADA YA KUPOKELEWA MCHANGO WAKO.
MCHANGO NI KIASI CHOCHOTE NA UTUMWE KTK NAMBA YANGU YA TIGO.
KARIBU..
078889889 hy ndo namba yake
NB: MARA UTUMAPO MCHANGO WAKO UTAPOKEA SMS YENYE NENO LA SIRI AMBALO UNATAKIWA KUFIKA NALO KWA MUHUSIKA NA KULITAJA.
NIMEWEKA MCHANGO KUPUNGUZA IDADI YA WATU...
Niliuzunika sana kwa mambo kama haya bado kuendelea kufanyika kwenye social networks......
ni hayo tu my truly fans wa Diamond i hope mmeninyaka wote....... PEACE & LOVE"

FUATILIA UKUSANYAJI WA SAHIHI ZA KUMFUKUZA KAZI NAIBU WAZIRI MULUGO.



 Katika mtandao wa kijamii wa  http://www.frankmakange.com/petitions/ kuna ukusanyaji wa sahihi ili Rais Kikwete aweze kumfukuza kazi Naibu Waziri Phillipo Mulugo

Katika ukusanyaji huo,kuna maneno yafuatayo yanayoenda kwa Mh.Rais Kikwete:-

"Dear President Kikwete,
When you were elected President, Tanzanians expected you to provide good and strong leadership. Unfortunately, so far at least, we have not had the privilege of experiencing responsible and ethical leadership in action.
Mr. President, in the wake of what is unarguably the worst Form Four National Examination Results, I share the urgency that Tanzanians cannot accept an incompetent and information illiterate Philipo Augustino Mulugo as a Deputy Minister of an office expected to adhere to the highest standards of academic integrity.
Sir, holding onto a man who has turned out to be a public embarrassment and a national disgrace, confirms that your administration just wants to soothe public opinion and continue with business as usual.
Will you surprise us this time around? Mr. President, somewhere I read, “Hope is what makes us look foward to each and every day; without hope there is no tomorrow.” It is with this hope that I believe you are going to show leadership and sack Mulugo. Sack him! Mr. President, please do the right thing and sack Philipo Augustino Mulugo! It is not hard to see why unless you too think that, “…Tanzania was formed in one nineteen sixty four (11964) by unifying the Indian Ocean Islands of Zimbabwe and Pemba and the mainland country formerly known as Tanganyika.”
Sincerely,
[signature]"

LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KUANZA MEI 12,2013

 Ligi ya Mabingwa wa Mikoa kutafuta timu tatu zitakazopanda kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao chini ya usimamizi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itaanza Mei 12 mwaka huu.

Mwisho wa mikoa kuwasilisha majina ya mabingwa wao ni Mei 1 mwaka huu wakati ratiba ya ligi hiyo itapangwa mbele ya waandishi wa habari Mei 3 mwaka huu kwenye ofisi za TFF.

Uwasilishaji wa jina la bingwa wa mkoa unatakiwa kufanyika pamoja na ulipaji ada ya ushiriki ambayo ni sh. 100,000. Mfumo wa ligi hiyo ni bingwa wa mkoa X kucheza na bingwa wa mkoa Y nyumbani na ugenini ambapo mshindi ndiye anayesonga mbele katika hatua inayofuata.

Usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika katika hatua ya mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho. TFF inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi hiyo.

NANI KUWA MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA ENGLAND KATI YA VAN PERSIE, BALE, SUAREZ, CARRICK, HAZARD NA MATA ???

Leo imetangazwa rasmi orodha ya wachezaji ambao wanagombania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa ligi kuu ya Uingereza - Man United imetoa wachezaji wawili, kiungo Micheal Carrick  na Robin Van Persie, Luis Suarez anaiwakilisha Liverpool, Gareth Bale, Juan Mata na Eden Hazard wakiliwakilisha jiji la london. Mabingwa watetezi Manchester City hawajatoa mchezaji hata mmoja katika listi hiyo iliyotangazwa leo.

Orodha yenyewe ni:-
Michael Carrick (Manchester United)
Gareth Bale (Tottenham Hotspur)
Robin van Persie (Manchester United)
Luis Suarez (Liverpool)
Eden Hazard (Chelsea)
Juan Mata (Chelsea)


Washindi wa miaka iliyopita

2011-12: Robin van Persie (Arsenal)
2010-11: Gareth Bale (Tottenham)
2009-10: Wayne Rooney (Man Utd)
2008-09: Ryan Giggs (Man Utd)
2007-08: C Ronaldo (Man Utd)

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...