Tuesday, September 10, 2013

TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA MADAKTARI, MADAKTARI WA MENO, TABIBU, TABIBU WASAIDIZI NA WATAALAMU WA MAABARA

Norwegian Government Quota Scheme for Eastern European, Developing & Central Asian Countries, 2013/14.

Norwegian Government offers Quota Scheme for Developing Countries’ Students in Norway. The scheme normally includes courses taught in English at Master’s and PhD level, in addition to certain professional degrees at selected Norway Universities. The Quota Scheme will only enrol students from institutions (organisations, universities, authorities) which have collaboration agreements with Norwegian universities or colleges. Norwegian institutions usually do not admit free movers (individual applicants) to this scheme. Only in very special cases will free movers be considered. The deadline for applications for the Quota scheme is usually 1st December every year.
Study Subject (s): Scholarships are provided to learn any of the courses offered by the Selected Norway Universities.
Course Level: The scheme normally includes courses taught in English at Master’s and PhD level, in addition to certain professional degrees at Selected Norway Universities.
Scholarship Provider: Norwegian Government
Scholarship can be taken at: Norway
Eligibility: -The Quota Scheme will only enrol students from institutions (organisations, universities, authorities) which have collaboration agreements with Norwegian universities or university colleges. Norwegian institutions usually do not admit free movers (individual applicants) to this scheme. Only in very special cases will free movers be considered. Please contact the institutions directly for individual information.
-Students who come to Norway as self-financing students will, as a rule, not be considered as being qualified for the Quota Scheme.
-Students usually apply for degree programmes that serve as a continuation of their studies in their home country or for courses which can be a joint part of a degree programme in their home country (joint degree or sandwich programmes). Most of the programmes offered are at Master’s or PhD level, but the Quota Scheme also offers certain Bachelor’s study programmes.

Monday, September 9, 2013

SHEIKH AKAMATWA KWA KUBAKA MOROGORO.

Sheikh wa Msikiti wa MasjidMaftah Mjini Morogoro amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka nane (8) nyumbani kwake.
Habari zaidi tutazidi kuwaletea kadiri tutakavyokuwa tunazipata.

TANGAZO LA SKOLASHIPU ZILIZOTOLEWA NA SERIKALI YA SRI LANKA KWA TANZANIA KWA MWAKA 2013/2014.

Serikali ya Tanzania imepokea mwaliko wa Skolashipu kutoka kwa Serikali ya Sri-Lanka kwa mwaka 2013/2014.

Wadau wote, raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wenye sifa wanashauriwa wasome mwongozo na fomu za maombi kwenye Kiambatisho cha tangazo hili na kuyafanyia kazi.

Maombi yaliyokamilika yakiwa na nyaraka zote zilizoorodheshwa kwenye Kiambatisho yawasilishwe Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kabla ya tarehe 15/09/2013 kwa anuani ifuatayo:-

Katibu Mkuu,
Wizara Ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
S. L. P 9121,
DAR ES SALAAM

JOB ADVERTISEMENT - POSTAL BANK SEPTEMBER 2013.

Rais JK aonja nguvu ya CHADEMA Mwanza.

ISHARA YA VIDOLE VIWILI, PEOPLES POWER VYATAWALA
RAIS Jakaya Kikwete jana alipata wakati mgumu, baada ya kukutana na nguvu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jijini Mwanza katika ziara yake, huku Waziri wake wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, naye akijikuta akizomewa mbele yake.
Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje, alivunja mwiko baada ya kujiunga katika msafara huo wa raia akiwa na gari lenye alama za Movement for Change (M4C) lililokuwa limefungwa bendera mbili za CHADEMA.
Hata hivyo maofisa usalama walipata wakati mgumu kulizuia gari hilo lisiwepo katika msafara huo, jambo lililozua tafrani kidogo katika uwanja wa Furahisha ambapo Kikwete alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara.
Awali wakati wa uzinduzi wa wodi ya wazazi iliyoko eneo la Butimba, Rais alilazimika kumpa Wenje nafasi ya kuwasalimia wananchi baada ya Mkuu wa Mkoa, Evarist Ndikilo, kutaka kufanya hila ya kumnyima haki hiyo kama mbunge wa jimbo husika.
Baada ya viongozi wote kutambulishwa bila Wenje kutajwa, wananchi walianza kupaza sauti wakitaka mbunge wao naye atambulishwe.
Wenje baada ya kusimama alimshukuru Rais Kikwete kwa kumpa nafasi hiyo lakini akamwomba amvumilie kidogo atoe salamu maalumu ya wana Mwanza.
Kama kawaida ya CHADEMA kwenye salamu yao, Wenje aliwaomba wananchi wakunje ngumi kisha akawasalimu kwa kibwagizo cha peoples… nao wakamwitikia power!
Akiwa katika viwanja vya Furahisha ambapo Rais Kikwete alichelewa kuanza mkutano wake, Wenje alifika hapo na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi huku polisi wakiwazuia bila mafanikio.
Ilipofika saa 12 jioni kabla Rais hajaingia uwanjani, wananchi hao walimtaka Wenje awahutubie huku wakidai bendera ya taifa ishushwe kwani muda wake ulikuwa umefika.
Kikwete aliingia uwanjani hapo saa 12:10 akiongozana na viongozi mbalimbali wa chama na serikali lakini wananchi hawakuonyesha kumshangilia badala yake walikuwa wakimwonyesha alama ya vidole viwili inayotumiwa na CHADEMA wakiimba ‘peoples…power’.
Katika hatua ya kushangaza wananchi hao walimshangilia kwa nguvu mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia, aliyekuwa ameongozana na Rais huku wakiwazomea Meya wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, ambaye hakufika kabisa mkutanoni hapo.
Matata alionekana mapema wakati Rais Kikwete akisomewa taarifa ya maendeleo makao makuu ya wilaya hiyo lakini hakufika uwanjani kabisa katika viti vya mbele alionekana naibu wake, Swila Dede.
Baadhi ya wananchi hao walisikika wakisema chini kwa chini kuwa Matata ni mwizi hawataki kumsikia lakini shangwe na nderemo zikajiri pale walipotambulishwa Wenje na Kiwia.
Rais Kikwete akiwa wilaya ya Ilemela, wananchi wengi waliokuwa wamesimama njiani walimwonyesha vidole viwili ikiwa ni alama CHADEMA.
Hata hivyo, hali hiyo ilionekana kumkera kiongozi huyo wa nchi pamoja na maofisa wa usalama, ambapo wana usalama wakiwemo polisi walionekana wakiwatisha na kuwazuia wananchi kunyoosha vidole viwili.
Magufuli azomewa
Waziri wa Ujenzi, Dk. Magufuli, alikumbana na jinamizi la kuzomewa mbele ya Rais baada ya kusimama jukwaani na kutaja jina la Matata, ambapo wananchi wengi walimzomea kwa miluzi huku wakimnyooshea vidole viwili.
Adha Magufuli alizomewa pia aliposema wabunge wa Ilemela na Nyamagana jijini hapa ni wana CHADEMA lakini ndani ya roho zao ni wana CCM.
Pia aliendelea kuzomewa aliposema kuwa iwapo Rais angehitaji kupokea kadi za CHADEMA zilizorudishwa angepokea nyingi.
“Mheshimiwa Rais, nampongeza Meya Matata (akazomewa), lakini pia wabunge wa Ilemela na Nyamagana wanachapa kazi vizuri, nje CHADEMA lakini ndani wao CCM (akazomewa).”
Akizungumza katika mkutano huo, Rais Kikwete alimpongeza mbunge wa Nyamagana kwa uchapakazi mzuri hasa kusimamia sekta ya elimu na kwamba wabunge wa namna hiyo wanastahili kuigwa.
Hata hivyo, alisema serikali yake imejipanga vizuri kuhakikisha usafiri wa reli, ndege, majini na barabara za lami vinaboreshwa maradufu kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
“Serikali yangu imeweka nguvu kubwa katika kuboresha sekta ya uchukuzi, ujenzi na nyinginezo. Hii ni kutaka kuwaletea wananchi wetu maendeleo ya kisekta,” alisema.
Baadhi ya mawaziri walioongozana na Rais mbali na Magufuli ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Kitwanga, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, Naibu Waziri wa Ujenzi na Dk. Charles Tizeba.

CANDIDATES TO BE SPONSORED BY MINISTRY OF HEALTH 2013/2014.

Friday, September 6, 2013

2014 Commonwealth Scholarships for Developing Commonwealth Countries’ Students in UK.

UK Department for International Development (DFID) offers Commonwealth Scholarships for developing countries’ students for pursuing Master’s, PhD and split-site (PhD) degree level at UK Universities. Approximately 300 scholarships are awarded each year. The CSC invites around three times more nominations than scholarships available – therefore, nominated candidates are not guaranteed to get a scholarship. There are no quotas for scholarships for any individual country. The application deadline for these Commonwealth Scholarships is 3rd December 2013.
Study Subject(s): Scholarships are provided in all subject areas offered at UK universities, although the CSC’s selection criteria give priority to applications that demonstrate strong relevance to development.
Course Level: Scholarships are available for pursuing Master’s, PhD, and split-site (PhD) degree level at UK Universities.
Scholarship Provider: UK Department for International Development (DFID)
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: To apply for the awards covered in this prospectus, candidates should:
-Be Commonwealth citizens, refugees, or British protected persons
-Be permanent resident in a developing Commonwealth country (a full list is available at http://bit.ly/cscuk-developing-cw-countries)
-Be available to commence their academic studies in the United Kingdom by the start of the UK academic year in September/October 2014
-Hold, by October 2014, a first degree of upper second class Honours standard (or above); or a second class degree and a relevant postgraduate qualification, which will normally be a Master’s degree and
-For awards enhance clinical skills in the fields of medicine and dentistry, have qualified as a doctor or dentist between 1 October 2004 and 30 September 2009.
-The Commission wishes to promote equal opportunity, gender equity and cultural exchange. Applications are encouraged from a diverse range of candidates.

HIVI NDIVYO MH.MBOWE ALIVYOONDOLEWA BUNGENI JANA.

UKUMBI wa Bunge leo uligeuka kuwa ulingo wa ngumi baada ya wabunge wa kambi ya upinzani kutunishiana misuri na askari wa bunge hilo ambapo  Kiongozi mkuu wa kambi ya upinzani Freeman Mbowe alipoamliwa kutoka nje na Naibu Spika Job Ndugai.

Hatua hiyo ilitokana  baada ya wabunge hao kupiga kura za kukubali au kukataa kuhusu kupitishwa kwa kujadili Mswaada wa Katiba uliopelekwa Bungeni hapo na Serikali ili kuweza kujadiliwa na bunge hilo.

Wabunge hao wa kambi ya upinzani wakiongozwa na Freeman Mbowe walipinga matokeo hayo na kuamua kusimama na wakati huo huo Spika Ndugai aliwataka kukaa chini ili kuendelea na kuchangia hoja za msingi za kujadili mswaada huo.

Ndugai aliwataka wabunge hao kukubaliana na matokeo yaliyotokea na kwa pamoja waweze kujadili mswaada huo 
ambao ni faida kwa taifa lakini mbali na ombi hilo kambi ya upinzani walikaidi ndipo Spika alitoa dakika tano kwa za kiongozi huyo kutoka ili bunge liendelee,ambapo hata hivyo kiongozi huyo alikaidi amri hiyo.

Baada ya mabishano hayo ndipo Spika alipotumia kiti chake na kuwataka askari wamtoe kwa nguvu nje ya ukumbi wa bunge, amri ambayo ilizua taflani na hekeheka kupelekea wabunge wa kambi ya wapinzani kuungana na kuwatunishia misuri askari hao wakimkingia kiongozi huyo kutolewa nje.

Tukio hilo lililochukua dakika zaidi ya 30 lilipelekea Bw. Job Ndugai kuwatolea macho askari hao akiwaamuru kutumia mabavu ili kuweza kumtoa nje ya ukumbi Bw. Mbowe.

Sakata hilo lilifanikiwa baada ya askari hao kutii amri ya Naibu Spika huo kwa kutumia mabavu kumtoa nje kiongozi wa kambi ya upinzani ambapo aliungwa mkono na wabunge  kutoka nje ya ukumbi na kususia kikao hicho.

Katika tukio hilo Mwenyekiti wa vyama vyenye wabunge wengi bungeni na Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mkoani Kilimanjari Agustino Mrema alisema kuwa kitendo kilichofanywa na wabunge wezake si cha kungwa na na kinaleta fedheha kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Alisema yeye kutokutoka kwake nje haimaanishi kuwa ni kibaraka wa CCM na  si ndicho alichotumwa kufanya na wananchi wake,hivyo haungi mkono hata kidogo na haeleweke hivyo kuhusu msimamo wake.

"Hatoki mtu hapa nitakaa ndani ya bunge mpaka kieleweke na mnielewe kwamba mimi ndiye kiongozi wao vyama vyote tisa,hivyo nastahili kuheshimiwa na sikubaki humu ndani kwa sababu mimi ni kibaraka wa CCM bali  kinachopiganiwa ni maslahi ya taifa na ndicho nilichotumwa na wananchi wangu sikutumwa nije kutoka nje au kususia bunge."alisema Mrema.

Naye, Mbunge wa Same Mashariki na Bi Anne Kilango Malecella aliitaka Serikali kusimama imara na isiogope vitisho vinavyotolewa na wasioitakiwa mema nchi katika kupigania maslahi ya taifa.

Alisema kuwa kitendo kilichofanywa na wapinzani bungeni hakina nia njema katika kupata katiba mpya na wajumbe 156 waliopiga kura wanavigenzo vya kuweza kuchangia Mswaada huo kujadiliwa.

Vurugu za bunge hilo ziliaza toka awali katika kipindi cha muongozo wa Spika ambapo vijembe,kashifa kwa wabunge kuzungumza bila kufuata utaratibu ilimradhimu Naibu Spika Job Ndugai kusimama mara kwa mara kujaribu kurejesha utulivu katika matukio yaliyotawala Ukumbini humo. 





Mara baada ya kutolewa mwongozo ulioombwa na wabunge juzi wakidai Muswada wa Mabadiliko ya rasimu ya katiba umeingizwa vipengele kinyemele, na Zanzibar kutoshirikishwa kikamilifu, wabunge wa kambi rasmi ya upinzani bungeni na wale wa CCM walikuwa wakituhumiana kusema uongo kuhusiana na hatua hiyo ya uandaaji wa mchakato wa Rasimu wa Katiba mpya.



Thursday, September 5, 2013

COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE UNITED KINGDOM FOR THE YEAR 2014.

The Ministry of Education and Vocational Training as a nominating agent in the country for the Commonwealth scholarships is inviting applications from qualified Tanzanians for Masters and Doctorate degrees tenable in the United Kingdom in the year 2014.

The Scholarships include:
·         One year taught masters courses or equivalent degrees.
·         Doctorate degrees, of up to three years duration.

Qualifications
1.    Applicants must be holders of bachelor or masters degrees;
2.    Applicants for masters must have bachelor degrees of GPA not less than 3.5; and
3.    Applicants for Doctorate degrees must have a B Grade Masters degrees or a GPA of 4.0 or above at Masters level.

Mode of Application:
·        All applications should be made directly to the Commonwealth Secretariat and should be online using the following link: http://bit.ly/cscuk-apply
·         It is important that applicants should read and understand all given instructions when filling the application forms, and should attach all necessary attachment such as certified copies of academic certificates, transcripts, birth certificates and submit online through the above mentioned link.

All applicants who wish to be nominated by the Ministry of Education and Vocational Training, should print one hard copy of completely filled application form, attach with certified photocopies of academic certificates, transcripts, and birth certificates and submit them to the address below before 15th October, 2013.


The Permanent Secretary,
Ministry of Education and Vocational Training,
P. O. Box 9121,
DAR ES SALAAM

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...