Monday, June 24, 2013

TANGAZO KWA WALIOPANGIWA VITUO VYA KAZI - WIZARA YA AFYA.

MWENYEKITI UVCCM TAIFA: SIAFIKI MFUMO WA SERIKALI TATU.


MWENYEKITI wa Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Taifa (UVCCM), Sadifa Juma Hamisi, amepinga vikali kuwepo kwa mfumo wa serikali tatu kama inavyopendekezwa katika rasimu ya katiba.

Sadifa ameyasema hayo wakati akizungumza na wanachama wasomi wa UVCCM kutoka katika vyuo vikuu mkoani kilimanjaro katika hafla ya kuwaaga wasomi hao na ambapo pia ametunuku vyeti vya uanachama kwa wanafunzi 312 pamoja na kuwakabidhi kadi za uanachama wanachama wapya.



Scholarships at Plymouth University in UK 2013/2014.

Plymouth University is offering international student merit scholarships for all postgraduate taught programmes. International Students can apply for these scholarships. Students must have 1st class Bachelor’s degree in a relevant subject. Applicants should hold a conditional or unconditional offer for a postgraduate taught programme at the Plymouth University for September 2013 entry. The applicant should be a self funded student and not in receipt of an official Government, company or any other scholarship. The application deadline is 30th June 2013
Study Subject (s): Scholarships are offered for all postgraduate taught programmes offered by the university.
Course Level: Scholarships are available for pursuing postgraduate degree level at Plymouth University.
Scholarship Provider: Plymouth University, UK
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: Applicant must meet the following eligibility criteria:

Friday, June 21, 2013

HIVI NDIVYO VIBONZO VYANGU VYA WIKI.





MAFURIKO YAUA WATU ZAIDI YA 300 INDIA.

Makundi ya waokoaji yanaendelea kuwatafuta walionusurika katika mafuriko yaliotokea katika jimbo la Uttarakhand nchini India leo, huku maafisa wakisema karibu watu 300 wamekufa.
Taarifa zinasema zaidi ya watu 13,800 wamepotea na wengine 62,800 wangali wamenasa katika maeneo hayo  karibu na miji ya shughuli za  hija za  waumini wa kihindu ya  Badrinath na Kedarth.
Picha za televisheni zimeonyesha watu wakipanda mabonde, huku wakisaidiwa na wanajseshi. Hadi sasa karibu watu 56,000 wameokolewa.

Source: DW

DAVID LUHENDE AONGEZWA KATIKA KIKOSI CHA TAIFA STARS.


  NAME  DAVID LUHENDE
NATIONALITY  TANZANIA
DATE OF BIRTH  21 JANUARY 1989
HEIGHT  5’5’ INCHES
WEIGHT  63KGs
POSITION  DEFENDER
JERSEY  29
PREVIOUS CLUB  Kagera Sugar FC

Beki wa Yanga, David Luhende ameongezwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kwa ajili ya mechi dhidi ya Uganda (The Cranes) kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Kocha Kim Poulsen amesema kutokana na uamuzi huo wa kumuongeza beki huyo wa kushoto amemuondoa mchezaji mmoja kwenye kikosi chake. Mchezaji huyo ni mshambuliaji Zahoro Pazi wa JKT Ruvu.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager sasa itaingia kambini kwenye hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam, Julai 3 mwaka huu badala ya Julai 4 mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa awali.

Mechi ya Uganda itachezwa Julai 13 mwaka huu, saa 9 kamili alasiri kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati ile ya marudiano itachezwa wiki mbili baadaye jijini Kampala, Uganda.

Wachezaji wanaotakiwa kambini ni Aggrey Morris (Azam), Aishi Manula (Azam), Ally Mustafa (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruni Chanongo (Simba), John Bocco (Azam), Juma Kaseja (Simba), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar) na Kelvin Yondani (Yanga).

Wengine ni Khamis Mcha (Azam), Mrisho Ngasa (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), Mwadini Ali (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Nadir Haroub (Yanga), Salum Abubakar (Azam), Shomari Kapombe (Simba), Simon Msuva (Yanga) na Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar). 


BUSH NA MKEWE KUJA NCHINI MWEZI UJAO.

Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush na mkewe, Laura, wanatarajiwa kuwasili nchini mwezi ujao ambapo watahutubia kongamano litakalojadili wajibu wa wake za marais katika kuinua wanawake duniani.
Taasisi ya George Bush  ndiyo imeandaa kongamano  hilo litakalofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 2 hadi 3.
Taarifa iliyotolewa jana na taasisi hiyo kwa vyombo vya habari, ilisema kongamano hilo, litahudhuriwa pia na mke wa Rais Barack Obama wa Marekani, Michelle na  muasisi wa Taasisi ya Wanawake ya Cherie, Cherie Blair ambaye ni mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair.
Wake wengine wa marais wa Afrika watakaohudhuria ni Mama Salma Kikwete, Chantal Campaore wa Burkina Faso, Roman Tesfaye wa Ethiopia, Maria da Luz Dai Guebuza (Msumbiji),  Penehupifo Pohamba (Namibia), Sia Nyama Koroma (Sierra Leone), Janet Museveni (Uganda) na Christine Kaseba wa Zambia.
Kongamano hilo litajikita zaidi katika kujadili masuala ya kuwekeza kwa wake, kuimarisha Afrika lakini pia wajibu wa wake za marais  kuhamasisha wanawake katika maeneo ya elimu, afya na kuwakwamua kiuchumi.
“Kongamano hili litakutanisha pamoja wake za marais, maofisa wa Serikali, mashirika binafsi, Asasi Zisizo za Serikali (AZISE) na wasomi kujadili mambo muhimu ya kuchukuliwa hatua ili kunufaisha wanawake,” ilisema taarifa hiyo.
Aidha, mada zitakazowasilishwa na kujadiliwa katika kongamano hilo ni kuinua wajasiriamali wanawake kiuchumi kupitia mafunzo na teknolojia, kupatia fursa wanawake wakulima kwa kupewa mafunzo ya kilimo cha kisasa, mafunzo kuhusu saratani ya matiti na umuhimu wa elimu kwa wanawake.
Kongamano hilo linafanyika sambamba na ujio wa Rais Obama anayetarajiwa kuwasili nchini mwanzoni mwa mwezi ujao.
Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika ambazo kiongozi huyo atazuru katika ziara itakayoanza Juni 26 hadi Julai 2. Nchi nyingine ni Senegal na Afrika Kusini.
Ziara za kiongozi huyo na Bush, inafanya Tanzania mwaka huu kushuhudia ugeni wa watu mashuhuri mfululizo, baada ya Rais Xi Jiping wa China Machi 28, ambapo Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza kutembelea Afrika tangu achaguliwe kuwa Rais Machi 14.
Amani, utulivu na uimara wa mfumo wa demokrasia  ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuvutia viongozi hao wa kimataifa kuja nchini.
Wapo  wengine ambao katika maoni yao juu ya ujio wa viongozi hao, wamekuwa wakisema ugunduzi wa rasilimali za asili kama vile gesi, mafuta na madini ya urani ni sababu nyingine ya Tanzania kutembelewa.
Hata hivyo, Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt alikaririwa hivi karibuni akifafanua, kwamba ziara ya Obama haina ajenda yoyote ya kuchukua rasilimali za Tanzania, bali ni ya uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo.
 
Source:CCM Social media.

WIZARA YA AFYA - APPLICATION FORM FOR PRE-SERVICE COURSES 2013/2014.

SCHOLARSHIPS UNIVERSITY OF BREMEN - GERMAN 2013/2014.

University of  Bremen offers postdoctoral positions for German as well as international researchers in Germany. Post-doc positions are offered in two different variants: early career postdoctoral positions for a period of two years and independent postdoctoral positions for a period of four years. Career coaching and intensive counseling prepares the post-docs for their next career step. Early career postdoctoral positions offer the opportunity to face up to the scientific competition and to secure further external funding within two years. The advanced post-docs should set up new research groups by acquiring third-party-funding and gain the qualifications necessary for a scientific career as a professor. The number of positions available is shared equally between the natural and engineering sciences and the social sciences and humanities. The application deadline is 1st September 2013.
Study Subject(s): Post-doc positions are available in the areas of  the natural and engineering sciences and the social sciences and humanities. The number of positions available is shared equally between these areas.
Course Level: Positions are available for pursuing postdoctoral degree level: Early Career Postdoctoral Positions and Independent Postdoctoral Positions  at University of Bremen.
Scholarship Provider: University of Bremen, Germany

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...