Wednesday, March 8, 2017

TADB, BODI YA NYAMA KUWAWEZESHA WADAU WA UFUGAJI WA NG’OMBE

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (Kulia) akiwakaribisha maafisa kutoka Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) walipomtembelea Ofisini kwake kujadiliana juu ya Mkutano Mkuu wa Wadau wa Bodi ya Nyama utakaofanyika mkoani Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 9 Machi, 2017. Kushoto ni Afisa Masoko na Utafiti, Bw. Nicholai Chiweka na Afisa Sheria, Bw. Praisegod Lukio (katikati).

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) zimejidhatiti kusaidia mnyororo wa thamani wa ufugaji wa ng’ombe wa nyama na maziwa ili kuongeza tija kwenye sekta ya ufugaji wa ng’ombe nchini.
Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga na Afisa Masoko na Utafiti, Bw. Nicholai Chiweka kutoka TMB wakati wa majadiliano kuhusu Mkutano Mkuu wa Wadau wa Bodi ya Nyama utakaofanyika mkoani Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 9 Machi, 2017.

Mashirika ya TGNP Mtandao ,Oxfam na Care International yaungana katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani.

Mkurungezi wa TGNP  Lilian Liundi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza uzinduzi wa kauli mbiu ya ya mwaka huu "Kuwa Jasiri, PingaUkatili Dhidi ya Wanawake” Katika kuadhamisha siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi ambapo  maadhimisho hayo yatafanyika kimkoa  katika viwanja vya MwembeYanga Temeke Jijini Dar es salaam, Pembeni yake kushoto ni Mkuu wa kitengo cha ushawishi Oxfam Eluka Kibona ,na kulia ni  Mkurungezi wa  wanawake wa Basketball Dar es salaam Bainasi Wamunza na mwishoni ni Makamu mwenyekiti wa Chaneta Bi Zainab Mbiro 





Mkuu wa kitengo cha ushawishi Oxfam  Eluka Kibona akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari wakati wa kutangaza uzinduzi wa kauli mbiu ya ya mwaka huu "Kuwa Jasiri, PingaUkatili Dhidi ya Wanawake” Katika kuadhamisha siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi ambapo  maadhimisho hayo yatafanyika kimkoa  katika viwanja vya MwembeYanga Temeke Jijini Dar es salaam,Kulia kwake ni Mkurungezi wa TGNP  Lilian Liundi.


Wawikilishi kutoka mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Oxfam nchini Tanzania, Care International na TGNP Mtandao wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa   ya mwaka huu "Kuwa Jasiri, PingaUkatili Dhidi ya Wanawake” Katika kuadhamisha siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi ambapo  maadhimisho hayo yatafanyika kimkoa  katika viwanja vya MwembeYanga Temeke
 Jijini Dar es salaam,

Waandishi wa habari wakichukua habari katika mkutano huo uliofanyika katika makao makuu ya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar-Es-Salaam kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Oxfam nchini Tanzania, Care International na TGNP Mtandao, kwa pamoja  tunaandaa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kwa mwaka 2017. Siku ya wanawake duniani kote huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 ya mwezi Machi. Tunaadhimisha siku hii maalumu kila mwaka ili kusherekea, kuheshimu, kukubali na kutambua mchango na mafanikio ya wanawake duniani kote katika kuinua na kuendeleza nyanja mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kijamii. Siku hii pia inatumika kutathmini na kutafakari changamoto anazokabiliana nazo mwanamke katika Nyanja zote muhimu za maisha yake.


Kila mwaka maadhimisho haya yanakuwa na dhima maalum ambako kidunia dhima ni “Kuwa Jasiri kuleta Mabadiliko” wakati dhima ya kitaifa ni “Tanzania ya Viwanda, Wanawake ni Msingi wa Mabadiliko  ya kiuchumi”.  Sambamba na dhima hizi sisi kama taasisi zinazohusika na masuala ya haki za wanawake na usawa wa kijinsia nchini, tunaamini kwamba ukatili wa kijinsia ni moja ya vikwazo vikubwa kwa wanawake vinavyowakwamisha kuchangia kikamilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo kushika nafasi za maamuzi na kumiliki rasilimali.  Ukatili wa Kijinsia hauwezi kuisha bila madadiliko makubwa katika maisha yetu ya kila siku, mila na tamaduni zetu pamoja na sera na sheria zetu. Ni kwa muktadha huo tumekuja na kauli mbiu isemayoni, “Kuwa Jasiri, Pinga Ukatili Dhidi ya Wanawake”.
Kaulimbiu hii inalenga kuhamasisha jamii, serikali na makundi mbalimbali na mtu mmoja kuchukua hatua katika kuzuia na kudhibiti ukatili dhidi ya wanawake. Ikumbukwe kuwa wanawake ambao ni zaidi ya asilimia 50 ya watanzania wote, wamekuwa wakikosa nafasi na sauti  ya kufanya maamuzi kutokana na mifumo kandamizi kwenye jamii zetu ukiwemo mfumo dume. Tunaamini na kutoa wito kwa wadau mbalimbali kusimama kwenye nafasi zao kupinga aina zote za ukatili kwa wanawake na watoto wa kike ikiwemo ndoa za utotoni ambazo bado ni changamoto na zimeongezeka kwa 4% kutoka 23% 2010 mpaka 27% 2015, huku wasichana 36 kati ya 100 wakipata mimba katika umri mdogo, rushwa ya ngono na aina nyingine za ukatili ambazo zinamzuia mwanamke na mtoto wa  kike kufikia ukombozi wa kiuchumi.
Ni dhahiri kwamba suala la kupinga ukatili wa kijinsia linahusisha rasilimali kwa kiasi kikubwa. Pamoja na juhudi za serikali kuandaa na kuzindua Mkakati wa kitaifa wa kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto mnamo mwezi Disemba mwaka 2016, tunatoa wito kwa watendaji hususan ngazi ya Halmashauri kuhakikisha fedha zinatengwa na kuelekezwa katika kutekeleza mkakati huo kama ilivyoelekezwa na Waziri wa  Fedha Mh. Philp Mpango wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati huo.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa kwa mwaka huu yatafanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga vilivyopo Temeke  kwa kukusanyika katika viwanja hivyo kuanzia saa 1:30 asubuhi na kisha kufuatiwa na maandamano mafupi ya amani yatakayofanyika katika viwanja hivyo hivyo vya Mwembe Yanga. Mkusanyiko huo utahusisha wimbo mfupi na ugawaji wa vipeperushi kwa washiriki watakaohudhuria. Mgeni rasmi katika shughuli hii anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Tunachukua fursa hii kuwapongeza wanawake wote Tanzania na kuwatia moyo katika kupigania haki na usawa wa wanawake.



      

Tuesday, February 28, 2017

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa afungua mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma leo Ikulu- Jijini Dar es Salaam

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba yake ya ufunguzi katika mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam mapema leo. Mkutano huo uliandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Takwimu zinazoonesha hali ya uzazi salama Nchini Tanzania




Monday, February 27, 2017

WANACHAMA PSPF SASA RASMI KUPATA MIKOPO KUPITIA BENKI YA CRDB

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, (kushoto), akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dkt. Charels Kimei, wakati wa uzinduzi wa ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili ambapo CRDB sasa itawakopesha Wanachama wa PSPF kwenye maeneo ya elimu, viwanja na pesa za kuanzia maisha kwa watumishi wa serikali. Uzinduzi huo umefanyika Februari 27, 2017 makao makuu ya PSPF jijini Dar es Salaam.

HABARI PICHA - WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA AZINDUA KONGAMANO LA WADAU WA SUA NA KUTEMBELEA BANDA LA TADB

Kaimu Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA), Prof. Deogratias Lutatora (Kushoto) na Mkuu wa Chuo cha Kilimo, Prof. Susan Nchimbi-Msolla (Wapili Kushoto) wakimuongoza Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (Mwenye tai nyekundu) kufungua Kongamano la Wadau la SUA. Kushoto kwa Mhe. Pinda ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe.

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (Katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Wadau la SUA mara baada ya kufungua Kongamano hilo. Wengine waliokaa ni  Kushoto kwa Mhe. Pinda ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe. Kaimu Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA), Prof. Deogratias Lutatora (Kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe (Kulia).

Friday, February 17, 2017

RED CROSS YAKABIDHI KADI ZA UANACHAMA IDARA YA MAAFA

Rais wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania Bw. Mwadini Jecha (katikati) akiweka saini kitabu cha wageni Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu walipotembelea Idara hiyo na kukabidhi Kadi za Uanachama kwa Idara  hiyo, tarehe 16 Februari, 2017.

Wednesday, February 15, 2017

ACACIA, UDSM INKS MOU TO IMPROVE ENGINEERING INDUSTRY IN THE COUNTRY


Vice Chancellor of the University of Dar es Salaam, Professor Rwekaza Mukandala, (L), and Deo Mwanyika, (R) , who is Acacia Vice President (Corporate Affairs), exchange documents after they had signed at the University’s Mlimani campus in Dar es Salaam late on Tuesday. The University of Dar es Salaam (UDSM) has signed a renewed Memorandum of Understanding (MoU) with Acacia Mining that would support 52 students and staff in various areas hence to improve quality of engineering sector. Right is Acacia's Chief Advisor, Learning and Training, Jannet Reuben Lekashingo, and UDSM's Acting Secretary to Council and Corporate Counsel 
who is also, the Intellectual Property Manager,
Dr. Saudin Mwakaje.
 K-VIS BLOG/Khalfan Said

<!--[if gte mso 9]>

JOB VACANCIES - SUA

Sunday, February 12, 2017

JOB VACANCIES - SUZA

LIST OF SUCCESSFUL LOAN APPELLANTS 2016/2017

The Higher Education Students’ Loans Board wishes to announce successful loan appellants. List of students is attached below.
Details of the loan allocations will be available in their respective institutions by end of 13th February, 2017.
Issued by:
EXECUTIVE DIRECTOR
HIGHER EDUCATION STUDENTS’ LOANS BOARD
11th February, 2017.

Saturday, February 11, 2017

HABARI PICHA: KUHAMIA KWA SERIKALI MAKAO MAKUU DODOMA

OFISI ZA MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA NDANI YA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
Serikali katika kutekeleza agizo la Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr. John P. Magufuri kuwa ofisi zote za serikali zinatakiwa kuhamia Dodoma, na kufuatia Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa ilishahamia Dodoma, Wizara zingine zimeshahamia Dodoma ikiwa ni pamoja na Wizara ya Katiba na Sheria, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora ambazo ofisi zao ziko ndani ya Chuo Kikuu cha Dodoma.

Friday, February 10, 2017

UTEUZI WA KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA PAMOJA NA KAMISHNA MKUU WA UHAMIAJI


TADB YAANZA KUTEKELEZA MKATABA WA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA MOROCCO

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki Maendeleo ya ya Kilimo Tanzania Bw. Francis Assenga (Katikati) Akiva Kwenye Kupamba Ukuta ya Pamoja baada ya viongozi wa Mikopo Agricole baada Tamwil El Fellah Wakati walipokagua Miradi mbalimbali ya Kilimo baada ya ufugaji katika vijiji Vya MJI wa Khemisset nchini Morocco jana. Kulia Kabisa nai Bw. Albert Ngusaru ambaye Mkurugenzi nai wa wa Hazina baada ya Utafutaji Fedha TADB.


Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) has ilianza kutekeleza kwa vitendo Mkataba wa Ushirikiano wa saini kati ya Serikali ya Tanzania na Morocco wakati wa ziara ya Mfalme wa ziara Morocco Mtume Mohammed VI wa Tanzania kwa mwaliko wa jeshi Rais wa Jamhuri ya Tanzania , Mhe. Dk John Magufuli Bia katika Oktoba 2016.

Wednesday, February 8, 2017

WAZIRI MHAGAMA: VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA NI YETU SOTE

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akijibu hoja za wabunge mbalimbali waliochangia wakati wa kujadili Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Ukimwi Bungeni Dodoma.

Na mwandishi wetu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amesema kuwa mapambano ya kukabiliana na tatizo la Dawa za Kulevya ni jukumu la kila mwananchi na wala sio suala la kuiachia Serikali peke yake.

Ameyasema hayo bungeni jana wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia juu ya Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya UKIMWI na Dawa za Kulevya iliyoibua maswali kwa Serikali kuendelea kupambana na wanaoshiriki katika biashara haramu ya dawa za kulevya nchini.


Monday, February 6, 2017

ORODHA YA WADAIWA SUGU WA BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU HII HAPA.

Kupata majina ya wadaiwa sugu wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu  bofya "link" ya hapo chini
Bofya hapa (Click here)

SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA AJIRA KWA VIJANA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwasilisha hoja katika mkutano wa Tano wa Bunge linaloendelea Mjini Dodoma.
Na mwandishi wetu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amesema kuwa Serikali imejipanga kusaidia vijana kutambua na kuchangamkia fursa mbalimbali za ajira zilizopo nchini ili kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira na  kutimiza adhma ya kuleta maendeleo hususani kwa vijana.

Mhe. Mhagama ameyasema hayo jana wakati akijibu hoja ya Mbunge wa Kinondoni Mhe. Maulid Mtulia iliyohoji juu ya jitihada za Serikali katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana wakati wa Mkutano wa Tano wa Bunge unaoendelea Mkoani Dodoma.

Katika Mkutano huo Mhe. Waziri alisisitiza kuwa Serikali ina mipango na mikakati madhubuti inayokusudiwa yakusaidia vijana wa Kitanzania ili kujiletea maendeleo yao wenyewe na kuondokana na umasikini.

Saturday, February 4, 2017

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...