Thursday, December 4, 2014

KIWANJA CHA NDEGE CHA KIGOMA KUTANULIWA

Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakionesha eneo lililoainishwa na kufanyiwa tathmini kwa ajili ya kazi ya utanuzi wa Kiwanja hicho.
Na Saidi Mkabakuli, Kigoma
Serikali imeazimia kuanza kufanya utanuzi wa Kiwanja cha Ndege Kigoma ili kuweza kukidhi mahitaji yanaongeza siku baada ya siku ya kiwanja hicho.
Azma imetolewa na Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya miundombinu katika Uwanja wa Ndege wa Kigoma.
Bibi Mwanri alisema kuwa serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini ipo kwenye mkakati wa kuuendeleza uwanja huo ili uwe wa kiwango kizuri kwa kuhudumia watumiaji wa wa kiwanja hicho.
“Kama munavyokumbuka Serikali katika mwaka ujao wa fedha imepanga kuendeleza na kuboresha miundombinu ya usafiri wa anga ili kuongeza ufanisi; na kuendelea na kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege katika maeneo ya kimkakati ikiwamo Kiwanja cha Ndege cha Kigoma,” alisema.

Tuesday, December 2, 2014

JOB VACANCIES - ARUSHA INTERNATIONAL CONFERENCE CENTRE

The Arusha International Conference Centre (AICC) was established under the Public Corporations Act No. 17 of 1969 by a Presidential Order through Government Notice number 115, published on 25th August, 1978. The Centre is wholly owned by the Government of United Republic of Tanzania and operates under the purview of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.
The AICC was established to manage and control the Headquarters’ complex of the defunct East African Community in Arusha which belonged to the defunct East African Community. It also owns Julius Nyerere International Convention Centre as per Arusha International Conference Centre (Amendment) Order of 2014, dated 19th March, 2014; and provide facilities and services on the complex for purposes of conferences, meetings, seminars etc.
The Centre invites applications from suitably qualified Tanzanians to fill in the below mentioned vacant posts:-

1. CUSTOMER RELATIONS OFFICER II (ONE POST)

Answerable to Senior Customer Relations Officer

Qualifications

  • Holder of a Bachelor Degree/Advanced Diploma in Journalism, Public Relations, Mass Communication, or any degree in Social Sciences with a major in communication from a recognized University/Institution.
  • At least three (3) years working experience
  • Must be computer literate

Duties & Responsibilities

KUKAMILIKA KWA UKARABATI WA UWANJA WA NDEGE MPANDA, WAASWA KUTUNZA MIUNDOMBINU.

Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakipata maelekezo ya uendelezaji wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda kutoka kwa Meneja wa uwanja huo, Bw. Seneti Lyatuu (Kushoto).
Na Saidi Mkabakuli, Mpanda
Kufuatia kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda, mkoani Katavi, Serikali imewaasa watumiaji wa uwanja huo kutunza miundombino ya uwanja huo ili kuweza kuhudumia wakazi na wageni wapitao uwanjani hapo kwa muda mrefu.
Wito huo umetolewa na Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya miundombinu katika Uwanja wa Ndege wa Mpanda, mkoani Katavi.
Bibi Mwanri alisema kuwa serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege imekamilisha kazi ya kuufanya uwanja huo uwe wa kiwango kizuri tayari kwa kutumika kwa ndege za binafsi na biashara, hivyo uongozi wa uwanja huo hawana budi ya kuhakikisha miundombinu ya uwanja huo inatunzwa ipasavyo.
“Kama munavyofahamu Serikali imekuwa ikiwekeza sana katika uendelezaji wa miundombinu ya usafiri nchini hasa kuendelea kuboresha miundombinu ya usafiri wa anga ili kuongeza ufanisi na kuendelea na kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege katika maeneo ya kimkakati, hivyo kuna haja ya kuunga mkono jitihada hizi za Serikali,” aliasa Bibi Mwanri.
Akitoa taarifa ya uendelezaji uwanja huo kwa msafara wa timu ya ukaguzi, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda, Bw Seneti Lyatuu alisema uwanja huo umeboreshwa na hivyo, unaweza kutumika kutua na kuruka ndege za kiwango cha kati na hata zile ndege kubwa zinaweza kutua kwa dharura.
“Uwanja huu umekarabatiwa na barabara ya kuruka na kutua ndege imerefushwa kwa kiwango cha lami kutoka urefu wa mita 1,500 na upana wa mita 30 hadi kufikia urefu wa mita 1,820 na upana wa mita 30,” alisema Bw. Lyatuu.

JOB VACANCIES - TANZANIA POSTAL BANK.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...