Wednesday, April 16, 2014

NAFASI ZA KAZI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MAGAZETI YA MWANANCHI NA DAILY NEWS.


PERSONAL  SECRETARY  III - 2 POSITIONS
Qualifications: Holder of Secondary Education Certificate who has attained a Certificate in Secretarial Duties stage  III, having a minimum shorthand speed of 100/120 w.p.m and pass in basic computer skills
Apply: Chief Government Chemist,Government Chemist Laboratory Agency
P. O. Box 164,Dar es Salaam
Details: Daily News, 9 April 2014
Deadline: 23 April, 2014

LOAN SUPERVISOR
Qualifications: University degree in Economics, Accounting,
Business Administration
Apply: The Chief Executive Officer,Visionfund Tanzania
P. O. Box 1546,Arusha
Details: Daily News, 9 April 2014
Deadline: 10 May, 2014

BRANCH MANAGER
Qualifications: University degree in Economics, Accounting,
Business Administration
Apply: The Chief Executive Officer,Visionfund Tanzania
P. O. Box 1546,Arusha
Details: Daily News, 9 April 2014
Deadline: 10 May, 2014

MAINTENANCE TECHNICIAN II
Qualifications: Holders of Full
Technician Certificate (FTC) in Electrical Engineering from
recognized institutions
Apply: Director General,
Tanzania Bureau of Standards,
P. O. Box 9524,Dar es Salaam
Details: Mwananchi, 9 April 2014
Deadline: 22 April, 2014

UFAFANUZI ZAIDI KUHUSU MATANGAZO YA KAZI - UTUMISHI.

Waombaji wa fursa za ajira Serikalini kupitia Sekretarieti ya Ajira wametakiwa kuweka kumbukumbu sahihi za matangazo ya kazi wanazoziomba ili kurahisisha kujua ni tangazo gani aliomba pindi matangazo ya kuitwa kwenye usaili yanapotolewa.
Hayo yamesemwa  na  Bw. Lucas Mrumapili ambae ni  Naibu Katibu wa Idara ya Ajira katika Sekretarieti ya Ajira wakati akitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wasailiwa waliofika  ofisini kwake ili kujua majina ya kuitwa kwenye usaili wa nafasi za kazi za PPRA utafanyika lini.
Akijibu swali hilo alisema kuwa ofisi yake imejipanga vyema kuhakikisha kila tangazo linalotolewa usaili wake unafanyika kwa wakati. Hivyo kuwataka waombaji wa fursa za ajira kuwa wavumilivu wakati mchakato huo ukiendelea, ambapo alitolea ufafanuzi wa usaili wa matangazo husika akianzia tangazo la kazi la tarehe 28 Desemba, 2013 ambalo mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 14 Januari, 2014 kuwa usaili wake utafanyika mwisho mwa mwezi Aprili mwaka huu.
Mrumapili amesema kwa tangazo la tarehe 30 Desemba, 2013 ambalo mwisho wa kupokea maombi ilikuwa tarehe 13 Januari, 2014 kuwa mchakato wake bado unaendelea kutokana na kuhitaji uchambuzi wa kina kwa kila kada maana baadhi ya waombaji kazi  wa tangazo hilo kujirudia zaidi ya mara mbili.

Breaking news: MELI YAZAMA

Meli yenye abiria 450 wengi wao wakiwa wanafunzi imezama karibu n Pwani ya Korea Kusini usiku wa kuamkia leo. Watu 56 wameokolewa mpaka sasa.
Kwa habari zaidi juu ya tukio hili endelea kutembelea blogu hii.

Tuesday, April 15, 2014

VACANCY - TUMAINI UNIVERSITY MAKUMIRA KILIMANJARO CHRISTIAN MEDICAL UNIVERSITY COLLEGE.

Mke wa Rais wa Kenya aweka historia London, akimbia mbio za Marathon.


Mama Margaret Kenyatta mke wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, amekuwa mwanamke wa kwanza mama wa taifa kushiriki mbio za London Marathon na kumaliza mbio hizo.
Alishangiliwa na wakenya wanaoishi nchini Uingereza alipomaliza mbio hizo za kilomita 42 kwa muda wa saa saba na dakika nne siku ya Jumapili.
Bi Kenyatta akilakiwa na mumewe Rais Uhuru Kenyatta

Bi Kenyatta alishiriki mbio za London Marathon kama sehemu ya mradi wake wa kuchangisha pesa za kuwasaidia wanawake wajawazito kujifungua katika mazingira salama na kuhakikisha kuwa watoto wao pia wanaishi nchini Kenya.Mama Margaret alilakiwa na Rais Kenyatta pamoja na waandalizi wa mbio hizo mjini London mwishoni mwa mbio huku akiwapa motisha wakenya na jamii ya kimataifa kwa kuwa mke wa kwanza wa rais kuwahi kushiriki mbio hizo.
Lengo lake kuu ni kupunguza idadi ya vifo vya wanawake wajawazito na watoto wachanga.
Wanawake wengi na watoto wachanga nchini Kenya hupoteza maisha yao wakati wa kujifungua kutokana na ukosefu wa huduma salama na sasa mama Kenyatta amejitwika jukumu la kuwapa akina mama wajawazito uwezo wa kujifungua salama.
Bi Kenyatta alikuwa na kikundi cha wasaidizi 8 waliokuwa naye hadi alipofika mwishoni mwa mbio hizo.
Wakenya kutoka sehemu mbali mbali uingereza walifika mjini London kushuhudia Bi Kenyatta akikamilisha mbio hizo.
Wakenya ndio walioshinda mbio hizo upande wa wanawake na wanaume.
Wilson Kipsang aling'aa upande wa wanaume kwa kuweka rekodi mpya ya saa mbili na dakika nne. Kipsang alifuatiwa na mkenya mwenzake Stanley Biwott.
Kwa upande wa wanawake, Edna Kiplagat alishikilia nafasi ya kwanza akifuatiwa na mkenya mwenzake Florence Kiplagat

Chanzo : BBC

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA HATI YA MUUNGANO.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiowaonesha waandishi wa habari hati halisi ya Muungano ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni (picha na Freddy Maro)

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS 

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE, 
P.O. BOX 9120, 
DAR ES SALAAM.
Tanzania. 
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Fax: 255-22-2113425 




TAMKO LA KATIBU MKUU KIONGOZI KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU HATI YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR IKULU, DAR ES SALAAM, TAREHE 14 APRILI, 2014
______________________________ ____________________ 


Siku 12 zijazo tutasherehekea miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wamezaliwa watu ndani ya Muungano huu na wengine wana wajukuu. 

Inasikitisha sana kuwa leo, miaka 50 baadaye ipo dhana potofu inayojengwa kuwa Muungano huu si halali kwa vile hakuna Hati ya Muungano (Articles of the Union). 


Waasisi wa Taifa letu ambao tarehe 22 Aprili, 1964 kule Zanzibar walitia saini Hati hiyo, mbele ya mashuhuda, nao wameonekana kama walichokifanya kilikuwa kiini macho, na kwa hiyo kwamba waliongoza Taifa jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa msingi wa kiini macho hicho kwa miaka yote hadi Mwenyezi Mungu alipowaita.

Monday, April 14, 2014

Madaktari wakuza 'uke' katika maabara.

Ni mara ya kwanza kwa uke wa mwanamke kukuzwa katika maabara

Madaktari nchini Marekani wamefanikiwa kuwatengezea wanawake wanne sehemu ya uke kwa njia ya kisayansi.
Walitumia mfano wa seli ya uke na mifupa ya mwili kuweza kukuza uke huo katika maabara kwa kuzingatia wastani na umbo la kila mwanamke.
Baada ya matibabu hayo, wanawake hao wote inaarifiwa walielezea kupata hisia sawa na kamilifu,matamanio, kuridhishwa wakati wa tendo la ndoa pamoja na kutopata maumivu yoyote wakati wa tendo la ndoa.

ALICHOSEMA ZITTO KABWE JUU YA SERIKALI 2 AU 3.


Kuna ambao wanaamini kabisa kwamba kuifukua Tanganyika ndani ya Muungano kutavunja Muungano na hivyo wanataka S2 ziboreshwe. Kuna ambao wanataka S2 kwa kufuata mkumbo tu na kwamba ni 'sera' ya chama chao. 
Kuna ambao wanaamini kabisa kwamba S3 ndio njia ya kuimarisha Muungano na kuufanya endelevu kwa kuweka uwazi katika muundo wa Muungano na usawa wa Washirika. Kuna ambao S3 ni njia ya kutokea kuelekea kuvunja muungano maana ama hawaamini katika muungano au hawana itikadi yeyote (ideological bankruptcy).
Wanaong'ang'ania S2 wakidhani wanalinda Muungano watambue kuwa wanawapa nguvu S3 wanaotaka kuvunja muungano.
Ni busara na maono ya mbali kwamba wale wanaoupenda Muungano ( ideologically clear people) kuhakikisha S3 zenye Serikali imara ya muungano. Usipotaka mabadiliko, mabadiliko yatakutaka. Tafakari


Chanzo: Zitto social media.

Call for Conference Papers - UDSM.

Invitation to National Occupational Safety and Health Course (NOSHC) MODULE TWO

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...