Sunday, October 1, 2017

CAAL FOR INTERVIEW - UDOM

KITUO KIPYA CHA KIMAREKANI CHAZINDULIWA MAKTABA KUU YA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM

Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Inmi Patterson na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella Manyanya, wakikata utepe katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Kituo Kipya cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu jijini Dar es Salaam Ijumaa hii. Hafla hii ilihudhuriwa pia na Mkurugenzi Mkuu wa Maktaba nchini, Dk. Alli Mcharazo.



Muonekano kituo  Kituo Kipya cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu jijini Dar es Salaam Ijumaa hii

Muonekano kituo  Kituo Kipya cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu jijini Dar es Salaam Ijumaa hii




 Naibu waziri wa Elimu na Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella Manyanya akihutuba katika uzinduzi wa kituo cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa kushirikiana na Ubalozi wa  Marekani nchini Tanzania pamoja na serikali ya Tanzania. 

kikundi cha Ngoma kikisherehesha wakati wa uzinduzi wa kituo  hicho mapema jana.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi rasmi wa Kituo Kipya cha Kimarekani wakifuatilia kwa karibu hotuba zilitotolewa na wazungumzaji wakuu wa sherehe hizo jijini Dar es Salaam Ijumaa hii. Kituo hicho cha Kimarekani kimeanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Injia Stella Manyanya ndiye alikuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Dk. Inmi Patterson na Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Maktaba nchini, Dk. Alli Mcharazo.

Tuesday, August 22, 2017

ZAMBI APIGIA DEBE UWEZESHAJI WA KILIMO CHA UFUTA NA MIHOGO

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi (hayupo pichani) wakati walipomtembelea ofisini kwake mjini Lindi.

Na Mwandishi wetu, Lindi
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi ameiomba Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kukopesha wakulima wa mazao ya ufuta na mihogo ili waweze kulima kilimo cha kisasa na cha kibiashara hasa kwa wakulima wadogo wadogo wa mkoani humo.
Bw. Zambi alitoa wito huo wakati wa mkutano wa Wadau wa Korosho na Ufuta Mkoa wa Lindi uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Bw. Zambi alisema kuwa mkoa wa Lindi ni mkoa uliojaaliwa katika kuzalisha mazao ya ufuta na mihogo lakini changamoto kubwa ni mtaji wa kulima kibiashara ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.
“Wakulima wa mkoa wa Lindi wapo tayari kushiriki katika kuleta mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara lakini kwa sasa suala la mtaji wa kilimo cha kibiashara ni changamoto kubwa,” alisema Bw. Zambi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga alisema kuwa Benki ya kilimo ipo tayari kutoa mikopo kwa wakulima wadogo wadogo waliokuwa kwenye vikundi ili waweze kukopeshwa.

Saturday, March 18, 2017

SERIKALI MTANDAO;TANAPA INAVYOTUMIA TEHAMA KUTOA HUDUMA ZAKE KWA UMMA

Huu ni mfululizo wa  vipindi vya Serikali Mtandao hapa utaona kwa namna gani TANAPA inavyotumia TEHAMA katika utoaji huduma kwa umma.


Friday, March 10, 2017

VACANCIES ANNOUNCEMENT - PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT

UTUMISHI by Rashid Bumarwa on Scribd

EMPLOYMENT OPPORTUNITIES - TANZANIA PORTS AUTHORITY

SCHOLARSHIPS TENABLE IN THAILAND 2017/2018.

VACANCY - CREDIT OFFICER (TPB)

VACANCY - ASS. BRANCH MANAGER (TPB)

VACANCY - CREDIT SUPERVISOR (TPB)

VACANCIES - OPERATIONAL RISK AND COMPLIANCE MANAGER (TPB)

JOB VACANCIES - RECEPTIONIST (TPB)

VIDEO;Utekelezaji wa Serikali Mtandao EP 01

Hiki ni  kipindi cha Utekelezaji wa Serikali Mtandao nchini kinachotoa elimu kwa umma jinsi Serikali mtandao ilivyorahisisha utendaji kazi kwa Taasisi za Serikali na utoaji huduma kwa umma kupitia mtandao.



Wednesday, March 8, 2017

TADB, BODI YA NYAMA KUWAWEZESHA WADAU WA UFUGAJI WA NG’OMBE

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (Kulia) akiwakaribisha maafisa kutoka Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) walipomtembelea Ofisini kwake kujadiliana juu ya Mkutano Mkuu wa Wadau wa Bodi ya Nyama utakaofanyika mkoani Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 9 Machi, 2017. Kushoto ni Afisa Masoko na Utafiti, Bw. Nicholai Chiweka na Afisa Sheria, Bw. Praisegod Lukio (katikati).

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) zimejidhatiti kusaidia mnyororo wa thamani wa ufugaji wa ng’ombe wa nyama na maziwa ili kuongeza tija kwenye sekta ya ufugaji wa ng’ombe nchini.
Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga na Afisa Masoko na Utafiti, Bw. Nicholai Chiweka kutoka TMB wakati wa majadiliano kuhusu Mkutano Mkuu wa Wadau wa Bodi ya Nyama utakaofanyika mkoani Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 9 Machi, 2017.

Mashirika ya TGNP Mtandao ,Oxfam na Care International yaungana katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani.

Mkurungezi wa TGNP  Lilian Liundi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza uzinduzi wa kauli mbiu ya ya mwaka huu "Kuwa Jasiri, PingaUkatili Dhidi ya Wanawake” Katika kuadhamisha siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi ambapo  maadhimisho hayo yatafanyika kimkoa  katika viwanja vya MwembeYanga Temeke Jijini Dar es salaam, Pembeni yake kushoto ni Mkuu wa kitengo cha ushawishi Oxfam Eluka Kibona ,na kulia ni  Mkurungezi wa  wanawake wa Basketball Dar es salaam Bainasi Wamunza na mwishoni ni Makamu mwenyekiti wa Chaneta Bi Zainab Mbiro 





Mkuu wa kitengo cha ushawishi Oxfam  Eluka Kibona akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari wakati wa kutangaza uzinduzi wa kauli mbiu ya ya mwaka huu "Kuwa Jasiri, PingaUkatili Dhidi ya Wanawake” Katika kuadhamisha siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi ambapo  maadhimisho hayo yatafanyika kimkoa  katika viwanja vya MwembeYanga Temeke Jijini Dar es salaam,Kulia kwake ni Mkurungezi wa TGNP  Lilian Liundi.


Wawikilishi kutoka mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Oxfam nchini Tanzania, Care International na TGNP Mtandao wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa   ya mwaka huu "Kuwa Jasiri, PingaUkatili Dhidi ya Wanawake” Katika kuadhamisha siku ya wanawake duniani tarehe 8 Machi ambapo  maadhimisho hayo yatafanyika kimkoa  katika viwanja vya MwembeYanga Temeke
 Jijini Dar es salaam,

Waandishi wa habari wakichukua habari katika mkutano huo uliofanyika katika makao makuu ya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar-Es-Salaam kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Oxfam nchini Tanzania, Care International na TGNP Mtandao, kwa pamoja  tunaandaa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kwa mwaka 2017. Siku ya wanawake duniani kote huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 ya mwezi Machi. Tunaadhimisha siku hii maalumu kila mwaka ili kusherekea, kuheshimu, kukubali na kutambua mchango na mafanikio ya wanawake duniani kote katika kuinua na kuendeleza nyanja mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kijamii. Siku hii pia inatumika kutathmini na kutafakari changamoto anazokabiliana nazo mwanamke katika Nyanja zote muhimu za maisha yake.


Kila mwaka maadhimisho haya yanakuwa na dhima maalum ambako kidunia dhima ni “Kuwa Jasiri kuleta Mabadiliko” wakati dhima ya kitaifa ni “Tanzania ya Viwanda, Wanawake ni Msingi wa Mabadiliko  ya kiuchumi”.  Sambamba na dhima hizi sisi kama taasisi zinazohusika na masuala ya haki za wanawake na usawa wa kijinsia nchini, tunaamini kwamba ukatili wa kijinsia ni moja ya vikwazo vikubwa kwa wanawake vinavyowakwamisha kuchangia kikamilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo kushika nafasi za maamuzi na kumiliki rasilimali.  Ukatili wa Kijinsia hauwezi kuisha bila madadiliko makubwa katika maisha yetu ya kila siku, mila na tamaduni zetu pamoja na sera na sheria zetu. Ni kwa muktadha huo tumekuja na kauli mbiu isemayoni, “Kuwa Jasiri, Pinga Ukatili Dhidi ya Wanawake”.
Kaulimbiu hii inalenga kuhamasisha jamii, serikali na makundi mbalimbali na mtu mmoja kuchukua hatua katika kuzuia na kudhibiti ukatili dhidi ya wanawake. Ikumbukwe kuwa wanawake ambao ni zaidi ya asilimia 50 ya watanzania wote, wamekuwa wakikosa nafasi na sauti  ya kufanya maamuzi kutokana na mifumo kandamizi kwenye jamii zetu ukiwemo mfumo dume. Tunaamini na kutoa wito kwa wadau mbalimbali kusimama kwenye nafasi zao kupinga aina zote za ukatili kwa wanawake na watoto wa kike ikiwemo ndoa za utotoni ambazo bado ni changamoto na zimeongezeka kwa 4% kutoka 23% 2010 mpaka 27% 2015, huku wasichana 36 kati ya 100 wakipata mimba katika umri mdogo, rushwa ya ngono na aina nyingine za ukatili ambazo zinamzuia mwanamke na mtoto wa  kike kufikia ukombozi wa kiuchumi.
Ni dhahiri kwamba suala la kupinga ukatili wa kijinsia linahusisha rasilimali kwa kiasi kikubwa. Pamoja na juhudi za serikali kuandaa na kuzindua Mkakati wa kitaifa wa kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto mnamo mwezi Disemba mwaka 2016, tunatoa wito kwa watendaji hususan ngazi ya Halmashauri kuhakikisha fedha zinatengwa na kuelekezwa katika kutekeleza mkakati huo kama ilivyoelekezwa na Waziri wa  Fedha Mh. Philp Mpango wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati huo.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa kwa mwaka huu yatafanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga vilivyopo Temeke  kwa kukusanyika katika viwanja hivyo kuanzia saa 1:30 asubuhi na kisha kufuatiwa na maandamano mafupi ya amani yatakayofanyika katika viwanja hivyo hivyo vya Mwembe Yanga. Mkusanyiko huo utahusisha wimbo mfupi na ugawaji wa vipeperushi kwa washiriki watakaohudhuria. Mgeni rasmi katika shughuli hii anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Tunachukua fursa hii kuwapongeza wanawake wote Tanzania na kuwatia moyo katika kupigania haki na usawa wa wanawake.



      

Tuesday, February 28, 2017

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa afungua mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma leo Ikulu- Jijini Dar es Salaam

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba yake ya ufunguzi katika mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam mapema leo. Mkutano huo uliandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Takwimu zinazoonesha hali ya uzazi salama Nchini Tanzania




Monday, February 27, 2017

WANACHAMA PSPF SASA RASMI KUPATA MIKOPO KUPITIA BENKI YA CRDB

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, (kushoto), akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dkt. Charels Kimei, wakati wa uzinduzi wa ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili ambapo CRDB sasa itawakopesha Wanachama wa PSPF kwenye maeneo ya elimu, viwanja na pesa za kuanzia maisha kwa watumishi wa serikali. Uzinduzi huo umefanyika Februari 27, 2017 makao makuu ya PSPF jijini Dar es Salaam.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...