Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Wednesday, April 17, 2013
Tuesday, April 16, 2013
ANNOUNCEMENT FOR MASTERS COURSE AT JUCO
Jordan University College
A Constituent College of St. Augustine University of Tanzania
Master of Education
From October 2013 Jordan University College will offer the Master of Education in the
following specializations:
• Curriculum and Instruction
• Educational Assessment and Evaluation
• Educational Planning and Administration
Fees
• Academic & Administrative Fees
(including Registration, Tuition, Library & Examination)
3,600,000
• Thesis Supervision 200,000
Total 3,800,000
• Medical Fee per Academic Year
(payable two times during Masters’ programme)
2 x 100,000
Grand Total (including Medical Fee) 4,000,000
NB: Those who have valid health insurance maybe opt to use the services provided by their health
insurance plan. For all others the medical fee is compulsory!
Fees are payable as follows:
Without
Medical Fee
With Medical
Fee
1st instalment at the beginning of the 1st semester of the 1st academic year
• 1/3 of Academic & Administrative Fees 1,200,000 1,200,000
• Medical Fee per Academic Year 100,000
Total 1st instalment 1,200,000 1,300,000
2nd instalment at the beginning of the 2nd semester of the 1st academic year
• 1/3 of Academic & Administrative Fees 1,200,000 1,200,000
Total 2nd instalment 1,200,000 1,200,000
3rd instalment at the beginning of the 1st semester of the 2nd academic year
• 1/3 of Academic & Administrative Fees 1,200,000 1,200,000
• Thesis Supervision 200,000 200,000
• Medical Fee per Academic Year 100,000
Total 3rd instalment 1,400,000 1,500,000
Pay your fees to:
Jordan University College, A/C No 015 027 752 7900 CRDB, Mandela Branch, Morogoro
Submit original copy of bank deposit slip indicating clearly your name, course and year of study!
For more information,
please contact our Admission Office 0717781455 jordanunivcollege@yahoo.com
and check our webpage morogoro.sds.org & morogoro.sds.org/GInf_admition.html
P.O. Box 1878, Morogoro, Tanzania.
Direct Student’s Cost for Master of Education
For living expenses and other costs like for books, stationeries, and so on, the following
information should be helpful to the students and their sponsors in reaching agreeable
direct student costs (which are payable DIRECTLY to the student and NOT to the
University)
1. An academic year has two semesters, each lasting for 120 days.
2. Accommodation costs are ranging from Tshs 350,000 to Tsh 450,000 for those who
will manage to get chance of accommodation on the college campus and in the
hostels near by the college.
3. Food prise is estimated at Tshs 10,000 – 15,000 per day.
4. Books expenditure is ranging from Tshs 200,000 to 300,000, depending on
sponsor’s financial ability.
5. For research and dissertation costs, students should come up with a breakdown of
what is needed to the accomplishment of research and dissertation and negotiate
with their sponsors on the amount of money they need.
Minimum Entry Requirements for Master of Education
An applicant must satisfy any of the following requirements:
• Holder of a Bachelor Degree in Education and other similar programmes offered like
BEd Maths, Science, Arts, Adult Education, Early Childhood Education, Psychology,
etc. with at least Upper Second Class Honours.
• Holder of a Bachelor Degree in Arts or Science teaching subject with at least Upper
Second Class Honours plus a Postgraduate Diploma in Education.
• Holder of a Bachelor Degree in Education with at least Lower Second Class
Honours plus teaching experience of minimum two years.
• Any equivalent qualification from a recognized university.
Wednesday, March 27, 2013
UTATA WA ELIMU YA NAIBU WAZIRI MULUGO WAZIDI KUZUA MENGI
Imebainika kuwa mmoja wa watu ambao Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo (pichani)anadaiwa kutumia jina lake kutafuta kazi ya ualimu katika Shule ya Sekondari ya Southern mkoani Mbeya ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (Muce), kilichopo mkoani Iringa.
Mhadhiri huyo ni Dick Aron Mulungu ambaye alisoma na Mulugo katika Shule ya Sekondari ya Songea Wavulana kati ya 1994 na 1996 na alijiunga na shule hiyo baada ya kuhitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kafule, ambayo iko mkoani Mbeya.
Taarifa zinaonyesha kuwa Mulungu alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kupata Shahada ya kwanza katika Elimu (BA Education) 2001 na baadaye alisoma na kupata Shahada ya Uzamili (MA Development studies ) 2007.
Alipotafutwa kupitia simu yake ya mkononi, mahojiano yalikuwa hivi:
Mwandishi: Hallow…(mwandishi akajitambulisha)
Mulungu: Sawa, unasemaje?
Mwanishi: Nazungumza na Dick Mulungu?
Mulungu: Ndiyo mimi.
Mwandishi: Hivi unamfahamu mtu anayeitwa Hamimu Agustino?
Mulungu: Aah… hivi ulisema unaitwa nani?
Mwandishi: Si nimeshajitambulisha jina na ofisi ninayotoka?
Mulungu: Nipigie kesho naona hapa kuna kelele.
Mwandishi: Mbona nakusikia vizuri tu?
Mulungu: Nipigie baada ya nusu saa basi.
Baada ya nusu saa…….
Mwandishi: Haloo… naona nusu saa imekwisha, uko tayari kuzungumza?
Mulungu: Huyo simfahamu.
Mwandishi: Kwani wewe si ulisoma Songea Boys?
Mulungu: Ndiyo
Mwandishi: Kwa hiyo humkumbuki mtu aliyekuwa akitumia jina hilo?
Mulungu: Huyo mtu namkumbuka ndiyo.
Mwandishi: Kwa sasa yuko wapi?
Mulungu: Siwezi kujua, si unajua tumesoma siku nyingi sasa huwezi kujua mtu amekwenda wapi… ni siku nyingi mno.
Mwandishi: Ahsante.
Chuo Kikuu na siasa
Taarifa zinaonesha kuwa Waziri Mulugo alijiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania 2002 akitumia majina ya Philipo Hamimu Augustino na alisomea Shahada ya Sanaa katika Elimu (BA. Ed). Namba yake ya usajili chuoni hapo ni 08652/T.02.
Alipokuwa akiendelea na kazi ya ualimu Mulugo alianza harakati za kisiasa na ndipo alipoamua kwenda kugombea ubunge katika majimbo ya wilaya ya Chunya.
Kada wa chama cha NCCR Mageuzi wilayani Chunya, Nyawili Kalenda aliyejitambulisha kama mlezi wa siasa wa Waziri huyo alisema walifahamiana naye 2004 wakati Mulugo na rafiki yake walipokwenda kumtaka ushauri wa kugombea ubunge katika jimbo la Songwe.
Katika nakala za wasifu wake zinaonyesha
kuwa 2008 alishika nafasi ndani ya CCM ambazo ni pamoja na mjumbe wa
baraza la jumuiya ya wazazi wilaya ya Chunya, Katibu wa Elimu, Uchumi,
Malezi na mazingira wa jumuiya ya wilaya hiyo na mjumbe wa baraza la
wazazi mkoa wa Mbeya.
Kauli yake
Mulugo anasema madai hayo yamekuwa yakitolewa mara kwa mara na amekuwa akiyajibu kwa kuwaonyesha vyeti vyake halali vya shule. “Hayo madai ni ya muda mrefu, wewe sijui utakuwa mtu wa 20 kuuliza swali kama hilo. Mimi vyeti ninavyo na hata ukitaka ushahidi nitakuonyesha,” alisema Waziri Mulugo.
Kauli yake
Mulugo anasema madai hayo yamekuwa yakitolewa mara kwa mara na amekuwa akiyajibu kwa kuwaonyesha vyeti vyake halali vya shule. “Hayo madai ni ya muda mrefu, wewe sijui utakuwa mtu wa 20 kuuliza swali kama hilo. Mimi vyeti ninavyo na hata ukitaka ushahidi nitakuonyesha,” alisema Waziri Mulugo.
Licha ya kukiri kurudia darasa la saba, Waziri Mulugo alisema jina la Hamimu amekuwa akilitumia katika elimu tangu awali na kwamba hakuvunja sheria kufanya hivyo.
“Jina la Hamim ni la nyumbani Philipo ni jina langu la ubatizo, nadhani haya ni mambo ya kawaida na kweli nilipokuwa shule watu walikuwa wananifahamu kama Hamimu pia Philipo ni jina langu la ubatizo na kumbuka tukifika chuo huwa tunatumia jina la baba.
“Na pia ni kweli nilirudia shule kwa sababu wakati ule wa Mwalimu Nyerere na Mwinyi (Ali Hassan), sheria ilikuwa inaruhusu maana wanafunzi walikuwa wachache mno, fikiria katika darasa letu la saba tulimaliza watu saba tu. Baadaye sheria hiyo ilibadilishwa,” aliongeza.
Kuhusu jina la Dick Mulungu, alikiri kumfahamu mtu huyo na kwamba walisoma wote shule ya Sekondari ya Songea Boys. Hata hivyo, alipinga kutumia vyeti vyake.
“Ni kweli Dick Mulungu tulisoma wote Songea Boys. Lakini hili jina la Mulungu ni jina letu la ukoo. Babu yangu alikuwa akiitwa Filipo Milambo Mulungu, kwa hiyo niliendelea kulitumia hivyo hivyo na hata jina la Mulugo ni letu pia,” alisema.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa Mwananchi Jumanne,Machi 26,2013.
Thursday, March 14, 2013
RAIS KIKWETE ATEMBELEA CHUO KIKUU CHA WAISLAM CHA MOROGORO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete leo asubuhi ametembelea Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro (MUM)
Jengo la ITC la Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro lililowekwa jiwe la msingi na Rais Kikwete. |
Ziara ya Rais hii leo itaendelea kwa kuelekea Magadu Mesi ambako atafanya halambee ya kuchangisha fedha za kujenga kanisa katoliki la Kigurunyembe.
Tuesday, February 19, 2013
NUSU YA WATAHINIWA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE WAPATA SIFURI
Waziri
wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (MB) leo ametangaza
rasmi matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne, maarifa-QT.
TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA MAARIFA (QT) NA KIDATO CHA NNE (CSEE)
ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012
1.0 UTANGULIZI
Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) kwa mwaka 2012 ilifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8-25 Oktoba 2012. Napenda kuchukua nafasi hii kutangaza rasmi matokeo ya mitihani hiyo kama ifuatavyo :
2.0 MTIHANI WA MAARIFA (QT)
2.1 Usajili na Mahudhurio
Katika Mtihani wa Maarifa 2012 watahiniwa waliosajiliwa ni 21,310 ambapo wasichana walikuwa ni 13,134 na wavulana ni 8,176. Jumla ya watahiniwa 17,137 sawa na asilimia 80.42 ya waliosajiliwa wamefanya Mtihani.
2.2 Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)
2.2 Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)
Watahiniwa 5,984 kati ya 17,137 waliofanya mtihani wamefaulu Mtihani wa Maarifa (QT).
3.0 MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012
Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ambapo vituo 4,155 vilikuwa vya watahiniwa wa shule na vituo 903 vilikuwa ni vya watahiniwa wa kujitegemea.
3.1 Usajili na Mahudhurio ya Watahiniwa
(a) Watahiniwa Wote
Jumla ya watahiniwa 480,036 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wakiwemo wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67. Watahiniwa waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ni 456,137 sawa na asilimia 95.44. Watahiniwa 21,820 sawa na asilimia 4.55 ya watahiniwa wote waliosajiliwa hawakufanya mtihani.
(b) Watahiniwa wa Shule
Watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 411,230 wakiwemo wasichana 182,978 sawa na asilimia 44.50 na wavulana 228,252 sawa na asilimia 55.50. Watahiniwa wa shule waliofanya mtihani walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57. Aidha, watahiniwa 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro, ugonjwa na vifo.
(c) Watahiniwa wa Kujitegemea
Watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa walikuwa ni 68,806 wakiwemo wasichana 34,605 sawa na asilimia 50.29 na wavulana 34,201 sawa na asilimia 49.71. Watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,917 na wavulana 30,084 wamefanya mtihani wakati watahiniwa 7,730 sawa na asilimia 11.23 hawakufanya mtihani.
4.0 MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE
(a) Watahiniwa wa Shule
Jumla ya watahiniwa wa shule 126,847 kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 46,161 na wavulana ni 80,686.
(b) Watahiniwa wa Kujitegemea
Idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 16,112 kati ya watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani. Wasichana waliofaulu ni 6,751 na wavulana ni 9,361.
5.0 UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI
Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 23,520 wamefaulu katika madaraja I – III ambapo kati yao wasichana ni 7,178 na wavulana ni 16,342.Mchanganuo wa ufaulu kwa kila Daraja kwa jinsi kwa Watahiniwa wa Shule mwaka 2012 ni kama ifuatavyo:
Idadi ya Wavulana
|
Idadi ya Wasichana
|
Jumla
|
|
I
|
1,073
|
568
|
1,641
|
II
|
4,456
|
1,997
|
6,453
|
III
|
10,813
|
4,613
|
15,426
|
I-III
|
16,342
|
7,178
|
23,520
|
IV
|
64,344
|
38,983
|
103,327
|
0
|
120,664
|
120,239
|
240,903
|
6.0 SHULE ISHIRINI ZILIZOFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI
Ubora wa ufaulu wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 hadi F = 5. Shule zenye watahiniwa 40 na zaidi ziko 3,391. Shule ya kwanza hadi ya ishirini zimeainishwa kwenye Jedwali lifuatalo :
NAFASI
|
JINA LA SHULE
|
IDADI YA WATAHINIWA
|
MKOA
|
1
|
ST. FRANCIS GIRLS
|
90
|
MBEYA
|
2
|
MARIAN BOYS S.S
|
75
|
PWANI
|
3
|
FEZA BOYS S.S
|
69
|
DAR ES SALAAM
|
4
|
MARIAN GIRLS S.S
|
88
|
PWANI
|
5
|
ROSMINI S S
|
78
|
TANGA
|
6
|
CANOSSA S.S
|
66
|
DAR ES SALAAM
|
7
|
JUDE MOSHONO S S
|
51
|
ARUSHA
|
8
|
ST. MARY’S MAZINDE JUU
|
83
|
TANGA
|
9
|
ANWARITE GIRLS S S
|
49
|
KILIMANJARO
|
10
|
KIFUNGILO GIRLS S S
|
86
|
TANGA
|
11
|
FEZA GIRLS
|
49
|
DAR ES SALAAM
|
12
|
KANDOTO SAYANSI GIRLS SS
|
124
|
KILIMANJARO
|
13
|
DON BOSCO SEMINARY SS
|
43
|
IRINGA
|
14
|
ST.JOSEPH MILLENIUM
|
133
|
DAR ES SALAAM
|
15
|
ST.JOSEPH’S ITERAMBOGO SS
|
64
|
KIGOMA
|
16
|
ST.JAMES SEMINARY SS
|
44
|
KILIMANJARO
|
17
|
MZUMBE SS
|
104
|
MOROGORO
|
18
|
KIBAHA SS
|
108
|
PWANI
|
19
|
NYEGEZI SEMINARY SS
|
68
|
MWANZA
|
20
|
TENGERU BOYS SS
|
76
|
ARUSHA
|
7.0 SHULE KUMI AMBAZO HAZIKUFANYA VIZURI ZAIDI KATIKA KUNDI LA SHULE ZENYE WATAHINIWA 40 AU ZAIDI
NAFASI
|
JINA LA SHULE
|
IDADI YA WATAHINIWA
|
MKOA
|
1
|
MIBUYUNI S.S
|
40
|
LINDI
|
2
|
NDAME S.S
|
41
|
UNGUJA
|
3
|
MAMNDIMKONGO S.S
|
63
|
PWANI
|
4
|
CHITEKETE S.S
|
57
|
MTWARA
|
5
|
MAENDELEO S.S
|
103
|
DAR ES SALAAM
|
6
|
KWAMNDOLWA S.S
|
89
|
TANGA
|
7
|
UNGULU S.S
|
62
|
MOROGORO
|
8
|
KIKALE S.S
|
60
|
PWANI
|
9
|
NKUMBA S.S
|
152
|
TANGA
|
10
|
TONGONI S.S
|
56
|
TANGA
|
8.0 TATHMINI YA UFAULU WA WATAHINIWA WA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012
8.1 Tathmini
ya awali iliyofanyika kuhusu ufaulu wa watahiniwa katika shule
mbalimbali inaonesha kuwa shule zilizofanya vizuri zaidi ni zile ambazo
zina mahitaji yote ya msingi ikiwemo walimu wa kutosha, miundombinu na
vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Aidha, shule zenye ufaulu wa chini
ni zile ambazo zina changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na:
(i) Baadhi ya shule za vijijini hazina kabisa walimu wa masomo ya Sayansi
na Hisabati na pia zina upungufu mkubwa wa walimu wa masomo mengine;
(ii) Kutokuwepo kwa maabara kwa shule zenye mikondo ya sayansi na pia kutokuwepo kwa maktaba kwa ajili ya kujisomea; na
(iii) Upungufu mkubwa wa vitabu vya kiada na ziada. Katika baadhi ya shule uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ni 1:10.
8.2 Mkakati wa Serikali ni kuendelea kupunguza changamoto hizo kila mwaka ikiwa ni pamoja na kufanya mambo yafuatayo:
(i) Kuajiri walimu kila mwaka ili kuondoa upungufu uliopo katika shule zetu. Mwaka 2011/2012 Serikali iliajiri walimu wa sekodari 13,246 na mwaka huu wa fedha 2012/2013 imeajiri walimu 12,973 ambao
wamepangwa katika shule zenye upungufu mkubwa wa walimu. Ajira ya
walimu wapya mwaka huu umetuwezesha kuwa na wastani wa walimu 2-3 kwa shule. Hali hii itaendelea kuboreka kadri tunavyoendela kuajiri walimu.
(ii) Kuboresha miundombinu iliyoko katika shule zetu ikiwa ni pamoja na
kujenga nyumba za walimu, madarasa na maabara. Mwaka 2012/2013 Serikali imepanga kuboresha miundombinu katika shule 264 zilizopo katika mazingira magumu ikiwemo miundombinu ya maabara na nyumba za walimu.
(iii) Kuendelea kutoa ruzuku ya Tsh 25,000 kwa mwanafunzi kwa mwaka, ambapo asilimia 50
ya fedha hizo ni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia na
kujifunzia ili kuziwezesha shule kununua vitabu pamoja na vifaa vingine
muhimu kitaaluma.
(iv) Wizara kuendelea kuzishauri Halmashauri kuweka mgawanyo mzuri wa walimu waliopo baina ya shule na shule.
(v) Wizara itaendelea kuimarisha Idara ya Ukaguzi wa Shule pamoja na
kuwawezesha Waratibu Elimu Kata na Wakuu wa Shule kufanya ukaguzi wa
ndani katika Shule za Sekondari zilizo katika maeneo yao.
9.0 MATOKEO YA MITIHANI YALIYOZUIWA
Baraza la Mitihani la Tanzania limezuia kutoa matokeo ya:
(a) Watahiniwa 28,582 wa
Shule ambao hawajalipa ada ya Mtihani hadi watakapolipa ada wanayodaiwa
pamoja na faini; na ikiwa hawatalipa katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.
(b) Watahiniwa 65 wa kujitegemea na 71
waliofanya Mtihani wa Maarifa (QT) mwaka 2012 bila ya kulipa ada ya
Mtihani hadi watakapolipa ada pamoja na faini. Ikiwa hawatalipa ada hiyo
katika kipindi cha miaka miwili (02) toka matokeo kutangazwa, matokeo yao yatafutwa.
10.0 MATOKEO YA MITIHANI YALIYOFUTWA
10.1 Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Udanganyifu
Jumla ya watahiniwa 789 wamefutiwa matokeo yao yote ya mtihani kwa mujibu wa kifungu Na.52(b) cha Kanuni za Mitihani baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu katika mitihani ya Oktoba 2012. Kati yao, watahiniwa wa shule ni 624 na watahiniwa wa kujitegema ni 148 na watahiniwa wa Mtihani wa Maarifa (QT) ni 17. Aina ya udanganyifu uliobainika na idadi ya watahiniwa husika ni kama ifuatavyo:
S/N
|
AINA YA UDANGANYIFU
|
IDADI YA WATAHINIWA
|
(i)
|
Watahiniwa
kubainika kuwa na skripti zenye miandiko tofauti au kuwa na miandiko
tofauti katika skripti ya somo moja au zaidi ya moja.
|
04
|
(ii)
|
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi ndani ya chumba cha mtihani wakiwa na ‘notes.’
|
170
|
(iii)
|
Watahiniwa kubainika kuwa na mfanano usio wa kawaida wa majibu.
|
590
|
(iv)
|
Watu kukamatwa wakiwafanyia watahiniwa wengine mtihani ‘impersonation”.
|
04
|
(v)
|
Watahiniwa kukamatwa na simu ndani ya chumba cha mtihani.
|
06
|
(vi)
|
Watahiniwa kukamatwa na wasimamizi wakibadilisha karatasi za maswali au skripti kwa lengo la kufanya udanganyifu.
|
15
|
JUMLA
|
789
|
10.2 Matokeo Yaliyofutwa Kwa Sababu ya Watahiniwa Kuandika Matusi Katika Skripti Zao
(i) Jumla ya watahiniwa 24 waliandika matusi kwenye skripti zao za masomo mbalimbali. Kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kifungu 5(13) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:
“Written
responses to any examination question which carry words, drawings or
pictures connected to sex or abusive language in such a way that it
becomes offensive shall consitute an examination offence and a candidate
who commits such an offence shall be punished by the Council.”
Kutokana na kosa hilo Baraza la Mitihani limefuta matokeo yao yote kwa mujibu wa Kifungu cha 6(2)(a) cha Kanuni za Mitihani kinachosomeka:
“A candidate found to have committed an examination offence shall – (a) have his examination results nullified”
(ii)Kitendo cha kuandika matusi kwenye karatasi za majibu (skripti)
kinaonesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu. Serikali haitaweza
kuwavumilia hata kidogo watahiniwa wa aina hiyo. Hivyo, Serikali
itaangalia hatua zaidi za kisheria za kuchukua dhidi ya watahiniwa wote
walioandika matusi.
Kwa mujibu wa kifungu Na. 6(2)(b)
cha Kanuni za Mitihani, watahiniwa wote waliobainika kufanya
udanganyifu katika mitihani au kuandika matusi katika skripti zao
hawataruhusiwa kufanya mitihani inayoendeshwa na Baraza la Mitihani la
Tanzania kwa kipindi cha mwaka mmoja (01) kuanzia tarehe ya kutangazwa kwa matokeo.
11.0 KUANGALIA MATOKEO YA MTIHANI WA CSEE na QT, 2012
(a) Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT), 2012 yanapatikana katika tovuti zifuatazo:
· www.udsm.edu.ac.tz, au
(b) Matokeo yanaweza kupatikana pia kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda namba 15311. Jinsi ya kutuma ujumbe andika:
MATOKEOXNAMBA YA KITUOXNAMBA YA MTAHINIWA
(Mfano : matokeoxS0101x0503)
Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb)
WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
18 Februari 2013
Wednesday, December 12, 2012
SHORT COURSE ON FIRST AID.
INDUSTRIAL FIRST AID COURSE
OSHA has organized the above mentioned course for all nominate first aiders at workplaces or
any one in need of comprehensive introduction to first aid.
Objective of the course: To equip participants with adequate knowledge and practical skills in
dealing with health emergencies at workplaces.
Participants will be able to minimize the outcome of workplace accidents or exposures, along
with enhancing their workplace compliance to First Aid legal requirement.
Course contents:
The First Aid provision as described in OHS act 2003.
Contents/ uses of first aid kit.
Medical emergencies(stroke, asthmatic and diabetic shock, epilepsy)
Accidents and incidents.
Treatment of an unconscious causality (CPR).
Foreign bodies and eye injuries.
Poisoning and allergic reactions.
Burns and scalds.
Fractures and dislocation.
FIRST AID PRACTICAL.
The course will be conducted for three days from 18th – 20th December, 2012 at OSHA
headquarters office Training lounge.
Course fee is Tsh.200, 000/= per participants, this is only for tuition and refreshment during
course. NOTE: Breakfast and lunch will not be provided.
Training methodology: Instruction lectures, plenary session and practical demonstrations.
For more information and booking please contact the following;
Chief Executive Officer, P. O Box 519, Tel +255 22 2760548/2760579
Shaaban Mkindi – 0713 826849, Naanjela Msangi – 0715 424 020
Jamani tuchangamkie course hii.
INDUSTRIAL FIRST AID COURSE
OSHA has organized the above mentioned course for all nominate first aiders at workplaces or
any one in need of comprehensive introduction to first aid.
Objective of the course: To equip participants with adequate knowledge and practical skills in
dealing with health emergencies at workplaces.
Participants will be able to minimize the outcome of workplace accidents or exposures, along
with enhancing their workplace compliance to First Aid legal requirement.
Course contents:
The First Aid provision as described in OHS act 2003.
Contents/ uses of first aid kit.
Medical emergencies(stroke, asthmatic and diabetic shock, epilepsy)
Accidents and incidents.
Treatment of an unconscious causality (CPR).
Foreign bodies and eye injuries.
Poisoning and allergic reactions.
Burns and scalds.
Fractures and dislocation.
FIRST AID PRACTICAL.
The course will be conducted for three days from 18th – 20th December, 2012 at OSHA
headquarters office Training lounge.
Course fee is Tsh.200, 000/= per participants, this is only for tuition and refreshment during
course. NOTE: Breakfast and lunch will not be provided.
Training methodology: Instruction lectures, plenary session and practical demonstrations.
For more information and booking please contact the following;
Chief Executive Officer, P. O Box 519, Tel +255 22 2760548/2760579
Shaaban Mkindi – 0713 826849, Naanjela Msangi – 0715 424 020
Jamani tuchangamkie course hii.
Subscribe to:
Posts (Atom)